Elections 2015 Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...

kama naiona Chadema itakavyopeta 2015. Mnamweka mwizi ndo awe rais? Wewe pasco na wasiwasi na thinking capacity yako!
Mkuu Chimunguru, huna haja ya kuwa na wasiwasi na thinking capacty yangu, kwa kifupi iko very low ila hii ndio level ya wapiga kura wetu.

Hakuna kitu kizuri kama kuwa ma matumaini na matarajio makubwa kuwa 2015 ni Chadema, itatinga ikulu ya magogoni, nilichotoa hapa ni angalizo kuwa kuwa iwapo CCM itamsimamisha EL uchaguzi wa 2015, nyie Chadema na wote wenye matarajio kama yako, Ikulu mtaishia kuisikia kwenye bomba!.

Kwa vile wengi humu mmehamanika na great expectations za ikulu, ikitokea mkaokosa, mtaishia kukata tamaa na hivyo kuwa tayari kwa lolote, hivyo angalizo hili ni kuwaandaa watu kama nyinyi kwa kama ni EL, 2015 ni CCM tena!.
 
Nakubaliana na maneno yako Pasco, lakini yamenifanya nianze kuwaza jingine... the fall out kati ya JK na Lowassa. JK anafahamika kama mtu anayependa popularity na Lowassa 'dikteta' anayependa kusukuma mambo yaende. Hivi hii ndiyo sababu iliyowakosanisha?
Mkuu, Mpita njia, JK ni populist leaders, ma populist leaders wote wanapenda sana sifa kwa kuimbiwa nyimbo za shangwe na mapambio hata kama nathing is realy done!. EL yeye ni action oriented leader anayetaka kuona na kuhakikisha the work is done.

Kwenye ile team ya Boys II Men, EL alimu outshine JK vibaya sana!. JK akitembelea mahali, hupokelewa kwa shangwe na kupewa taarifa ya maendeleo yenye maneno mazuri kwenye makaratasi with nothing on the ground, yeye huridhika na taarifa na kuendelea na ziara, tena anapangiwa very tight schedule, ili asione ukweli!. EL alipokea taarifa na baada ya hapo alilazimisha kwenye site to witness with his own eyes na hapo ndipo tofauti ya viongozi wasemaji na watendaji.

Ilifikia point, huko mikoani wakisikia JK anakuja, hawana wasiwasi, wameshamjua anapenda nini, anatayarishiwa ile kitu roho inapenda, akifika ni hutuba tuu za kwenye makaratasi jioni ni mambo yetu yalee..kazi kwisha!. Lakini wakisikia anayekuja ni EL, huko kunakuwa na mtafutano, watu hawalali, maana jamaa sio mchezo!, japo na yeye pia kama binadamu, mambo yetu yale naye anayakwakwe, lakini angalau kazi inaokekana japo nae pia ni kazi na dawa!.

Katika mazingira kama haya, bwanamdogo una mu outshine boss wako, nini kitatokea?, ni kuwa flushed out!. Na baada ya kumflush EL, wengi mmeshuhudia jinsi serikali ya JK ilivyo flop!.
 
mimi naona kuwa sera na nia ya dhati ya kuitekeleza hiyo sera ndio muhimu zaidi. sera ni lazima itokane na wanachi wenyewe yaani watanzania. Tanzania ina watu wengi sasa ukisema kuwa EL ndio pekee anayeweza unakuwa kama unafanya kampeni. hiyo ni subjectivity.
jambo la maana ni sote tujadili kuwa tanzania tunataka nini hasa kilimo au elimu kwanza n.k. matokeo ya mijadala yetu ni kuwepo kwa sera. hapo tutaweza kumchagua mtu atuongoze kupitia sera hizo kufikia malengo yetu. mtu si hoja kwanza. EL si mtume wala si nabii hata ufikie kusema ni yeye pekee.
 
Mkuu, Mpita njia, JK ni populist leaders, ma populist leaders wote wanapenda sana sifa kwa kuimbiwa nyimbo za shangwe na mapambio hata kama nathing is realy done!. EL yeye ni action oriented leader anayetaka kuona na kuhakikisha the work is done.

Kwenye ile team ya Boys II Men, EL alimu outshine JK vibaya sana!. JK akitembelea mahali, hupokelewa kwa shangwe na kupewa taarifa ya maendeleo yenye maneno mazuri kwenye makaratasi with nothing on the ground, yeye huridhika na taarifa na kuendelea na ziara, tena anapangiwa very tight schedule, ili asione ukweli!. EL alipokea taarifa na baada ya hapo alilazimisha kwenye site to witness with his own eyes na hapo ndipo tofauti ya viongozi wasemaji na watendaji.

Ilifikia point, huko mikoani wakisikia JK anakuja, hawana wasiwasi, wameshamjua anapenda nini, anatayarishiwa ile kitu roho inapenda, akifika ni hutuba tuu za kwenye makaratasi jioni ni mambo yetu yalee..kazi kwisha!. Lakini wakisikia anayekuja ni EL, huko kunakuwa na mtafutano, watu hawalali, maana jamaa sio mchezo!, japo na yeye pia kama binadamu, mambo yetu yale naye anayakwakwe, lakini angalau kazi inaokekana japo nae pia ni kazi na dawa!.

