Kuhusu hili jukwaa la MMU (Love connect)

Kuhusu hili jukwaa la MMU (Love connect)

Michael Ngusa

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2014
Posts
1,637
Reaction score
463
Nimekuwa nikishuhudia watu wa jinsia ya kiume wakishambuliwa kwa kuitwa majina kama domo zege, huko mtaani hujaona n.k. kwenye jukwaa la MMU (Love connect). Baada ya kupost kuwa anatafatufa mke, mchumba nk. Kwani lengo la hili jukwa ni nini? Kwanini mtu umrudishe na madongo.

Mwanamke akipost anatafuta wala hawamshushui, atazongwa na PM huyo mpaka basi na pengine wanao PM ndo hao hao wa kwanza kuwashushua wenzao wa kiume wanaopost kutafuta. Kama huwezi msaidia mtu si upite kulia jamani?

Ni kweli mtaani wapo lakini nini maana ya teknolojia kwanini niache kitanda na TV nikazunguke mtaani kutafuta mwanamke wakati simu yangu yenye Jamii Forums app inaweza niletea mapenzi hadi kwangu.
 
Hakuna madomo zege wanawake ndiyo maana hawasumbuliwi
 
Hili ni Jukwaa la Love Connect nadhani wengine hudhani wameingia Jukwaa la Siasa. Kwa wanaoingia humu basi kama hawana nia ya kuwa connected wasiwaseme 'TARGET' ya Jukwaa hili kwani wanahitaji huduma hii ya kuwa connected!
 
pole bwana lazima upewe moyo na urushiwe madongo pokea yote
 
Wanatumia "defensive mechanism" ili waendelee kubaki na kuwa wao tu katika game. They just play their cards well
 
kama madongo yatakuwepo kwani hata huko mtaani nanko kuna madongo sembuse kwenye mitandao

wacha wapewe madongo na makavu live watapewa ila cha kuafanya wao wawe wavumilivu na wastahimilivu tu
 
Back
Top Bottom