Kuhusu asilimia 60 mimi nimeelewa hivi

Kuhusu asilimia 60 mimi nimeelewa hivi

EllySkyWilly

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2020
Posts
2,204
Reaction score
2,086
Habari za wakati na wasaa huu ndugu zangu.

Wakuu gharama ya usafiri ya kupitisha pipa moja la mafuta kwenye bomba kutoka Uganda mpaka Tanga ni dola 12.25 Yaani hiyo ndio nauli yake.

Katika hiyo nauli sasa ambayo ni dola 12.25 Tanzania atapata asilimia 60 alafu uganda atapata asilimia 40 ya nauli.

Kwanini sisi tutapata gawio kubwa la nauli.

kwasababu kilometa nyingi za bomba zipo upande wa Tanzania hivyo gharama za uendeshaji zitakua nyingi zaidi upande wa Tanzania.

Lakini pia bomba linapita katika mikoa mingi na wilaya nyingi zaidi katika ardhi ya Tanzania hivyo risk nyingi zitakuwa upande wa Tanzania. Mfano wa risk zinaweza kuwa kupasuka kwa bomba au risk nyingine yoyote inayoweza kuathiri afya au maisha ya Watanzania na hata viumbe vyovyote vilivyopo kwenye ardhi yet.

Hivyo lazima Uganda wapate asilimia chache.

Gharama za kuuziana mafuta sisi hazituhusu ni za wao wenyewe wenye mali na wawawekazaji wao.

Uganda watauza pipa zao za mafuta sisi tunawasafirishia kwa bomba hivyo sisi wanatupa pesa ya usafiri.

Ndugu zangu nawaombeni sana tusiwe tunapinga kila linalo fanywa na serikali. Huu mradi unafaida kubwa sana kwa watanzania na vizazi vyetu vijavyo. Hiyo asilimia 60 tutakayo ipata ni pesa nyingi sana. Na bado kuna ajira hapo zitakazo patikana ni nyingi mnoo.

Bado pia huko mradi unakopita pia wafanyabiashara mbalimbali mfano wa vyakula, vinywaji, nyumba za kulala wageni wote watafaidika na huo mradi.

Hivyo ndivyo maisha yanavyokwenda duniani tuache Jamani kuwa wapinzani wa mambo muhimu na ya maendeleo. Tuache kukosoa kosoa mambo muhimu na ya maendeleo.

Bali tujikite kuingalia Tanzania ya kesho itakuwaje kwaajili ya vizazi vyetu vijavyo na tuache kupoteza muda wa kukosoa Rais wetu bali tujikite kwenye kuungana naye ili maono aliyo nayo yaweze kutimia. Mambo anayofanya Mh. Rais ni makubwa mno na anastahili pongezi kwakweli.

Mambo ya kujenga na kuimarisha miundo mbinu ndio mambo muhimu duniani hilo ndilo walilo lifanya China miaka ya nyuma ndio sababu uchumi wao unakimbia kwa kasi sana.

Miundombinu ya uhakika na imara inaharakisha maendeleo ya nchi. Naomba tumwaachie Rais wetu Magufuli hii nchi hakika nawambia tutafika mbali sana. Huyu Rais ana akili nyingi mnoo.

Kama kuna mtu anaweza kufanya rushwa na asikamatwe Tanzania ya leo naomba ajitokeze na ajaribu kufanya.

Kama kuna mtu yeyote anaweza kufanya ufisadi kwenye taasisi yeyote ya serikali katika Tanzania ya leo naomba ajitokeze na ajaribu tuone kama hata julikana.

Ametumia akili nyingi mno Mhe. Rais , anastahili pongezi nyingi mno.

Basi nichukue fursa hii ndugu zangu na watanzania wenzangu kumwombea kura Rais Magufuli. Mitano tena kwa Magufuli.
 
Ni ufafanuzi mzuri, ila tunataka kujua kwa uhakika 60 v/s 40% ni kwanini iwe hivyo, haya maelezo yako ni mazuri ila ni hisia zako zaidi.
 
Kwahiyo basi sio faida bali ni mgawanyo wa nauli kulingana na umbali huku risk nyingi zikibaki Tanzania...in fact kwenye hili mganda anaweza kufaidika zaidi

Jr[emoji769]
 
Kwahiyo basi sio faida bali ni mgawanyo wa nauli kulingana na umbali huku risk nyingi zikibaki Tanzania...in fact kwenye hili mganda anaweza kufaidika zaidi

Jr[emoji769]
Siyo anaweza, ni amefaidika maana hatatumia gharama kubwa za maintenance umeme na ulinzi. Sisi tumekurupuka ili tupate kitu kidogo!
 
Kwanini tudijenge

Kwanini tusijenge oil refinery yetu mji wa kahama bomba linakopita Ili uganda watuuzie mafuta Ili yatumike Mara, mwanza, shinyanga,geita,katavi,simiyu ,tabora na singida Ili tupate upungufu wa Bei badala ya kuchukua mafuta dar na kuyarudisha tena kwenye hiyo mikoa?
 
Ni ufafanuzi mzuri, ila tunataka kujua kwa uhakika 60 v/s 40% ni kwanini iwe hivyo, haya maelezo yako ni mazuri ila ni hisia zako zaidi.
Hivi ninyi wafuasi wa Chadema huwa mnatumia akili kupambanua mambo? Uganda lazima wapate faida zaidi sababu wao ndio wanauza hayo mafuta ghafi,sisi tumechangamkia dili bomba lipite ili tupate mapato kwa bomba kupita nchini kwetu tu,bado mnaona kama tunanyonywa na sio mradi mzuri. Mnakera sana.
 