Katika mazingira kama haya, bwanamdogo una mu outshine boss wako, nini kitatokea?, ni kuwa flushed out!. Na baada ya kumflush EL, wengi mmeshuhudia jinsi serikali ya JK ilivyo flop!.
Sasa Pasco hapa ndipo tatizo jingine la Lowassa litakapotokea. Sysyem ya uongozi iliyopo hivi sasa imezoea kwua na kiongozi mpenda sifa, nao wakabibea kwenye kusifian kwa sababu walijua kuwa hicho ndichom kipimo cha utendaji kazi wao. Kuna tatizo la jumla yanapokuja mabadiliko, hasa mabadiliko ya ghafla. Kutoka kuwa kiongozi bingwa wa kusifia, hadi kuwa kiongozi mchapa kazi ili kuonyesha matokeo ni jambo gumu kwa aina ya watu, si tu viongozi, tuliopo Tanzania leo hii. Ndio maana awali nilisema kuhusu 'team work'. Lowassa anaweza akaingia na udikteta wake na hapo ndipo matatizo yake yataka[poanzia kwa sababu ya ukinzani (si upinzani) atakaokumbana nao.
lakini, hilo ni kama akiingia. Kuna wengiw aliopo katika mfumo wa uongozi hivi sasa wanaofahamu hulka ya Lowassa, nakuhakikishia, hawa wanaweza kuungana ili kuhakikisha shindi kwa sababu wanajua chini yake hawataweza. Sijui ni kwa nini unaona kwua njia ni nyeupe kwa Lowassa katika mazingira kama haya
 
Last edited by a moderator:
mimi naona kuwa sera na nia ya dhati ya kuitekeleza hiyo sera ndio muhimu zaidi. sera ni lazima itokane na wanachi wenyewe yaani watanzania. Tanzania ina watu wengi sasa ukisema kuwa EL ndio pekee anayeweza unakuwa kama unafanya kampeni. hiyo ni subjectivity.
jambo la maana ni sote tujadili kuwa tanzania tunataka nini hasa kilimo au elimu kwanza n.k. matokeo ya mijadala yetu ni kuwepo kwa sera. hapo tutaweza kumchagua mtu atuongoze kupitia sera hizo kufikia malengo yetu. mtu si hoja kwanza. EL si mtume wala si nabii hata ufikie kusema ni yeye pekee.
Mkuu Mzamifu, kama ni kujadili, tumeshajadili sana humu, yote usemayo ni kweli, ili amini usiamini, kwa tuliyofika sasa, Watanzania, hawachagui seri, chama, itikadi wala ilani!, Watanzania wanachagua mtu!, EL ni maoni yangu kama mtu pekee, ila na wewe kama unaye pia mlete tumjadili, nilichosema mimi, kwa hapa tulipofikishwa sasa, EL hana mpinzani ndani na nje ya CCM, he is the one and only!.
 
Kwa kweli huu ni zaidi ya ushabiki. 2015 watu wengi hawataki CCM no matter anagombea nani? Ukitaka kuhakikisha jinsi watu wanavyoichukia CCM nenda sehemu yeyote public hata unaponunua gazeti jifanye unaisifia CCM utaona macho ya watu. Utatamani ukimbie.
 
Sasa Pasco hapa ndipo tatizo jingine la Lowassa litakapotokea. Sysyem ya uongozi iliyopo hivi sasa imezoea kwua na kiongozi mpenda sifa, nao wakabibea kwenye kusifian kwa sababu walijua kuwa hicho ndichom kipimo cha utendaji kazi wao. Kuna tatizo la jumla yanapokuja mabadiliko, hasa mabadiliko ya ghafla. Kutoka kuwa kiongozi bingwa wa kusifia, hadi kuwa kiongozi mchapa kazi ili kuonyesha matokeo ni jambo gumu kwa aina ya watu, si tu viongozi, tuliopo Tanzania leo hii. Ndio maana awali nilisema kuhusu 'team work'. Lowassa anaweza akaingia na udikteta wake na hapo ndipo matatizo yake yataka[poanzia kwa sababu ya ukinzani (si upinzani) atakaokumbana nao.
lakini, hilo ni kama akiingia. Kuna wengiw aliopo katika mfumo wa uongozi hivi sasa wanaofahamu hulka ya Lowassa, nakuhakikishia, hawa wanaweza kuungana ili kuhakikisha shindi kwa sababu wanajua chini yake hawataweza. Sijui ni kwa nini unaona kwua njia ni nyeupe kwa Lowassa katika mazingira kama haya
Mkuu Mpita Njia, hili, hili wewe unaloliona kama ni tatizo kwa EL, hiyo ndio strength yake!. Kikweli jamaa akiingia, kuna viongozi wanaweza mpaka kula bakora mbele ya wake zao!. We have had enough of the nonsense, we now need a no nonsense man! EL is the one and only kwa upande wa CCM!.
 
Kwa kweli huu ni zaidi ya ushabiki. 2015 watu wengi hawataki CCM no matter anagombea nani? Ukitaka kuhakikisha jinsi watu wanavyoichukia CCM nenda sehemu yeyote public hata unaponunua gazeti jifanye unaisifia CCM utaona macho ya watu. Utatamani ukimbie.
Mkuu Mpitwanga, usemayo ni kweli, angalau wewe unasikilizia sauti za watu hizo sehemu public jinsi wanvyoichukia CCM, mimi nimezama field na kushuhudia jinsi Chadema inavyopendwa, mikutano yake inafunga funika bovu!, tatizo tukija kwenye sanduku la kura, hatuwaoni hao watu unaowasema, wengi ni wasemaji wazuri na walalamika wakubwa huko kwenye vijiwe vya kahawa, lakini sii wapiga kura hao!. Hao wanaolalamikia CCM ni furahisha genge tuu, wengi wao midomoni ndio Chadema, lakini mioyoni ni CCM, haswa kwa kuzingatia wengi wao pia ni kulipa fadhila za T-shirt, kofia na ile shibe ya siku moja!.

