Kuhusu kuitisha kura ya maoni

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
1,606
1,956
Wadau tumeshuhudia nchi jirani kama Rwanda wakifanya utaratibu wa kupiga kura ya maoni kwa lengo lakuongeza kipindi cha kukaa madarakani kwa Rais wa Rwanda. Naamini waliofanya hivyo walitumia haki yao ya kidemokrasia na hasa baada ya kuridhishwa na utendaji kazi mzuri wa Kiongozi wao mpendwa Mhesh. Paul Kagame. Kwa kuzingatia sababu hizo kwanini Tanzania tusiige mfano wa jirani zetu ili kumuwezesha Kiongozi wetu mpendwa kupata muda wa kutosha kutuletea maendeleo nchi yetu na kutuondoa kwenye umaskini? Nawasilisha
 
hivi unaelewa wa kutosha kuhusu siasa walau ya nchini kwetu? kwa hiyo rwanda walipiga kura ya maoni???
 
Kwa hiyo akiengezewa muda ndio viwonder vitakuja?hatumtaki aondoke zake
 
Hivi mtaacha lini kuwa walemavu wa akili?hivi waliotangulia wangeamua kufanya hayo unayoyataka huyo Magufuli ungemfahamu? hivi ni kweli baada ya Magufuli hakuna mtanzania mwingine wa kuiongoza Tanzania? Ni mlemavu wa akili pekee anayeweza kuwaza haya. Ni hatari kuishi na kuamini kwamba Magufuli yupo juu ya Tanzania yetu iliyojengwa kwa gharama kubwa na wazee wetu.
 
Ungetoa ushuhuda wa alichofanya cha maana tangu aanze kupanga magogoni kilichoinua kiwango cha maisha ya anaowaita "wanyonge" kwanza ili ipate msingi wa hoja yako.

Sana sana ninachoona ni mipasho,visasi,ukiukwaji wa katiba/sheria na kupandikiza chuki katika jamii ndo naona kajitahidi. Nipe zuri wake japo kiduuchu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii thread ya kichochezi asee . Nashangaa mbona imeachwa ?
 
  • Thanks
Reactions: Ban
Kwahiyo unataka Tujifunze kutoka rwanda???? upumbavu ni mzigo!!!
 
Naamini waliofanya hivyo walitumia haki yao ya kidemokrasia na hasa baada ya kuridhishwa na utendaji kazi mzuri wa Kiongozi wao mpendwa Mhesh. Paul Kagame. Kwa kuzingatia sababu hizo kwanini Tanzania tusiige mfano wa jirani zetu ili kumuwezesha Kiongozi wetu mpendwa kupata muda wa kutosha kutuletea maendeleo nchi yetu na kutuondoa kwenye umaskini? Nawasilisha


Tutumie muda mwingi kuandaa viongozi bora wa baadaye na kuwajengea uwezo kwa kutumia katiba badala ya kutegemea kiongozi mmoja miaka nenda rudi
 
Wadau tumeshuhudia nchi jirani kama Rwanda wakifanya utaratibu wa kupiga kura ya maoni kwa lengo lakuongeza kipindi cha kukaa madarakani kwa Rais wa Rwanda. Naamini waliofanya hivyo walitumia haki yao ya kidemokrasia na hasa baada ya kuridhishwa na utendaji kazi mzuri wa Kiongozi wao mpendwa Mhesh. Paul Kagame. Kwa kuzingatia sababu hizo kwanini Tanzania tusiige mfano wa jirani zetu ili kumuwezesha Kiongozi wetu mpendwa kupata muda wa kutosha kutuletea maendeleo nchi yetu na kutuondoa kwenye umaskini? Nawasilisha
Mmh, mi nafikiri ni mapema mno!
 
Ni mjinga tu anayeweza kufikiri kuwa yeye hajiwezi hadi awezeshwe na wengine. Mleta hoja umeprove failure kabisa kwa kuonyesha kuwa wewe umezaliwa kuongozwa na sio kuongoza.
Hiyo ya kumwongezea fanya hivyo ili awe baba mdogo wako wa maisha but kwa nafasi nyingineyo asimamie na kuitii katiba ya chama chake na nchi at a large!
 
Wadau tumeshuhudia nchi jirani kama Rwanda wakifanya utaratibu wa kupiga kura ya maoni kwa lengo lakuongeza kipindi cha kukaa madarakani kwa Rais wa Rwanda. Naamini waliofanya hivyo walitumia haki yao ya kidemokrasia na hasa baada ya kuridhishwa na utendaji kazi mzuri wa Kiongozi wao mpendwa Mhesh. Paul Kagame. Kwa kuzingatia sababu hizo kwanini Tanzania tusiige mfano wa jirani zetu ili kumuwezesha Kiongozi wetu mpendwa kupata muda wa kutosha kutuletea maendeleo nchi yetu na kutuondoa kwenye umaskini? Nawasilisha

Maana tulitaka tupate katiba mpya ambayo ingemruhusu mgombea binafsi lakini akina Mwakyembe na wenzake wakakomaa kukataa maoni yale. sasa wewe unayetaka leo maoni yapite sijui unataka mchakato mwingine zaidi ya ule wa katiba au unataka upi hasa. Suala mnalolipigia chapuo leo la kutaka Magufuli abaki ni suala lisilowezekana katika mazingira ya sasa kwa sababu mchakato wa Katiba ulishapuuzwa na kutupiliwa mbali tena na akina Magufuli wenyewe. Unataka maoni yapi tena toka kwa wananchi au mnataka kupiga hela tu??? Mnataka CCM ipumzike kufanya kazi kwa kujificha nyuma ya akina Magufuli. Ruanda haina viongozi wengi wanaofaa kama ilivyo kwa Tanzania. Tuna utitiri wa viongozi bora hapa. Shida ni mfumo wa uongozi na utawala wa CCM
 
Back
Top Bottom