Kuhusu kukaribisha wageni chakula

Show umeifanya wewe, mimi huku nimeona aibu.

Itafikia kipindi watu hawatatembeleana, kwa wakazi wa Dar hiyo imeshaanza, ni heri kukutana sehemu neutral na kumaliza mazungumzo kuliko kwenda kwa mtu. Kwanza wengi ni "chumba kimoja" au "viwili", watoto na mke/mume wote wanashare mazingira yaliyo finyu sana, wanasema person per square meters haipo sawa.
 
Na ndivo ilivo,wengi kwasasa wanavizia mda wa kula umepita ndio waje
 
Wewe ni kauzu zaidi ya dagaa
 
Kwa sisi waafrika ni bora mwenyeji usile wageni wale hata kama hawajatoa taarifa.
Tulishawahi kuharibikiwa na gari njiani wenyeji wetu walitupa chakula na malazi bure huo ndio uafrika.

Wewe ni mchoyo.
Hii night zaidi ya uchoyo
 
Mwema kwa mzee wangu sio kwa wageni wa hafla wasiokuwa na mawasiliano.
 
Mwema kwa mzee wangu sio kwa wageni wa hafla wasiokuwa na mawasiliano.
Ina maana kila mara ukipata wageni wa ghafla muda wa msosi utawasema?sometimes tujifunze kumezea vitu vingine
 
Mimi naomba unieleweshe nini maana ya "okoyoko"
 
Ina maana kila mara ukipata wageni wa ghafla muda wa msosi utawasema?sometimes tujifunze kumezea vitu vingine
Maisha ya Dasalama na Mikowani tofauti dada yangu. Nyinyi wakaribisheni mimi sibadilishi msimamo chakula sio shida. Tatizo kuja kwangu bila taarifa tena wakati wa kula. Kwanini asinijuulishe na yeye nikamuwekea plate yake maisha ya dar lazima uwe na budget.
 
Ongeza bidii upate kipato ambacho u never worry mgeni wa ghafla akija atakula nini,..katika milo nliowahi furahia maishani mwangu ni ile niliyoshare na watu wengine
 
sio kiivyo aisee,wewe umezidi
 
Nimewahi kufanyiwa hivyo na watoto wangu,gari iliharibika mahali ikabidi tupigie simu ndugu aliepo karibu hivyo nilibeba watoto wangu walikua wawili by the time nilikua na kimimba kidogo cha miezi miwili,kiukweli majibu hayo yanaumiza,walitujibu fyongo ila kwa bahati mume wangu alikua amenunu mbuzi choma njiani tukiwa tunaenda na ndizi,tulipofika tulikuta chakula kinatayarishwa ila hatukukaribishwa baada ya muda ikaanza lecture lol,basi mume wangu akasema tumebeba chakula chetu msijali,tukatoa mbuzi tukala nao wanakula mezani,ila nilisikia vibaya,huo ni uchoyo
 
Asante DJ,...mpaka sasa mleta mada katoka nduki sio kwa madongo aliyopewa
 
Duh kwa hii hali ya magufuli naona watu wataanza kulia chumbani teh teh teh
 
You have violated our social norms.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…