Ila pia chuku kubwa kwa CCM ni shauri ya udhaifu wa JK, kwa vile EL sii dhaifu, akisimama yeye, ile chuki yote dhidi ya CCM itayeyuka na kugeuka upendo kwa CCM na utashangaa jinsi CCM itakavyoshinda kwa kishindo mwaka 2015 but only if itamsimamisha EL, vinginevyo bila EL, tutashuhudia anguko kubwa la CCM kwa kufa kifo mende huku kinajiangalia!.
 
Mkuu Mzamifu, kama ni kujadili, tumeshajadili sana humu, yote usemayo ni kweli, ili amini usiamini, kwa tuliyofika sasa, Watanzania, hawachagui seri, chama, itikadi wala ilani!, Watanzania wanachagua mtu!, EL ni maoni yangu kama mtu pekee, ila na wewe kama unaye pia mlete tumjadili, nilichosema mimi, kwa hapa tulipofikishwa sasa, EL hana mpinzani ndani na nje ya CCM, he is the one and only!.
Mkuu pasco mimi pia nimekuelewa nami kwa sehemu naona EL anakidhi kwa kiwango fulani kwa mtazamo wangu lakini wavumao baharini ni papa lakini wengine wamo. ndo nikasema hebu tuone kwanza tunataka nini kama alivoshauri mwalimu mwaka 1995. tunataka rais awe mtu mweye sifa zipi awe rais. watu ambao kisirisiri wanafanya vitu sasa hivi ili kutushawishi kuwa wanafaa kkugombea urais ndani ya CCM wanatakiwa waangaliwe kwa makini sana. wanaweza kuwa hatari baadae.
 
Pasco wa JF........Lowassa for president 2015.
Rais 2015 lazima atoke kaskazini.

:spy::spy::spy:

Mimi sikatai obsession ya Pasco kwa Lowassa, kila mtu anayo obsession yake at one point, it is natural. However, it become unnatural and a bit weird kama Mtu huyo anaelezewa kama man alone from a failed system. System ambayo haijaweza kufanya yale yaliyotarajiwa na wengi.

A system where, individuals ndani ya systems are biting each other, sabotaging each other, making deals with devils in and out of that same system.

An individual who was accused of getting across Procurement procedures, altering the process and causing a massive economical shake to the country, accepted the accusation as major and resigned - of-course while :A S cry:, who wouldn't.
Hata waziri wa uchukuzi wa Znz ali-resign juzi huku akinung'unika.

Ukikubali ku-resign, maana yake umekubali kosa. Issue ya kuthibitishwa mahakamani ni swala jingine kabisa. nani asiyejua kwamba kupelekwa mahakamani hapa Tz ni mapaka mkulu aamue?? Hata majizi yanaambiwa yarudishe fedha yazizokwiba.

Mkuu, huyu jamaa hasafishiki.....he has been around for a long long time.....amefanya nini?? usiongelee shule za kata kwasababu that is a disgrace to education system in Tanzania...what else?

Mkuu Bigirita, mtazamo wako ni wa kisomi zaidi na umekweenda deep, mimi nazungumza lugha ya wapiga kura!, wapiga kura wetu, hawapigii kura system, hawapigii kura vyama, hawapigii kura sera, wao wanapigia kura mtu!, nikauliza na ninauliza na kuuliza tena, kama CCM ikimsimamisha EL,who else can dare challenge him?, ndio maana nimesema, uchaguzi wa 2015, kama CCM ni EL, then matokeo ni CCM tena, EL ndani ya CCM hana mshindani, na nje ya CCM, hana Mpinzani!.

Hizi hoja za EL hasafishiki hazina mashiko!, kwani Wapiga kura wanachagua wasafi?. JK alipoingia na kuchaguliwa kwa 80%, aliikuwa na usafi gani?!. Watanzania wanachagua sura tuu, hapo ulipo, hebu funga macho, imagine unaiona sura ya EL kwa CCM, hebu ifikirie sura gani ya nani mwingine anaweza kusimama nae akachaguliwa?.


Mimi nawazungumzia Watanzania hawa wanaochagua sura kuwa kama kwa uchaguzi wa 2015, sura ya CCM ni EL, then matokeo ni CCM Tena!.
 
Pia naona elimu ya urai yafaa kutolewa kuanzia sasa. vyama hiari, vyombo vya habari, majukwaa ya kijamii, asasi mbalimbali vianze kutoa elimu ya uraia kupitia majukwaa yao kwa kasi ili kupitia elimu hiyo ifikapo 2015 wanachi waweze kushiriki wote kufanya uamuzi sahihi. kwa kweli umefika wakati wa kuzaliwa upya. tunataka maendeleo, tunataka maelewano, amani na utulivu zaidi tunataka haki na kila mtu atimize wajibu wake . hatutaki ufisadi kamwe!
 
Mkuu pasco mimi pia nimekuelewa nami kwa sehemu naona EL anakidhi kwa kiwango fulani kwa mtazamo wangu lakini wavumao baharini ni papa lakini wengine wamo. ndo nikasema hebu tuone kwanza tunataka nini kama alivoshauri mwalimu mwaka 1995. tunataka rais awe mtu mweye sifa zipi awe rais. watu ambao kisirisiri wanafanya vitu sasa hivi ili kutushawishi kuwa wanafaa kkugombea urais ndani ya CCM wanatakiwa waangaliwe kwa makini sana. wanaweza kuwa hatari baadae.
Mkuu Mzamivu, ni kweli wavumao bahari ya CCM ni papa, na wengine wapo, hao wengine wavumao CCM, hao ni papa usingizi, EL ni papa upanga!. Hoja ya kutoteuliwa EL ni moja tuu, nayo ni kuhusu afya yake na hapa ndipo kifo cha mende kwa CCM kitaifika huku kinajiangalia!.

