One and Only
Senior Member
- Mar 7, 2011
- 161
- 62
Habari zenu great thinkers, naomba msaada wa mawazo mwenzenu, nina bibi yangu amegoma kula na hataki kuongea na mtu yoyote hapa nyumbani kisa kijijini kwao wazee wenzake wote wameenda kupata kikombe cha babu kasoro yeye kwa hiyo anataka kupelekwa loliondo. Mtu mwenyewe anamatatizo makubwa ya miguu, je kuna ndege za kwenda loliondo na kama zipo tutapata wapi? Apelekwe yaishe maana imekuwa taabu na hawezi kusafiri mwendo mrefu na gari anaumwa sana miguu. Nawasilisha janvini, msaada wenu jamani