Lego
Senior Member
- Aug 31, 2016
- 114
- 115
- Thread starter
- #21
asante kwa maelezo kindakidankiUtatakiwa ufungue petition (madai) mahakamani kwa ajili ya ugoni.
Utadai malipo ya madhara (kitu kama fidia iv) dhidi ya uliyemkamata.
Ila sasa lazima uthibitishe uhalali wa ndoa yako na mwanamke huyo au mwanaume huyo kisheria. Yaani iwe ni ndoa halali kabisa na pia hamjaachana. Pia huyo mtu asiwe amedanganywa na mkeo kuwa hana mume au kinyume chake.
Pia mahakama katika kutoa maamuzi itaangalia kama mlikuwa mnaishi pamoja au laa (wanandoa)
Halafu pia isiwe ni mpango uliosukwa na wawili hao (mke na mume ili kumfumania mtu wa tatu)
Halafu mwanaume au mwanamke asiwe ameruhusu kitendo kifanyike (condone) halafu akageuka baadae na kuanza kudai malipo.(NO person shall benefit from his own wrong)
Lazima uwe umefumania wakifanya. Actually performing. Yaani infragrante delicto.
(Kitendo tu cha kuwaona wanakiss au wamekaa pamoja kwenye sofa au wamo chumbani au wanakumbatiana haitoshi kuthibitisha ugoni kisheria (hii inategemea pia na utamaduni wa jamii husika). Etc.
NB: LAZIMA UHALALI WA NDOA KISHERIA UTHIBITISHWE KWANZA(NA HAPA NDIO MUHIMU), KAMA KWELI MMEOANA NA HUYO UNAYEDAI NI MKEO AU MUMEO UMEMFUMANIA NA MTU MWINGINE, NDO HAYO MENGINE YANAFUATA.
PIA HAUWEZI KUDAI MALIPO YALEYALE KUPITIA UGONI AMBAYO PIA UNAYADAI AU UMEYADAI KUPITIA TALAKA KAMA KWA MFANO UNATAKA KUTALAKIANA NA MPEZI WAKO.
Hivyo basi utadai tu gharama kwenye ugoni zile ambazo haujazidai kwenye talaka.
Nimechoka
Nawasilisha.