Hao wanaofanya kisirisiri, wanasumbuliwa tuu na njaa zao, ukimuondoa EL, then Membe, tena Membe mwenyewe as Membe sii lolote sii chochote bila back up ya EL!, CCM itapigwa chini kama kuupuliza unyoya!.

Ile enzi ya Mwalimu ya kuwapima wataka urais kwa vigezo, imepita, kwa sasa concentration ya CCM sio jinsi ya kuendelea kutawala, bali jinsi ya kujiokoa, kwa hiyo mgombea wa CCM ajae ni mtu atakayeweza kuikoa CCM, nothing more, nothing less!.

Kufuatia mimi kutokuwa na chama na sifungamani na chama chochote, nimekuwa nikipigia kelele haja ya sisi wana jf kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kuwa pamoja na mabaya yote ya CCM, pia kuna mazuri ambayo CCM imelifanyia taifa hili!. Sambamba na mazuri hayo, pia hakuna ubishi, CCM imeoza na kunuka rushwa huku viongozi wake wakigubikwa na ufisadi wa kutisha!, lakini ndani ya CCM hili hili lililooza na kunuka rushwa na ufisadi, bado kuna viongozi wachache wa CCM ambao ni watu safi, waadilifu na hawana uchafu wala tuhuma zozote za ufisadi na hawana hata chembe ya harufu ya rushwa!.

Mfano wa watu safi ndani ya CCM na wasio na mawaa yoyote, wenye sifa za kutwaa uongozi wa taifa hili ni Dr. Ali Mohamed Shein, huyu ni muadilifu wa hali ya juu, asiye na uchu, kashfa, tamaa au tuhuma yoyote iwe ya ukware, rushwa, ufisadi au majungu yoyote!. Tena kwa kuzingatia bara tumeshatoa rais kwa mara mbili mfulilizo, safari hii ilipaswa kuwa ni zamu ya Zanzibar!. Mtihani pekee ni jee mtu safi huyu, anachagulika?. Jee anaweza kuikoa CCM na kifo kinachoinyemelea?!. Panga pangua, hakuna yoyote mwingine ndani ya CCM anayeweza kupangua mawimbi ya M4C zaidi ya EL!. hivyo 2015 ni ama EL ama CCM..Puu!, chini!.
 
Pia naona elimu ya urai yafaa kutolewa kuanzia sasa. vyama hiari, vyombo vya habari, majukwaa ya kijamii, asasi mbalimbali vianze kutoa elimu ya uraia kupitia majukwaa yao kwa kasi ili kupitia elimu hiyo ifikapo 2015 wanachi waweze kushiriki wote kufanya uamuzi sahihi. kwa kweli umefika wakati wa kuzaliwa upya. tunataka maendeleo, tunataka maelewano, amani na utulivu zaidi tunataka haki na kila mtu atimize wajibu wake . hatutaki ufisadi kamwe!
Kiukweli, hiki ndicho kilichopaswa kufanywa hata kabla ya kuingia mfumo wa vyama vingi na ndicho sasa kinachofanywa na M4C, kuwafunguo macho Watanzania, na ni kwa kuizingatia kasi ya M4C, Watanzania wameamka na 2015, wataipiga chini CCM bila huruma, mkombozi pekee wa CCM dhidi ya kipigo hiki ni EL!.
 
Kwanza, Edward Lowassa si Waziri Mkuu mstaafu. Ni Waziri Mkuu wa zamani aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond. Mawaziri wakuu wastaafu walio hai ni kina Cleopa David Msuya, Salim Ahmed Salim, John Malecela, Joseph Warioba na Frederick Sumaye. Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuwa "mstaafu" na yule "aliyejiuzulu" tena kwa kashfa ya ufisadi. Hivyo bora mumuite waziri mkuu wa zamani na si waziri mkuu mstaafu, kwani Lowassa hakuwahi kustaafu bali kalazimika kuachia madaraka.Kama walivyosema wenzangu, Watanzania tupo karibu milioni 50, hivi tumefilisika kiasi hiki mpaka tuendelee kung'ang'ania wanasiasa wenye kashfa za ufisadi na utajiri usioelezeka na wenye mashaka kama Lowassa? Jibu ni kuwa la hasha, kuna Watanzania na wanaCCM wengi sana waadilifu na wenye uwezo. Ila Lowassa anajulikana kuwa na uchu wa madaraka na kuwapanga watu humu JF na kwingineko kwa kuwapa pesa ili wampambe na wajaribu ku-brainwash Watanzania wasahau tuhuma za ufisadi na za ukosefu wa uadilifu dhidi ya Lowassa.Ni upumbavu mkubwa kujaribu kumtakasa fisadi. Mungu hapendi hilo na kamwe halitafanikiwa.
Mkuu Fareed, mimi nimemwita EL ni waziri mkuu mtaafu, kwa vile hivyo ndivo anavyokuwa addresed officially, msamiati wa "Waziri Mkuu Mjiuzulu", au Waziri Mkuu Mjiengua" bado haujawa adapted, ukipitishwa, tutamuita kwa title yake stahiki!.

Kama ni kweli, EL amepenyeza watu wake humu jf na kuwapa pesa ili wampambe, na ikatokea mimi ni mhitaji wa hizo pesa, jee kuna ubaya wowote kwa mimi kumpamba ili nipate huo ujira?.

Naungano na wewe kuwa "upumbavu mkubwa kujaribu kumtakasa fisadi"!, ila nakuomba kuwa mkweli, mpumbumbavu zaidi ni mimi ninayeyaelezea mema ya mtu anayenyoonyesha vidole tuu vya ufisadi, lakini hana tuhuma zozote za ufisadi mbele ya sheria, hana kesi, yoyote, wala hajawahi hata kuitwa na kuhojiwa kwa jambo lolote kuhusiana na ufisadi!.

