Mwafrika Halisia
Member
- Feb 14, 2022
- 68
- 105
Habari wakuu, naomba msaada
Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika kozi ya diploma in Clinical Dentistry nikiendelea na masomo yangu katika Kigamboni City College of Health and Allied Sciences. Ni mnufaika wa mkopo kutoka HESLB.
Kutokana na gharama kuwa nyingi chuo hiki Cha private Nina nia ya kuhamia katika chuo cha serikali mwaka wa pili, haswa chuo cha Lugalo Military Medical School kwa ajili ya kuendelea na kozi hiyo hiyo.
Naomba kufahamu yafuatayo:
1. Mchakato wa kuhama kutoka chuo binafsi kwenda chuo cha serikali ukoje? Kuna taratibu gani rasmi zinazopaswa kufuatwa?
2. Kwa upande wa mkopo wa HESLB, nikiendelea na kozi hiyo hiyo katika chuo cha serikali, nitakuwa na nafasi ya kuendelea kupokea mkopo kama kawaida au kuna hatua maalum zinazopaswa kuchukuliwa?
Naomba msaada kwa yeyote mwenye uzoefu au taarifa sahihi kuhusu hili. Nawashukuru sana wakuu kwa msaada wenu na ushauri wenu wa kitaalamu.
Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika kozi ya diploma in Clinical Dentistry nikiendelea na masomo yangu katika Kigamboni City College of Health and Allied Sciences. Ni mnufaika wa mkopo kutoka HESLB.
Kutokana na gharama kuwa nyingi chuo hiki Cha private Nina nia ya kuhamia katika chuo cha serikali mwaka wa pili, haswa chuo cha Lugalo Military Medical School kwa ajili ya kuendelea na kozi hiyo hiyo.
Naomba kufahamu yafuatayo:
1. Mchakato wa kuhama kutoka chuo binafsi kwenda chuo cha serikali ukoje? Kuna taratibu gani rasmi zinazopaswa kufuatwa?
2. Kwa upande wa mkopo wa HESLB, nikiendelea na kozi hiyo hiyo katika chuo cha serikali, nitakuwa na nafasi ya kuendelea kupokea mkopo kama kawaida au kuna hatua maalum zinazopaswa kuchukuliwa?
Naomba msaada kwa yeyote mwenye uzoefu au taarifa sahihi kuhusu hili. Nawashukuru sana wakuu kwa msaada wenu na ushauri wenu wa kitaalamu.