Kuhusu Escrow, Kanisa Katoliki limejifedhehesha

Kuhusu Escrow, Kanisa Katoliki limejifedhehesha

Mantombazane

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
579
Reaction score
367
Sakata la Escro limeitikisa serikali pamoja na kujidai pesa husika hazikuwa za serikali. Mawaziri na mwanasheria mkuu wamepoteza nyadhifa zao kutokana na kashfa hiyo. Baadhi ya watendaji nao wamechukuliwa hatua.

Kashfa hii ilihusisha hata maaskofu wa kanisa letu tena ni wale tuliowaheshimu sana kutokana na kauli zao za kujidai wanakemea ufisadi. Na mbaya kuliko zote uchafu huu umefanyika kupitia benki yetu ya kanisa.

La ajabu hatujaona kanisa likichukua hatua za kujisafisha badala yake tunaona watuhumiwa wakiendelea kutoa huduma ya kanisa.

Hii imetufanya baadhi yetu tudhani zile pesa kuna zingine walimpa mkuu wao kama wale wa magogoni ambao nao hawajachukuliwa hatua yoyote kwani wengi tunaona ni kama walitumwa tu kuchukua mzigo wa mwenye nyumba.

Vyovyote iwavyo hawa maaskofu wamelichafua kanisa kwani hata utetezi wao haujai hata kwenye kiganja cha mkono. Lakini kwakuwa kanisa limenyamaza kimya na kuwaacha waendelee na huduma ya kanisa, ni wazi kuwa kanisa nalo linajihusisha kutakatisha fedha kupitia kwa watendaji wake kama maaskofu husika na vyombo vyake kama benki ya mkombozi.

Kwakuwa kanisa limeamua kuwa sehemu ya uchafu ulifanyika Escrow, ni vizuri sasa likafunga mdomo kuikemea serikali inapotokea kuna ufisadi ambao kimsingi kanisa ndio wajibu wake kukemea.

Kesho hatutashangaa kuona hata pesa za madawa ya kulevya zinatakatishwa kupita vyombo vya kanisa na kubarikiwa na maaskofu. Tukifika hapo umuhimu wa kanisa unakuwa haupo tena!
 
Kwa nini watu wanashindwa kutulia kidogo na kufikiri kiukweli kuhusu kashfa ya escrow na jinsi ambavyo maaskofu walivyojikuta wakichanganywa ndani bila kujua?

Inawezekana hata wewe ungeweza kupewa mgao wa fedha na Ruge kama ungekuwa na taasisi na kufahamiana na Ruge.

Sasa kwanini mnalipuka tu hovyo na kusema Kanisa limeshiriki escrow. Mnafikiri kwa undani au mnaongea kishabiki tu ilimradi kwasababu ni rahisi kuwaaminisha watu wasiofikiri vizuri
 
Mbona mnatumia Lawama kanisa ?kanisa Halifanyi kazi zake kwa kukurupuka linafanya kwa Ustadi wa hali ya Juu kabisa na kwa Ufanisi ,weka pembeni hawa Maskofu wetu kwa muda,sasa tuangalie upande wa shina nini kilifanyika baada ya miaka mingi ya Uharibifu wa watoto wa kiume ndani ya majumba ya kuabudia na ilichuwa miaka mingi zaidi kabla ya hayo mambo kutafutiwa suluhisho na kupigiwa vita rasmi ,sasa ukija kuhusu hapa Tz makanisa mengi bado yanhitaji fedha au tuseme wachungaji bado wanahitaji fedha kwa shuhuli zao binafisi na zile za kuendeleza makanisa na kama tunavyo ijuwa hali ya maisha Tz ni kama vile mbuga ya wanya mwenye Uwezo wa kumuangusha mwenziwe hula nyama kwa hali hiyo ndio imelikumba kanisa na kufumbia macho hayo madai ya Escrow (mchungaji nae pesa anaiona Tamu kama mie na wewe )
 
Mtoa mada anatakiwa atambue kanisa lina maaskofu wangapi na sio kukurupuka kisa anataarifa za askofu mmoja tena msaidizi.pumba za kupindukia unapost
 
Mtoa mada anatakiwa atambue kanisa lina maaskofu wangapi na sio kukurupuka kisa anataarifa za askofu mmoja tena msaidizi.pumba za kupindukia unapost
Kujua idadi ya maaskofu ili iweje? Wewe unajua idadi yao? Hata angekuwa mmoja au msaidizi la msingi ni kuwa matendo yake yanaliabisha kanisa. Sasa jiulize kina Ngeleja, Chenge, Tibaijuka, na wengineo wameachishwa uongozi kwa kupokea mgao ambao maaskofu wetu Nzigilwa na Kilaini nao waliupata. Sasa kwanini serikali imeona sio maadili lakini kanisa linauchuna? Hao maaskofu hawana udhu!
 