Lakini kuna mafisadi ya kiukweli ambayo ni majizi, yalikwapua mifwedha kibao kule BOT kwenye kasfa ya EPA, tena mifisadi hii ilikamatwa readyhanded, sio tuu haikushitakiwa, bali ilibembelezwa, kurejesha walivyokwiba and life goes on, jee mpumbavu hapa ni nani, anawatetea wasio na hatia kwa kunyooshewa tuu vidole, au analiyeyasamehe majizi yaliyokamatwa readyhanded?!.

Tuna viongozi wenye kesi za ufisadi mahakamani, JK alidiriki kupanda jukwaani kuwanadi kuwa hao ni watu safi na kuwaomba wananchi wawachague, jee mpumbuvu ni yupi, huyu anayesema humu jf kuwa EL hana kesi yoyote ya ufisadi popote, au mtetezi wa fisadi mwenye kesi kabisa mahakamani, huku kesi haijaisha, unamsimamisha jukwaani na kumnadi kuwa ni mtu safi?!.

Nimesema mara kibao humu, kama EL ni mchafu kwa ufisadi, CCM wote ni mafisadi, na kati yao mwenye afadhali ndio EL!. Kama ni kweli EL ni mtoaji rushwa mzuri, CCM yote imeoza kwa rushwa, hivyo kwa maoni yangu, ni heri ya mtoaji rushwa ambaye hatimaye utakiona alichokifanya kukuletea maendeleo kuliko asiyetoa rushwa na hana chochote afanyacho kuleta maendeleo na kama kipo, basi hakionekani!.

Chagua moja , "someone who is good for nothing"?, au "someone who is bad, but does something good for the people?!

Mimi nimemchagua a bad guy EL who can do good, na wewe endelea kuwachagua hao hao good for nothing!.
 
Mtoa mada hii sio mara ya kwanza kuiweka Mada ya E.L. kuwania Urais, sijamsikia yeye mwenyewe akisema hicho kitu ila tumeona yaliyotokea Arumeru Mashariki, Nafahamu 1995 ulikuwepo na yaliyotokea Chimwaga uliyaona, JK Mrisho alikuwa wa karibia mwisho kuchukua fomu za kugombea, na matokeo Mkapa akashinda Lowassa alikuwepo mengine yapo hapo chini
Ila nataka niwakumbushe hasa waandishi wa Habari mbona muda bado? na Vyama
(CCM) wana njia zao za kumpata mgombea, kwa wakati huu wapo katika Ngazi ya NEC ambayo ni kutoka kila Wilaya hao ndio wanaweza kuamua nani Rais ajaye kama ni msafi ni wao wala sio Wananchi, au WanaJF Jina likipita hapo ndipo muanze kumkampenia na itakuwa labda May 2015 lakini leo ni kutafuta tuanze kuchangia na uhasama wakati mnajua LOWASSA alishawapiga mkwara kuwa atakayemsema vibaya atakula naye sahani moja, lakini hakusema atakayemsema vizuri atampa nini ila naona wiki hili mmecharuka sana hapa JF
[post=4540994] BOFYA[/post] kuna pdf za KIM KARDASH ambazo nimezipenda km unaweza kuzisoma ok ila nachotaka kukueleza Bw Pasco ni kuwa hata Waandishi wa habari huwa hamtaki kujibu hizi tuhuma km ni za kweli au la sasa Watanzania kuelekea 2015 sio mambumbumbu kuanza kuwapigia kampeni. mapema hii
Mara baada ya kurudi Butiama, 1995, baada ya kuenguliwa kugombea nafasi ya urais, siku moja mapema asubuhi Bwana Lowasa alonipigia simu na kusema yafuatayo:

"Bwana Kasori, naomba uende kumwambia Baba wa taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, aende Monduli kusaidia kusafisha jina langu ili nisikose ubunge kutokana na yale aliyonisema Dodoma". Nilishikilia mkono wa simu (TTCL) kwa zaidi ya nusu saa tukiwa tunazungumza na hatimaye mimi nilipata ujasiri wa kumwambia Bwana Lowasa kuwa siwezi kwenda kusema maneno hayo kwa Baba wa taifa na kwamba akitaka aje Butiama na nitamruhusu waongee ana kwa ana. Nikanyamaza na hatimaye yeye akawa wa kwanza kukata simu. Hiyo ikawa itifaki njema kwangu!

Kesho yake tena asubuhi nilipokea simu, safari hii akawa ni mheshimiwa Mzee Rashidi Mfaume Kawawa. Kwa maneno yake alisema "Bwana Kasori,jana ulizungumza na Edward Lowasa; naomba ufikishe ombi lake kwa Baba wa taifa tafadhali".

Kutokana na heshima ya Mheshimiwa Mzee Kawawa, nilikubali na nikaenda na kabla ya hapo nilimuomba Mzee Kawawa akae karibu na simu ili nimpe jibu muda si mrefu.

Nilimueleza Baba wa Taifa kuwa "Mheshimiwa Edward Lowasa kupitia kwa Mhe. Mzee Rashidi Mfaume Kawawa anaomba usaidie kusafisha jina lake kule jimboni kwake Monduli ili asikose ubunge kutokana na yale uliyomsema katika Kamati Kuu ya CCM Dodoma". Jibu la Baba wa Taifa alilonipa ni kuwa "Nenda umwambie Mzee Rashidi Mfaume Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa"!

