Nebuchadinezzer
JF-Expert Member
- Oct 1, 2018
- 1,403
- 2,549
Habari zenu wakuu...
Huku kwetu kuna mgogoro wa kidini na issue yenyewe iko hivi...
Huyu dada alikubali kubadili dini ili apate cheo cha "mrs" . Alikubali kujifunika kichwa. Ndoa yao ilikuwa ya kisasa na watu tulikula na kunywa na kusaza siku hiyo.
Kama mjuavyo ndoa sio harusi, hawa wapendanao walichokana. Sijui sababu iliyowafanya wachokane ila nahisi ni ugumba wa huyu mgalatia. Hivyo walitengana kila mmoja akashika hamsini zake.
Dada wa watu amepumua pumzi yake ya mwisho ghafla hivi karibuni. Na hapo ndo mgogoro umeanza. Mmewe anataka azike kwao kwa taratibu za dini yake. Nduguze na mwanamke hawataki mtoto wao awekwe alazwe mwandani.
Unaambiwa pande zote zimechachamaa....wagalatia na wasaudia wanataka kupigana kisa maiti. Serikali imeingilia kati, tunasubiri uamuzi wa serikali.
Hivi kuna faida gani kugombania mtu mfu?
NB. Usioe wala kuolewa na mtu asie wa dini yako!
ASANTENI
Feedback: Mwanamke atazikwa kwao.
Huku kwetu kuna mgogoro wa kidini na issue yenyewe iko hivi...
Huyu dada alikubali kubadili dini ili apate cheo cha "mrs" . Alikubali kujifunika kichwa. Ndoa yao ilikuwa ya kisasa na watu tulikula na kunywa na kusaza siku hiyo.
Kama mjuavyo ndoa sio harusi, hawa wapendanao walichokana. Sijui sababu iliyowafanya wachokane ila nahisi ni ugumba wa huyu mgalatia. Hivyo walitengana kila mmoja akashika hamsini zake.
Dada wa watu amepumua pumzi yake ya mwisho ghafla hivi karibuni. Na hapo ndo mgogoro umeanza. Mmewe anataka azike kwao kwa taratibu za dini yake. Nduguze na mwanamke hawataki mtoto wao awekwe alazwe mwandani.
Unaambiwa pande zote zimechachamaa....wagalatia na wasaudia wanataka kupigana kisa maiti. Serikali imeingilia kati, tunasubiri uamuzi wa serikali.
Hivi kuna faida gani kugombania mtu mfu?
NB. Usioe wala kuolewa na mtu asie wa dini yako!
ASANTENI
Feedback: Mwanamke atazikwa kwao.