Mtoa mada anatakiwa atambue kanisa lina maaskofu wangapi na sio kukurupuka kisa anataarifa za askofu mmoja tena msaidizi.pumba za kupindukia unapost

kanisa kama taasisi linapaswa kujitenga na uovu.
Kama mtumishi wa kanisa anafanya uovu wazi kabisa na kanisa linakaa kimya inamaanisha kuwa kanisa zima limefanya uovo na linaunga mkono uovu huo.
Njia pekee ya kulisafisha kanisa ni kuwatenga na kuwachukulia hatua za kikanisa wale watumishi wote waliofanya uovu husika.
Mpaka sasa Pengo alivyokaa kimya mie naamini kanisa linafanya uovu wa kutakasa pesa haramu.
 
Kujua idadi ya maaskofu ili iweje? Wewe unajua idadi yao? Hata angekuwa mmoja au msaidizi la msingi ni kuwa matendo yake yanaliabisha kanisa. Sasa jiulize kina Ngeleja, Chenge, Tibaijuka, na wengineo wameachishwa uongozi kwa kupokea mgao ambao maaskofu wetu Nzigilwa na Kilaini nao waliupata. Sasa kwanini serikali imeona sio maadili lakini kanisa linauchuna? Hao maaskofu hawana udhu!

Kanisa haliwezi kuaibika anaeaibika ni yule mtenda maovu kwa unafiki wake.
 
Ninavyolijua kanisa katolliki kukurupuka ni mwiko kwa hawa jamaa. Jipe muda ndugu. Nilitegemea serikali iwachukulie hatua hao maaskofu huku tukisubiri hatua za kanisa katoliki. Hawa jamaa hawakurupuki ndugu.
 
Sio kweli,kanisa katoliki hatujafedheheshwa na escrow,tumeshindwa kufedheheshwa na ulawiti wa watoto dunia nzima tuje kufedheheshwa na escrow ya tanzania.
 
Sakata la Escro limeitikisa serikali pamoja na kujidai pesa husika hazikuwa za serikali. Mawaziri na mwanasheria mkuu wamepoteza nyadhifa zao kutokana na kashfa hiyo. Baadhi ya watendaji nao wamechukuliwa hatua.

Kashfa hii ilihusisha hata maaskofu wa kanisa letu tena ni wale tuliowaheshimu sana kutokana na kauli zao za kujidai wanakemea ufisadi. Na mbaya kuliko zote uchafu huu umefanyika kupitia benki yetu ya kanisa.

La ajabu hatujaona kanisa likichukua hatua za kujisafisha badala yake tunaona watuhumiwa wakiendelea kutoa huduma ya kanisa.

Hii imetufanya baadhi yetu tudhani zile pesa kuna zingine walimpa mkuu wao kama wale wa magogoni ambao nao hawajachukuliwa hatua yoyote kwani wengi tunaona ni kama walitumwa tu kuchukua mzigo wa mwenye nyumba.

Vyovyote iwavyo hawa maaskofu wamelichafua kanisa kwani hata utetezi wao haujai hata kwenye kiganja cha mkono. Lakini kwakuwa kanisa limenyamaza kimya na kuwaacha waendelee na huduma ya kanisa, ni wazi kuwa kanisa nalo linajihusisha kutakatisha fedha kupitia kwa watendaji wake kama maaskofu husika na vyombo vyake kama benki ya mkombozi.

Kwakuwa kanisa limeamua kuwa sehemu ya uchafu ulifanyika Escrow, ni vizuri sasa likafunga mdomo kuikemea serikali inapotokea kuna ufisadi ambao kimsingi kanisa ndio wajibu wake kukemea.

Kesho hatutashangaa kuona hata pesa za madawa ya kulevya zinatakatishwa kupita vyombo vya kanisa na kubarikiwa na maaskofu. Tukifika hapo umuhimu wa kanisa unakuwa haupo tena!
Jamani unabii unasema kanisa la Roman Catholic ni kanisa la freemason ukweli ni huo,hosea anasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maandiko.
 
Back
Top Bottom