Watanzania wote, leo March19, 2008, nawaomba radhi kuwa jibu hilo kwa uzito wa maneno hayo kuwa "Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa" kweli kwa kuzingatia heshima kati ya wazee hao wawili; "Kawawa sikumwambia hivyo"! Badala yake nilimdanganya (nawaomba radhi tena watanzania) jibu nililompa Mzee Kawawa ni kuwa juma lililokuwa linafuata tungekuwa Dar es Salaam na kwamba aje Msasani aongee na Baba wa Taifa. Mhe. Kawawa alikubali.

Nikarudi kwa Baba wa taifa kusema uongo (naomba radhi tena) kuwa "Mzee Kawawa ameomba mzungumze tatizo la Lowasa tutakapofika Dar es Salaam". Baba wa taifa alikubali na akaagiza nimuombe Mhe. mzee Kawawa kuwa Lowasa na Guninita na wapambe wengine wa Lowasa wote wafike Msasani.



Siku ya siku ikafika. Tukawepo Msasani na Mhe.mzee Kawawa akaja. Lowasa hakuwepo! Sababu anazijua mwenyewe.(muulizeni maana nasema ukweli).
Mkutano ulipoanza mzungumzaji wa kwanza nikawa mimi, kueleza lengo la mkutano. Mzungumzaji wa pili alikuwa Baba wa Taifa na swali la kwanza ni kuuliza Lowasa yuko wapi?.

Bila kupoteza wakati Mwalimu alisema "Rashidi , huyu Kasori ananiambai eti niende Monduli nikasafishe jina la Mhe. Lowasa eti asikose ubunge kwamba nilimchafulia Dodoma katika Kikao cha Kamati Kuu ya CCM. Kutokana na ombi lako nilimtuma akuambie usiwe mjinga kama Lowasa. Kasori alikuambia eh?"

Oneni , huko nyuma tayari nilishasema uongo kwa kutosema maneno hayo kwa Mhe. mzee Kawawa. Kweli hilo kurudiwa na Baba wa Taifa kwa Mzee Kawawa mbele yangu lilisababisha kalamu yangu kuanguka, nikatetemeka na nikatokwa na jasho jingi mbele ya hao wazee!!! Bila kutegemea na kwa mshangao mkubwa Mhe. mzee Kawawa alikubali kwa kuitikia "NDIO ALINIAMBIA". Mwalimu akacheka sana!!!! Sababu sijui hadi leo kwa nini alicheka sana.

Kwa kuendelea, Mwalimu alimwambia Mzee Kawawa kuwa "Kasori ana umri mkubwa kuliko Lowasa. Kasori alipata taabu sana kufikisha kwangu ombi la Lowasa na aliniambia kuwa jana yake alikuwa amekataa ombi la Lowasa. Sasa nasema kuwa kwa umri wangu mimi mzee, Lowasa ni mtoto wangu tena mdogo sana. Kwa heshima mliyonayo kwangu na kwa chama cha Mapinduzi mtanishangaa sana mkisikia niko Monduli eti nipo kwenye majukwaa nasafisha jina Bwana Lowasa asikose ubunge.

Kweli Lowasa ni jasiri sana kusema maneno hayo. Hayo ningeambiwa na Kasori tu ningesita kumuamini. Lakini kwamba hata wewe Rashidi ulitumiwa kusema maneno hayo! Huyu Lowasa ni jasiri sana!!. Lakini kwa nini hajatuambia ukweli kuhusu mali hizo ambazo ni nyingi kuliko mimi ambaye nimekuwa Rais wenu kwa kipindi kirefu? Sasa Bwana Rashidi, nakuomba hivi, kamwambie mwenyekiti wa CCM Mhe. Mwinyi aitishe wajumbe wote wa Kamati Kuu, chagueni tarehe na mahali popote Tanzania, mimi nitakuja kumsafisha Bwana Lowasa na nitagharamia mkutano huo kwa hela zangu. Kamwe msitumie hela za chama wala serikali. Monduli sitokwenda,umesikia eh?"

Mkutano ukaisha hapo Msasani. Hadi uchaguzi 1995, unafanyika na kumalizika Baba wa Taifa hakwenda Monduli. Alichukia sana tabia za Lowasa na alimfahamu kama mtu muongo na mwenye kiburi. Hadi Baba wa Taifa anafariki,sikuwahi na hata niandikapo makala hii sijasikia wala kusoma popote ambapo Lowasa anakanusha alivyolombikiza mali akiwa mtumishi wa CCM na serikali kwa muda mfupi kiasi cha kumzidi Rais wa Kwanza !!!

Sasa anatuhumiwa na vyombo vya habari kununua sehemu ya Ranchi za Taifa kwa kuandika majina ya wanafamilia! Kama hilo nalo ni kweli, ningekuwa mimi nisingeota tena kugombea URAIS n.k Tanzania. Bora kuendelea na biashara kwa uwazi kuliko kupitia mgongo au wa serikali au wa chama ( CCM). Huo ndio ushauri wangu kama mwana CCM kwa Lowassa.

Angalia tunavyofanya "total transgression of CCM regulations and ethics." Kamati kuu 1995 ilimwona Mhe. Lowassa hana uadilifu. Mhe. Mkapa baada ya kuingia madarakani baada ya muda si mrefu sijui ni kwa kikao gain cha CCM na taasisi ipi ya serikali akamwona Lowassa ni safi na akamweka katika safu yake ya baraza la mawaziri.

Huyu bwana akaendelea na huo usafi hadi akaukwaa uwaziri mkuu 2005. Yote haya yanatia shaka kama kweli ndani ya CCM na Serikali tuna benki sahihi za takwimu za mienendo kitabia ya wanachama na watumishi wetu kama si kubebana kwa majina tu! Nilinunua gazeti la mzalendo nikampa Baba wa Taifa na aliposoma kuwa Lowassa ni Waziri alimaka AHH!!