Siyo anaweza, ni amefaidika maana hatatumia gharama kubwa za maintenance umeme na ulinzi. Sisi tumekurupuka ili tupate kitu kidogo!
Wewe unafikiri kwa kutumia makamasi na kinyesi kwani gharama za maintainance na ulinzi ni za nchi moja? Huu mradi unagharamiwa na Uganda na Total,sisi hapa tunapata pesa kwa bomba kupita nchini tu.
 
Hivi ninyi wafuasi wa Chadema huwa mnatumia akili kupambanua mambo? Uganda lazima wapate faida zaidi sababu wao ndio wanauza hayo mafuta ghafi,sisi tumechangamkia dili bomba lipite ili tupate mapato kwa bomba kupita nchini kwetu tu,bado mnaona kama tunanyonywa na sio mradi mzuri. Mnakera sana.
Hahahaaaa....... Wanakera kwa kweli!
 
Kwanini tudijenge o
Kwanini tusijenge oil refinery yetu mji wa kahama bomba linakopita Ili uganda watuuzie mafuta Ili yatumike Mara, mwanza, shinyanga,geita,katavi,simiyu ,tabora na singida Ili tupate upungufu wa Bei badala ya kuchukua mafuta dar na kuyarudisha tena kwenye hiyo mikoa?

Ujenge refinery kwa mafuta yapi? Hayo mafuta ni ya Total. Sio ya UG wala TZ. Total kashayanunua.. kwa bongo hapa yanapita tu.
 
Kwahiyo basi sio faida bali ni mgawanyo wa nauli kulingana na umbali huku risk nyingi zikibaki Tanzania...in fact kwenye hili mganda anaweza kufaidika zaidi

Jr[emoji769]
Hiyo ni faida kubwa sana. Kumbuka kuwa mafuta wala bomba sio mali yetu, sisi tunanufaika kwa sababu linapita kwetu ; ni kama vile ndege inapotumia anga ya Tanzania wakati inaenda nchi nyingine au magari ya transit yanayobeba mizigo au mafuta kwenda nchi jirani.
Pia matengenezo ya bomba sio kazi yetu ni kazi ya mmiliki na akitumia umeme wetu au maji atalipia nje ya hizo 60% kama gharama za uendeshaji.

Kwa ufupi hiyo ni faida ya moja kwa mija lakini kuns indirect profits nyingi sana.
 
Umefafanua vizuri ila museven kaja kupiga kampeni chato.yeye na mwenyeji wake hawakulifafanua vizuri kwa makusudi hii ni hatari wakitoka madarakani Marais wanaokuja wataona ni utapeli mkataba utaleta shida
 
Hivi ninyi wafuasi wa Chadema huwa mnatumia akili kupambanua mambo? Uganda lazima wapate faida zaidi sababu wao ndio wanauza hayo mafuta ghafi,sisi tumechangamkia dili bomba lipite ili tupate mapato kwa bomba kupita nchini kwetu tu,bado mnaona kama tunanyonywa na sio mradi mzuri. Mnakera sana.
Qq

Mkuu umepamia maelezo, mimi nimetaka kujua hiyo 60% ya kwetu ni kutokana na maelezo ya mleta mada, au ndio haswa kilicho ndani ya huo mkataba. Rejea kichwa cha habari cha mleta mada.
 
Kwanini tudijenge o
Kwanini tusijenge oil refinery yetu mji wa kahama bomba linakopita Ili uganda watuuzie mafuta Ili yatumike Mara, mwanza, shinyanga,geita,katavi,simiyu ,tabora na singida Ili tupate upungufu wa Bei badala ya kuchukua mafuta dar na kuyarudisha tena kwenye hiyo mikoa?
Mafuta bado ni ya Uganda na Kampuni la Total la Ufaransa hayatuhusu kabisa wao wamefanya kuyapitishia Tanzania
mfano Basi la abiria likitokea Uganda na kwenda Tanga Tanzania kuwapitisha abiria au watalii katika nauli wamekupa 60% huwezi kudai Basi ni lako, sisi Tanzani tukubali hiyo % inatosha
 
Usisahau kutoa gharama ya ujenzi! $3.4 billions, zikilipwa hizo ndo uje huku Sasa unakosema faida ya 60%
 
Mkuu umepamia maelezo, mimi nimetaka kujua hiyo 60% ya kwetu ni kutokana na maelezo ya mleta mada, au ndio haswa kilicho ndani ya huo mkataba. Rejea kichwa cha habari cha mleta mada.
Mkataba wa nini? Kama sio kupitisha mafuta ghafi mpaka Chongoleani.
 
Mafuta bado ni ya Uganda na Kampuni la Total la Ufaransa hayatuhusu kabisa wao wamefanya kuyapitishia Tanzania
mfano Basi la abiria likitokea Uganda na kwenda Tanga Tanzania kuwapitisha abiria au watalii katika nauli wamekupa 60% huwezi kudai Basi ni lako, sisi Tanzani tukubali hiyo % inatosha
Kwa mantiki hiyo cruide oil inapita na mabomba zaidi ya kms 1100 kwani Nadi tusiyanunue then tufanye refinery Ili mafutayashuke Bei ? Kwa usemi wako tutaendelea kuagiza mafuta nje ya nchi kwa muda mrefu na gharama kubwa wakati chini ya ardhi ya tanzania mafuta yanapita kwenye mabomba kuelekea tanga tukisubiri kulipwa 60%? Kitakuwa kituko Cha mwaka. Ushauri wangu tupokee chetu 60% then tununue cruise oil yao tuifainye refinery Ili kupata faida Mara mbili . Tanzania tuamke
 
Back
Top Bottom