"Kufulia" kwa CUF Bara!

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
Hivi kwa nini Chama cha Wananchi (CUF) kimekosa umaarufu kiasi kwamba kilikosa kiti hata kimoja bara 2005? Wabara wengi hawakioni kama Chama mbadala bali Chama Cha Waislamu kutokana na viongozi wake almost wote kuwa Waislamu! Je, ipi hasj ni sababu? 1. Kwa sababu ya Udini? 2. Hujuma za CCM? 3. Sera mbovu? 4. Lugha ya vitisho, eg tusipoingia Ikulu damu itamwagika? 5. Viongozi wake hawauziki? 6...?
 
Hivi kwa nini Chama cha Wananchi (CUF) kimekosa umaarufu kiasi kwamba kilikosa kiti hata kimoja bara 2005? Wabara wengi hawakioni kama Chama mbadala bali Chama Cha Waislamu kutokana na viongozi wake almost wote kuwa Waislamu! Je, ipi hasj ni sababu? 1. Kwa sababu ya Udini? 2. Hujuma za CCM? 3. Sera mbovu? 4. Lugha ya vitisho, eg tusipoingia Ikulu damu itamwagika? 5. Viongozi wake hawauziki? 6...?
mi nadhani ni kutokana na hapo kwenye nyekundu, kutumia sana kanzu yaani lile vazi la maandano kama vazi la chama kitaifa
 
CUF ni chama cha kipemba ndugu, huku bara wapo tu kama signposts. Ni watu wa kujitoa mhanga, wenye imani kali ya mrengo wa kushoto.
 
bahati mbaya siyo swala lililopo hapa, zaidi ya kufulia kwa cuf
Hili ndiyo umelinote. Waliyeanza hukutaka kusema. Ukweli, wengi wamechoshwa na siasa za ubabaishaji. Lakini kinachoonekana sasa hivi ni kwamba vyama vya upinzania vinapigana vijembe saana na kudhaurauliana. Kwahakika ni kazi saana kwa upinzani kuchukua nchi maana strategy zao ni poor. Hebu angalia Ubungo, anakwenda Mtatiro na Mnyika wanapambana na yule mama Hawa. Hapo inamaana upinzani watagawana kura vilivyo jimbo hilo na CCM itashinda kiurahisi. Kwahiyi propaganda kati ya upinzani kwa upinzani ni kama vita vya Panzi.
 
Kama muna dai CUF ni chama cha Kiislamu sababu viongozi wake wengi ni waislamu basi tukubali kuwa chadema ni cha wakiristo sababu viongozi wake wengi ni wakiristo na bila shaka CCM itakuwa ni chama kisicho na dini kwani kina mchanganyiko wa dini zote hivyo kinatufaa watanzania ili tuepuke machafuko ya kidini.

Ama wanaodai kuwa CUF wamefulia bara basi waseme pia Chadema hawana mvuto visiwani.
 
Kama muna dai CUF ni chama cha Kiislamu sababu viongozi wake wengi ni waislamu basi tukubali kuwa chadema ni cha wakiristo sababu viongozi wake wengi ni wakiristo na bila shaka CCM itakuwa ni chama kisicho na dini kwani kina mchanganyiko wa dini zote hivyo kinatufaa watanzania ili tuepuke machafuko ya kidini.

Ama wanaodai kuwa CUF wamefulia bara basi waseme pia Chadema hawana mvuto visiwani.

Mh Zito Kabwe na Mh Said AMour Arfi wanasali Makanisa yepi?

Mwenyekiti wa CCM, Makamu wake wa Visiwani na Katibu Mkuu hawa ni dini gani?
 
Siasa in mchezo wa public relations. It is all about perception and how people perceive you. Kinacho iponza CUF labda (I can only theorize) ni kwamba kinaonekana ni a marginal party. Kwa bahati mbaya au nzuri CUF kina onekana kama ni chama cha Waislamu au Pemba. I don't think it is the case bali nadhani ni swala lililo jitokeza ambalo wao wenyewe wameshindwa kuli address.

The best thing for CUF kwa sasa ni kudervisify. Lazima ijionyeshe kuwakilisha Watanzania wote na si sehemu fulani tu ya jamii au eneo fulani tu la kigeografia. Hili ni swala ambalo nadhani nalo linge kiathiri chama cha Chadema lakini kwa jitihada zao wenyewe au kwa bahati inaelekea wameondoa hiyo perception kwa kiasi kikubwa. Ukichukulia mfano wa CCM. Kwa kuangalia CCM hauwezi kusema ni chama cha dini fulani au eneo fulani kutokana na proportionality iliyo kuwepo.