Katika hili nabaki nimeduwaa hasa tunapopeana madaraka makubwa ya kuendesha nchi kimzaha tu. Tukumbuke kuwa kwa kila kitu na kwa dini yoyote Mungu huweka wazi mambo mahali na kwa muda atakao yeye.( Time and space) ya Mwalimu J.K Nyerere juu ya Lowassa tuliyapuuza. Sasa Mungu kayaanika! Basi tuone hizi tuhuma za RICHMOND n.k, Mikataba ya Madini, EPA zitakavyoshughulikiwa.

Ni huyu Lowasa leo anasema kanyimwa "Natural Justice" hakuulizwa na kamati , kaonewa, kamati ya Mwakyembe inauonea wivu uwaziri mkuu wake na ni mahiri wa kuchukizwa mikataba mibovu na kudhalilika! Oh kweli?

Hivi Lowassa amewahi kusoma wasifu wa kila mmoja wa hao? Bila kupima uzito, busara na hekima ya maneno yake anasema ameachia ngazi kama alivyofanya Mhe.Alli Hassan Mwinyi, Peter Kisumo, Peter Siyovelwa n.k. Hivi CCM yetu hawa ndiyo viongozi tulio nao ngazi za juu? Wasio sema ukweli? Tukumbuke na kukiri kwa dhati wajibu wa wanachama wa CCM , katika katiba (ccm) inasema 15 (7) " kuwa tayari kujikosoa na kukosolewa…

Watanzania wenzangu haya anayosema Lowasa yanafanana na nukuu niliyoanza nayo? Fikiria nairudia tena "For those winding and crooked courses, are the goings of the serpent, which goes basely upon the belly and not upon the feet!

There is no vile that does cover a man with shame as to be found false and pertifidious" Niharakishe kusema hapa kuwa viumbe vyote ambavyo havikupenda kusema ukweli Mungu aliviadhibu kwa kuvifanya vitembelee matumbo yao milele nyoka wakiwemo! Lowasa, Mwanyika, Hosea na wenzake naomba kama nilivyoanza, tafadhali wasome hiyo nukuu mara kadhaa na waielewe na kuizingatia.

Watanzania wanawashangaa, wanadharau na kuchukizwa na viongozi wasiopenda kusema ukweli kwa maisha magumu waliyo nayo ambayo wao wanawazomea kwa dharau kuwa ni wavivu na wachovu wa kufikiri. Wanasahau kuwa hawa watu wa kawaida ndio wanaozalisha kile kinacholipa mishahara na marupurupu yao.

Kama viongozi wakuu wa CCM, katika hili daima kumbukeni wajibu wenu kwa mujibu wa katiba ya CCM, ibara ya 15 (4) kuwa wakati wote mkweli, mwaminifu na raia mwema wa Tanzania. Onekaneni hivyo kwa vitendo tafadhali. Utaratibu huu wa kusema uongo unadhoofisha amani na utulivu Tanzania.

Hayo niliyasema niko tayari kuyasema bungeni akiwepo Lowasa ikibidi. Hatuwezi kukubali nchi hii kuendelea kuwa na viongozi wa aina hii. WAWE WAKWELI, WASEME UKWELI TU. WANAPOKOSEA HARAKA NA KWA UKWELI NA UNYENYEKEVU WAOMBE RADHI KWENYE VYAMA VYAO, SERIKALINI NA KWA WANANCHI. NI UPUUZI WA HALI YA JUU KUJITETEA OVYO NA KUINGIZA UKABILA ( LOWASSA NA OLE NAIKO) HATA KWA MAKOSA YALIYO DHAHIRI.

Katika mahojiano na TVT Lowassa alikiri kuwa alishindwa kuvunja mkataba wa RICHMOND. Sababu alizitaja. Sawa. Waziri mkuu kama mtendaji mkuu wa Serikali, kwa mujibu wa kanuni za kudumu za utumishi wa umma ( Toleo 1994), kifungu F33, makosa yake kiserikali ni haya yafuatayo; 33( xi) omission which is against public interest. 33(xiii) negligence occasioning loss to the employer ( yaani serikali na taifa kwa ujumla). 33( xiv) gross negligence in the performance of duty.

Kama mtendaji mkuu wa shughuli zote nzito za serikali bwana Lowassa hana namna ya kujitetea kwa makosa hayo yaliyodhahiri ambayo TANESCO imeendelea kudhoofishwa na RICHMOND kwa yeye kuogopa kutumia utaalam nje ya wale aliowaamini. Mbona tuna vyuo vikuu, je, aalivitumia kikamilifu? Mbona kwa maswala yasiyo na maslahi ya maana tumezoea sasa kukodi wataalam wa nje?

Kwanini hakujiridhisha katika maeneo yote hayo?
Tatizo hili ni kubwa sana maana watanzania sasa wanatozwa viwango vikubwa sana kulipia umeme ikiwa ni pamoja na sehemu za uzalishaji zenye kutumia umeme achilia mbali malipo ya capacity charges? Nani anabisha kuwa kwa huu mkataba wa RICHMOND n.k Bwana Lowassa na Wenzake waliweka sahihi za kifo siyo kwa TANESCO tu bali pia cha kuvuruga maendeleo ya nchi yetu na kuendeleza umasikini?
Katika yote haya ambayo yamesemwa, Bwana Lowassa na wenzake wajue kuwa kama watanzania, we have a compelling moral case for complaining against him.

There is also a compelling case that is in Tanzania's self interest.
Recently many trade agreements already have made the poorest countries worse off. Such agreement already have condemned to death thousands of our people . Corporations of whatever name do strip Tanzania of its natural resources leaving behind a trail of environmental devastation etc. This is done through very poor legal frameworks. Nimuhimu tukawa na viongozi waaminifu, waadilifu na wasema ukweli. Kwa haya yanayotendeka, something is fundamentally wrong with our government.

