Hivi kwa nini Chama cha Wananchi (CUF) kimekosa umaarufu kiasi kwamba kilikosa kiti hata kimoja bara 2005? Wabara wengi hawakioni kama Chama mbadala bali Chama Cha Waislamu kutokana na viongozi wake almost wote kuwa Waislamu! Je, ipi hasj ni sababu? 1. Kwa sababu ya Udini? 2. Hujuma za CCM? 3. Sera mbovu? 4. Lugha ya vitisho, eg tusipoingia Ikulu damu itamwagika? 5. Viongozi wake hawauziki? 6...?
Nakerwa saaaaaaaaaana na hoja za udini.tufikirie utaifa kwanza jamani, dini ni jambo binafsi kati ya mtu na muumba wake
Kweli mkuu chuki zitakuua. Hivi mwaka 2005 CUF ilishika nafasi ya ngapi? Ukristo aka udini wako ndo unakuponza hata usione kama unaandika pumba humu JF. Visiwani kuna watu wachache sana kiasi ambacho hata kama wangepigia kura CUF wote wasingepata nafasi ya pili. Kwenye nyekundu hapo, nilishawahi kuandika huko nyuma kuwa wewe ni mdini sana, tena sana, na namaanisha. Naleo hii umedhihirisha. Tena kweli umedhihirisha. Shame on you.Hivi kwa nini Chama cha Wananchi (CUF) kimekosa umaarufu kiasi kwamba kilikosa kiti hata kimoja bara 2005? Wabara wengi hawakioni kama Chama mbadala bali Chama Cha Waislamu kutokana na viongozi wake almost wote kuwa Waislamu! Je, ipi hasj ni sababu? 1. Kwa sababu ya Udini? 2. Hujuma za CCM? 3. Sera mbovu? 4. Lugha ya vitisho, eg tusipoingia Ikulu damu itamwagika? 5. Viongozi wake hawauziki? 6...?
Hivi ninyi wakereketwa wa CHADEMA madai yenu ya kukipakazia CUF ni cha dini fulani ati kwa sababu wanachama wake wengi wanavaa vikofia au wana majina yanayo fanana na Uislamu ni lini watu wenye majina yanayofanana na Ukiristo walitaka kujiunga na CUF wakakataliwa uanachama?
Kwanza tangu uchaguzi wa 2000 na 2005 CUF walikuwa namba 2 ktk matokeo ya kura zilizopigwa! CHADEMA kama munataka upinzani ushinde kupakaziana hakusaidii chochote! sana sana mutasababisha hasira kwa WAISLAMU ambao mpaka sasa hivi tunapoongea hawana chama maalum wakipigie kura CUF, CCM au wapige kura za MARUHANI kama walivyofanya wana CUF huko PEMBA miaka ya nyuma!
Lyatonga Mrema 1995 hakuna aliyefikiri angekosa Urais kutokana na mbwembwe na nyota yake ya wakati huo kuvuma akisaidiwa na jopo la mashushushu kama Mabere Marando, Tenga, James Mbatia na wenzao wote lakini ameishia wapi?
CHADEMA nawapa ushauri wa bure! kama munataka DR. Slaa ashinde urais basi muache chokochoko na matusi dhidi ya CUF kwa kupakazia kuwa ni chama cha Waislamu kwani hayo ni matusi dhidi ya Uislamu na waislamu! ni lini Waislamu wa TZ walitangaza rasmi kuwa Profesa Lipumba ni chaguo la Mungu? kama walivyodai Wakiristo 2005 kuwa Kikwete alikuwa chaguo la Mungu! jee! sasa munakiri kuwa Mungu alikosea kumchaguwa Kikwete? au na sasa Mungu amebadilisha uwamuzi wake na ameamuwa kutuchagulia PADRI WILBERD SLAA kuwa Rais wetu mpya?
Hii mada nilikuwa sitaki kuchangia kwa sababu mna upuuuzi mtupu watu hawaongei "sense but nonsense" lakini Mkuu ulipotaja habari za kofia (sijuwi kama zinaitwa hivyo kwenu) nikakumbuka Mzee wa Kiraracha alipokuja visiwani akapewa yake mpaka leo anayo, alikuja Nyerere naye akapewa yake alipokanyaga Mrima tu akaivua...juzi nilipata mpya kumuona Dr.Slaa, akiwa kibanda maiti, Zanzibar na kofia yake..ha! ha! ha!