Kugombania maiti

Kugombania maiti

Mkuu, "ndoa ya kisasa" ndio ipi hiyo?
Ndoa ya kisasa, ndoa ambazo zinaambatana na sherehr kubwa. Bibi harusi na bwana harusi wanatembezwa mji mzima wakiwa wanapungia watu mikono.
Ndoa zenye gharama zake.
 
mtihani mkubwa ni pale wanandoa ni dini tofauti na kila upande wamekolea kwenye dini husika
 
Kumbe walishaachana nasema hiviii huyo mwanaume ana kiherehere
Habari zenu wakuu...

Huku kwetu kuna mgogoro wa kidini na issue yenyewe iko hivi...

Huyu dada alikubali kubadili dini ili apate cheo cha "mrs" . Alikubali kujifunika kichwa. Ndoa yao ilikuwa ya kisasa na watu tulikula na kunywa na kusaza siku hiyo.

Kama mjuavyo ndoa sio harusi, hawa wapendanao walichokana. Sijui sababu iliyowafanya wachokane ila nahisi ni ugumba wa huyu mgalatia. Hivyo walitengana kila mmoja akashika hamsini zake.

Dada wa watu amepumua pumzi yake ya mwisho ghafla hivi karibuni. Na hapo ndo mgogoro umeanza. Mmewe anataka azike kwao kwa taratibu za dini yake. Nduguze na mwanamke hawataki mtoto wao awekwe alazwe mwandani.

Unaambiwa pande zote zimechachamaa....wagalatia na wasaudia wanataka kupigana kisa maiti. Serikali imeingilia kati, tunasubiri uamuzi wa serikali.

Hivi kuna faida gani kugombania mtu mfu?

NB. Usioe wala kuolewa na mtu asie wa dini yako!

ASANTENI

Feedback: Mwanamke atazikwa kwao.
 
nakazia hapa USIOLEWE NA USIOE MTU ASIYE WA DINI YAKO KWANI UNABANA RIZIKI KWA WENGINE WANAOLANDANA DINI NA HUYO UNAYEENDA OLEWA AU KUMUOA
Nakazia ukimwomba Mungu lazima atakupa wa kufanana nawe hawezi kukupa wa tofauti hakuna kitu kigumu kama kubadili dini wallah
 
Nakazia ukimwomba Mungu lazima atakupa wa kufanana nawe hawezi kukupa wa tofauti hakuna kitu kigumu kama kubadili dini wallah
nakazia hakuna kitu kibaya ukitengwa na waamini wako wa zamani katika mambo mengine ya kijamii baada ya kuhama dini
 
Back
Top Bottom