Kwa kila maamuzi tunayoyafanya mara zote tuzingatie ni kwa maslahi ya nani; yale ya Taifa ni kipaumbele cha kwanza. Tuzingatie matumizi mazuri ya rasilimali zetu daima. Duniani ziko serikali nyingi tu ambazo zimevunja mikataba mibovu. Kwa ziara nyingi ambazo viongozi wetu wanafanya na baada ya wanahabari kupigia kelele RICHMOND, kwanini Lowassa huko nje hakutaka kujifunza namna ya kuvunja mikataba mibovu?

Yaani umahiri wake uliishia mkataba wa maji Dar es salaam na kiwanja cha Mnazi Mmoja? Mikakati yetu ya maendeleo imekuwa haileti tija iliyokusudiwa moja ya sababu ikiwa a flawed vision of development. Successful countries have a broader vision of what development entails and a more comprehensive strategy for bringing it about.

It is very unfortunate that in the majority of developing countries Tanzania included the nation – state has been weakened thoroughly! Haya maamuzi yanayofanywa na viongozi kama Lowassa ndiyo matokeo ya kutojua namna ya kuthibiti na kutumia kwa uangalifu fursa za kitu kinaitwa UTANDAWAZI.

Government that attempt to control capital flows find themselves unable to do so, as individuals find ways of circumventing the regulations. A county may want to raise the minimum wage, but discovers it can't, because foreign companies operating there will decide to move to a county with lower wages.
 
Last edited by a moderator:
Mtoa mada hii sio mara ya kwanza kuiweka Mada ya E.L. kuwania Urais, sijamsikia yeye mwenyewe akisema hicho kitu ila tumeona yaliyotokea Arumeru Mashariki, Nafahamu 1995 ulikuwepo na yaliyotokea Chimwaga uliyaona, JK Mrisho alikuwa wa karibia mwisho kuchukua fomu za kugombea, na matokeo Mkapa akashinda Lowassa alikuwepo mengine yapo hapo chini
Ila nataka niwakumbushe hasa waandishi wa Habari mbona muda bado? na Vyama
(CCM) wana njia zao za kumpata mgombea, kwa wakati huu wapo katika Ngazi ya NEC ambayo ni kutoka kila Wilaya hao ndio wanaweza kuamua nani Rais ajaye kama ni msafi ni wao wala sio Wananchi, au WanaJF Jina likipita hapo ndipo muanze kumkampenia na itakuwa labda May 2015 lakini leo ni kutafuta tuanze kuchangia na uhasama wakati mnajua LOWASSA alishawapiga mkwara kuwa atakayemsema vibaya atakula naye sahani moja, lakini hakusema atakayemsema vizuri atampa nini ila naona wiki hili mmecharuka sana hapa JF
[post=4540994] BOFYA[/post] kuna pdf za KIM KARDASH ambazo nimezipenda km unaweza kuzisoma ok ila nachotaka kukueleza Bw Pasco ni kuwa hata Waandishi wa habari huwa hamtaki kujibu hizi tuhuma km ni za kweli au la sasa Watanzania kuelekea 2015 sio mambumbumbu kuanza kuwapigia kampeni. mapema hii
Duh...!, Mkuu Ukwaju, umemaliza kila kitu!. Sina tena kitu cha kuchangia, nimebaki speechless!.

Namumuomba mode, aifunge hii thread, hapa ndio mwisho wake!.


Natoa wito kwa wachangiaji wengine mlioguswa, nawaombeni tusichangie tena uzii huu, baada ya kuzosoma hizo nondo, nawaombeni kuthibitisha kwa sasa ni hands down, nikisubiria tukaribie darajani, ndipo tujadiliane tutavuka vipi!.

Alamsiki.

Pasco.
 
Inaniwia vigumu kila nikitazama safu ya Chadema kumpata wa kumliganisha uzito na huyu bingwa wa uzito wa juu katika medani za siasa ya Tanzania.
lowassa-important.JPG


Nashindwa kupata jibu ni mwana siasa yupi ndani ya chadema ambae atasimama haswa na kuwakinaisha Watanzania wamchaguwe badala ya Lowassa iwapo ataamuwa kugombea kiti cha Urais Tanzania?


Maana najuwa Mbowe hana hamu tena baada ya kugaragazwa vibaya sana na Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2005.

Slaa nae choka mbaya, hana jipya zaidi ya majungu na siasa zisizo na mpango, hata ujumbe kwa Mwema ni ushahidi tosha kuwa kaishiwa kisiasa.

Nilidhani Zitto ataweza kwa kuwa ni damu changa lakini napata mashaka kuwa siasa za ukanda za chadema zitampa fursa ya kugombea, dalili zote zinaonesha chadema wa kanda ya kaskazini hawamtaki kabisa. Kwa hiyo huyu nnamtoa kwenye kinyan'ganyiro.

Shibuda hata akipitishwa kugombea akiambiwa Lowassa anagombea atakataa kuchuana nae.

Ka Mnyika, haka bado sana, hata ubungo inamshinda na sijui kama atashinda tena hata akigombea Ubunge huko. Kwishnei.

Halima Mdee, huyu hana ubavu, huyu akisikia Lowassa anagombea labda ajitafutie umaarufu tu - kwa hiyo huyu nje.

Nani mwingine?

Natamani Lowassa atangaze mapema kugombea 2015 angalau chadema waanze kujitayarisha mapema na mgombea ambae uchaguzi hautokuwa boring, maana hao wote juu Lowassa atawaonea tu.

CCM inatisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom