Kuhusu bodaboda, Waziri wa Mambo ya Ndani sema neno

maiyanga1

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
1,317
1,790
Kama ilivyokuwa kwa wapiga debe kwenye stand mbalimbali nchini walivyoanza taratibu kujiingiza kwenye udalali wa kugombea abiria kiasi cha abiria kupelekwa gari nyingine na mizigo yake gari nyingine na sasa hawadhibitiki tena, ikaja kwa machinga ambao nao sasa haiwezekani tena kuwadhibiti kwa jinsi walivyojimilikisha maeneo mbalimbali ya kufanyia biashara.

Na sasa kuna tatizo kubwa la boda boda kutozingatia sheria za barabarani kiasi kwamba wanasabisha ajali. Mifano ipo mingi watu wanavyogongwa kwenye taa za barabarani au kwenye vivuko vya wenda kwa miguu. Pia sasa hata watoto wanaendesha bodaboda, lakini mbaya zaidi bodaboda wamekuwa waporaji. Kipindi cha Lugola ndio alitoa maelekezo kwamba bodaboda wasikamatwe na ni marufuku polisi kushikilia pikipiki vituoni.

Kwako Simbachawene bodaboda ni bomu jingine ambalo halitaweza kudhibitika.

Kauli ya "Tii sheria bila shuruti" iwahusu pia bodaboda.
 
... wamefikia kiwango cha kero kiasi kwamba barabarani ikitokea ajali ya bodaboda anayeonewa huruma ni abiria tu kama hakuwa na abiria wala hakuna anayejali kwamba ni binadamu kafa au kajeruhiwa amelala chini! Ile roho ya ubinadamu kwa bodaboda haipo tena kutokana na tabia zao za kishenzishenzi.
 
Nyie mnataka vijana wetu wafanye shughuli gani hapa mjini? Machinga hamtaki boda pia hamtaki
 
Viongozi huwa hawanaga akili ya kufikiria impact ya kitu in a long run wao wanafikiria kwa miaka mitano mitano tu ya uchaguzi. Ulikua ni uzwazwa wa hali ya juu kupunguza faini ya boda boda kutoka 30 hadi 10 alfu.

Hiyo deficit wangefund katika elimu ya usalama barabarani kwa bodaboda ama kuunda task force ya kupunguza ajali na majanga ya boda kwa kaw enforcement.

Rais aliingizwa chaka bajeti iliyopita kwa kuambiwa kwamba hiyo ni kuwanyanyua wanyonge na wapiga kura wa 2025.
Unaminya kule unalegeza huku. Bodaboda versus Machinga bila kujua kuwa ni disaster on creation.

Bodaboda now hatuaogopi fine, polis akikataa buku yangu namwongezea jero Kibati akizengua mwisho buku 2 nachapa rapa aandike fine buku 10 kichwa kimoja tu natanua ndani ya siku 7.

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Kama mtoa mada alivyoainisha, bodaboda na bajaji Ni kana kwamba sheria za barabarani haziwahusu.

Wao ku overtake gari ni mahali popote; iwe kushoto, kwenye Kona, kwenye kivuko cha zebra n.k.

Boda boda wanapakia mizigo ya hatari sana kwa watumiaji wengine wa barabara. Mfano, milango, bati, nondo, n.k.

Yote haya yanafanyika polisi wa usalama barabarani wakiangalia lakini hakuna hatua wanazochukua dhidi yao!
 
Bodaboda,hawafuati sheria za barabarani,hawasimami kwenye taa za kuongoza magari,wanapakia abiria wanne,watoto wadogo wanaendesha pikipiki.
 
Labda nikuulize Waziri!

Mmejipangaje kudhibiti uhalifu;
1. Wizi ambao unaotekelezwa Kwa njia za bodaboda.

2. Kugonga magari ya watu kwenye Trafic jam na kukimbia wakijua huwezi kuwakimbiza?
Mna mfumo gani wa kutafuta pikipiki ikiwa inahitajika kama imetenda uhalifu? Kama kumsimamisha tu Kwa ajili ya ukaguzi wa kawaida Polisi wamekwama kwenye hilo

Huoni Kuna balaa kubwa siku za mbeleni?

3. CCM mnaposema mmetengeneza ajira Kwa vijana kujiajiri kwenye bodaboda hivi mnafikiri Kwa kutumia akili kweli au Kuna mifumo mipya ya kufikiri imeingia?
 
Kumbe mnatuonea wivu tunavyoendesha spidi mwendo wa mbwa, mtuache maisha yenyewe magumu
st,small,507x507-pad,600x600,f8f8f8.png
 
Duh! Nikiiona kasi yake ya kuongezeka mtaani naishiwa pozi kabisa....maana ndio ajira nafuu inayochangamkiwa na ya haraka zaidi iliyobaki kwa vijana kwa Sasa .Hasa wanaotoka kuhitimu vyuo.😥😥😥😥
 
Duh! Nikiiona kasi yake ya kuongezeka mtaani naishiwa pozi kabisa....maana ndio ajira nafuu inayochangamkiwa na ya haraka zaidi iliyobaki kwa vijana kwa Sasa .Hasa wanaotoka kuhitimu vyuo.😥😥😥😥
Sidhani kama ni kuchangamkia ajiria bali hakuna namna.
Kuongezeka kwake mtaani kunamaanisha kuwa umaskini unaongezeka.
 
Viongozi huwa hawanaga akili ya kufikiria impact ya kitu in a long run wao wanafikiria kwa miaka mitano mitano tu ya uchaguzi. Ulikua ni uzwazwa wa hali ya juu kupunguza faini ya boda boda kutoka 30 hadi 10 alfu.
Ilitakiwa serikali ipandishe maradufu kodi ya kuingiza pikipiki nchini ili ziwe chache and bei ghali.
Nadharia ya bodaboda kuwa ni mtaji wa maskini ni mbaya sana na inadumaza ubongo wa vijana.
 
Back
Top Bottom