So kama ndugu zetu wa CUF wali kazania visiwani kama strategy ( which maybe is the reason baadhi ya watu wana kiona ni chama cha kidini kutokana na ukweli kwamba visiwani 99% ni Waislamu ni lazima watambue kwamba vyama vinavyo lenga kundi fulani haviwezi kufanikiwa kwa sababu Tanzania hamna dominant group iwe kwenye dini au kabila. It's time they did something about this. Sasa hivi siasa Tanzania ina under go some chances na ita fika kipindi kuta kuwa na vyama viwili au vitatu vyenye nafasi yoyote ya kushinda. Wasipo angalia CUF wata jiondoa kwnye ramani ya siasa na kupunguza nguvu yao kabisa.

*With that said lakini tusi sahau kwamba CUF waka 2005 kwenye uchaguzi wa raisi ilishika nafasi ya pili. Mwaka huu tena ndiyo ita kuwa hukumu ya ita fanyaje.
 
LABDA TUCHAMBUE HAYA MAJINA YA WAGOMBEA WAO CUF YA UBUNGE KUTOKANA NA GEOGRAFICAL AREAS NDIO TUWEZE KUPEMBUA UKABILA NA UDINI WA CUF
Tanga
ni Mussa Mbarouk (Tanga Mjini); Remmy Shundi (Handeni); Bakar Mbega (Mkinga); Abubakar Bakari (Muheza); Gogola Gogola (Mlalo); Fabi Sozi (Bumbuli); Abassy Mkankamghanga (Lushoto), Jumaa Magogo (Korogwe Mjini); Mohamed Asiu (Korogwe Vijijini) na Omar Masomaso (Pangani).

Kilimanjaro
ni Awadh Mwarabu (Same Magharibi). Mtwara ni Hassan Abdallah (Mtwara Mjini); Katani Katani (Tandahimba); Clara Mwatuka (Masasi); Mtikita Mtikita (Lulindi); Hakika Maarifa (Newala) na Chikamba Wanainuka (Mtwara Vijijini).

Lindi
ni Salum Barwany (Lindi Mjini); Ayubu Nassor (Mchinga), Khalfan Mandanje (Mtama); Madaraka Beyi (Liwale), Nanjase Nanjase (Nachingwea), Abubakary Kondo (Ruangwa), Seleman Bungara (Kilwa Kusini) na Said Manoro (Kilwa Kaskazini).

Tabora
ni Edward Zombwe (Urambo Mashariki), Kirungi Kirungi (Urambo Magharibi), Hassan Mwigwayasila (Igalula), David Kassoga (Tabora Kaskazini), Kidumla Kidumla (Bukene), Dominic Kizwalo (Nzega) na Abdallah Katala (Sikonge).

Kagera
ni Christina Kasimbazi (Bukoba Vijijini), Nicolaus Batalingaya (Karagwe), Twaha Taslima (Bukoba Vijijini), Hamida Issa (Biharamulo Magharibi), David Tibanywana (Chato) na Yahya Ndyema (Nkenge).

Arusha
ni Ghariby Baalawy (Arusha Mjini), John Pallangyo (Arumeru Mashariki), Adella Kileo (Arumeru Magharibi) na Navaya Ndaskoi (Monduli).

Mara
ni Mustafa Wandwi (Musoma Mjini), Vedastus Msita (Mwibara) na Wilegi Songambele (Bunda).

Pwani
ni Jafar Ndende (Mkuranga), Seif Porwe (Kibiti), Ali Kihambwe (Rufiji), Wahabi Twalut (Mafia), Adui Kondo (Kisarawe), Zahoro Vuai (Bagamoyo) na Miraj Mtibwiliko (Chalinze).

Shinyanga
ni Mwalimu Mbukuzi (Shinyanga Mjini), Khanipha Ruhinda (Maswa Mashariki), Seif Baya (Maswa Magharibi), Jackson Deodatus (Bukombe), Shashu Lugeye (Solwa), Sauda Kasiga (Msalala), Hamisi Makapa (Kahama), Creoface Magere (Mbogwe) na James Matinde (Kisesa).

Kigoma
ni Fatma Kinguti (Kigoma Mjini), Salum Kajanja (Buyungu), Athumani Hamisi (Muhambwe), Rashid Kaduguda (Kasulu Magharibi) na Ibrahim Magara (Buhigwe).

Mbeya
ni Ezekia Mtafya (Ileje), Asukile Kabango (Mbozi Magharibi), Nkuyuntila Siwale (Mbozi Mashariki), Yusuf Said (Kyela) na Shaweji Salinyambo (Mbarali).

Iringa
ni Mussa Fufumbe (Isimani), Godfrey Hongele (Njombe Kaskazini), Stanley Fwila (Njombe Kusini) na Jacob Mhanga (Njombe Magharibi).

Manyara
ni Rashid Mgaya (Babati Mjini), Juma Nyeresa (Kiteto) na Eliseus Amedeus (Mbulu).

Ruvuma
ni Mazee Mazee (Tunduru Kaskazini), Mohammed Mambo(Tunduru Kusini) na Hassan Mtwangambati (Namtumbo).

Morogoro
ni Willy Dikundile (Kilosa Kati), Abeid Mlapakolo (Morogoro Mjini) na Blandina Mwasabwite (Morogoro Kusini Mashariki).

Mwanza
ni Komanya Athanas (Buchosa), Mbaraka Chiru (Sengerema), Peter Malebo (Geita), Oscar Ndalahwa (Busanda), Andrea Mkanga (Nyang'hwale), Abdallah Mtina (Misungwi), Omar Mbalamwezi (Nyamagana), Mtebe Msita (Ukerewe), Ligawa Ndalahwa (Kwimba) na Julius Samamba (Sumve).

Katavi
ni Aram Ndimubenya (Mpanda Mjini), Athumani Kababende (Mpanda Vijijini) na Abbas Ally (Katavi).

Singida
ni Rashid Mindicar (Singida Mjini), Sizimwe Kanyota (Singida Kaskazini) na Dalfina Patric (Singida Magharibi).

Dodoma
ni Ngomoka Joseph (Mtera), Ngomoka William (Chilonwa), Yahya Deni (Kondoa Kaskazini), Hassan Missanya (Kondoa Kusini). Tabora ni Kapasha Kapasha (Tabora Mjini).
 
brother kama cuf hakina mvuto sasa twambie chadema kilipata kura ngapi huko bara mwaka 2005 na cuf walipata ngapi.
pili kwanini ccm hawakubali tume huru ya uchaguzi kama kweli hakina mvuto.
 
Na zile kofia zao wanaziita baga la shia!

Hii mada nilikuwa sitaki kuchangia kwa sababu mna upuuuzi mtupu watu hawaongei "sense but nonsense" lakini Mkuu ulipotaja habari za kofia (sijuwi kama zinaitwa hivyo kwenu) nikakumbuka Mzee wa Kiraracha alipokuja visiwani akapewa yake mpaka leo anayo, alikuja Nyerere naye akapewa yake alipokanyaga Mrima tu akaivua...juzi nilipata mpya kumuona Dr.Slaa, akiwa kibanda maiti, Zanzibar na kofia yake..ha! ha! ha!
 

Attachments

  • slaa zanzibar.JPG
    slaa zanzibar.JPG
    176.6 KB · Views: 77
brother kama cuf hakina mvuto sasa twambie chadema kilipata kura ngapi huko bara mwaka 2005 na cuf walipata ngapi.

Mkuu hakuna wa kujibu swali hilo. Vijana malimbukeni wanaokuja humu na sumu zinazopambwa na vyombo vya habari (Products za chuo cha Nyegezi) wanataka tuamini kuwa CUF ni chama cha kiislam lakini PADRI akigombea Urais hapo poa tu! Hakuna zaidi ya ulimbukeni na chuki za kupandikiza.

Huyo Zitto Kabwa alipewa ubunge na CCM katika jitihada za kukivunja nguvu chama cha CUF bara na kuifanya chadema chama kikuu cha upinzani. Muulize aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini jinsi alivyolalamikia wasimamizi kuwa upande wa Zitto - yalikuwa ni maagizo dogo apewe cheo kuondoa sura ya Ukabila na Ukristu ndani ya Chadema. But wanajisumbuwa, hiyo Chadema ni NGO ya Mbowe na Mkwe wake Mtei - aliyefuatilia uchaguzi wao mkuu analijuwa hilo.
 
Kama:
CUF = Upemba na Uislam
CHADEMA = Ukabila na Ukristo

Kwanini CCM isitawale Milele!
 
Watu waliostaarabika kama Watanzania hawawezi kujadili ubaguzi wa kidini,
na ukimuona mtu anajadili mambo ya udini, ukabila au rangi ya ngozi ya mtu
basi ujue kuwa hana la maana la kujadili. Tanzania niijuayo mimi haina ubaguzi
wa rangi ya mtu, dini yake au kabila lake wote ni sawa tu mbele ya Taifa hili.

Tazameni nchi zilozunguka Tanzania na migogoro yao isiyomalizika yote ni
kwa sababu ya ubaguzi ama wa rangi udini au ukabila.
 
kilichowaponza ni jinsi walivyoanza kujitambulisha kwenye jamii, kwa mfano ushakuja na kauli kama jino kwa jino, cjui unategemea nini!
 
Hivi kwa nini Chama cha Wananchi (CUF) kimekosa umaarufu kiasi kwamba kilikosa kiti hata kimoja bara 2005? Wabara wengi hawakioni kama Chama mbadala bali Chama Cha Waislamu kutokana na viongozi wake almost wote kuwa Waislamu! Je, ipi hasj ni sababu? 1. Kwa sababu ya Udini? 2. Hujuma za CCM? 3. Sera mbovu? 4. Lugha ya vitisho, eg tusipoingia Ikulu damu itamwagika? 5. Viongozi wake hawauziki? 6...?


Huku bara CUF hawana dira wala muelekeo, hizo sababu ulizozilist zinawaua mbaya, CUF ni chama cha kisiwani(zenji), huku bara Lipumba anaongea pumba tu hana sera.
 
Back
Top Bottom