Kubet ni dhambi?

Kubet ni dhambi?

kubeti ni kama uzinzi, wizi au ulevi

ni kama familia au jamii ya watu wazinifu, mashoga, wasagaji na makundi ambayo yanapambana kwamba wanachokifanya ni haki yao halali na sio dhambi.

watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa...
Kwa kukosa maarifa 🤣🤣🤣 marifa yakowapi?tupe eleza dhambi inatoka wapi ?Wewe hapo usipobeti huwezi ukakizi mahitaji yako ya kila siku.
 
91 -92
 

Attachments

  • Screenshot_20231210_202558_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20231210_202558_Samsung Internet.jpg
    120.3 KB · Views: 30
Onyesha proof
proof ya nini tena?

Mashoga wanatafuta uhalali kwamba wanachofanya ni haki yao na ni halali haina shida kabisa....

Wabetiji nao ni hivyo hivyo...

Ndio maana kuna wanaoona ni sawa na kuna wanao ona si sawa...

Akili za kuambiwa changanya na zako...
 
proof ya nini tena?

Mashoga wanatafuta uhalali kwamba wanachofanya ni haki yao na ni halali haina shida kabisa....

Wabetiji nao ni hivyo hivyo...

Ndio maana kuna wanaoona ni sawa na kuna wanao ona si sawa...

Akili za kuambiwa changanya na zako...
We mtu Akiwa shoga nini kinabadilika katika maisha yako, same as betting, hawavunji sheria, hii sio Afghanistan sio kila mtu anamuamini Mungu wako wa kiarabu... heshimu mipaka ya watu
 
Kubet ni dhambi??

Hellow hellow nakusalimu Tena na Tena

Kuna jambo limenitafakarisha kidogo nimeona nikumegee japo Kwa sehemu halafu nawewe utoe unachokijua kuhusu hilo

Kimsingi Maisha siku hizi yamekuwa na ugumu kidogo kwenye swala Zima la utafutaji iwe ni biashara n.k ushindani umekuwa mkubwa na ndio maana wanaofanikiwa sana siku hizi ni watu wenye talents eg wachezaji mpira , wanamuziki n.k

Tunamwona misso misondo katoka kusini kaja dar kirahis sana Kwa kile alichokua akifanya yawezekana hakuwa anajua kma angefanya kazi Efm siku moja

Na hili limepelekea kugunduliwa Kwa njia nyingi za utafutaji wa pesa Leo hii mchezo wa kubet umekuwa unashika nafasi ya juu sana kama ingekuwa ni hits za YouTube basi ingeshika 01 trends

kwasababu wanaoshiriki huo mchezo wamekuwa wengi na ndio maana Kila kukicha kampuni nyingi za kubet zinaanzishwa ni Kwasababu hata watumiaji pia wapo wengi hivyo watu wenye mitaji wameona ni biashara inayolipa Kwa haraka

Sambamba na Hilo hao wenye mitaji wameona ni biashara inayolipa lakini pia wanaobet nao wameona fursa ya kujipatia pesa za haraka na wakati mwingine ni pesa nyingi ambayo mtu anaweza akatengeneza akiwa ndani na simu yake,

Na kiukweli wapo wengi wanaendesha Maisha mjini Kwa betting tu hakuna kingine mtu ana mtaji wake wa million moja tu anatafuta odds 1.2 ambayo akiamua kuweka kiasi Cha 250,000/= anaweza kuapata 300,000/= hiyo elf 50 ni faida ndani ya muda mfupi kuliko akafungua duka kariakoo Kisha kusubiri wateja na kuanza kulogana Ili kuleta mvuto katika biashara Ili iende n.k

Sasa swala linakuja kwenye dini mbili ambazo ndio zinafahamika sana yaani (Ukristo& Uislam) hili swala la kupata faida ya Namna hiyo inaonekana kama ni kosa na dhambi japo Kwa utashi wa kawaida tu hii ni biashara kama biashara nyingne ambayo mtu angefanya

Yaani anayebet hatofautiani na mwenye duka la simu kwasb wote wanaweka mtaji na lengo ni kupata faida. Na Kwa upande mwingine wote hawa Huwa wanakumbana na hasara pia

Ni kwanini huu uwekezaji ambao mtu ameamua kuufanya uonekane ni dhambi au halamu kama wengine wanavyouita.

Lakini pia nikipita kwenye maandiko labda nizungumzie Kwa upande wa Biblia Kuna andiko linazungumza jambo Fulani ni gumu kidgo kulielewa

Muhibiri 9:11
Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.

Huyu anayeongea hapa ni Suleiman ambaye alikuwa tajiri mkubwa sana lakini pia ni mtu wa hekima sana.
Sasa jambo ambalo ameongea hapo ambalo naona ni kama code Fulani imefichwa,

Yaani aliwaza nini hadi kusema bahati ni muhimu katika mafanikio ya mtu.

Kumbe unaweza ukapambana sana kwenye Maisha na usifanikiwe ila kwenye Maisha pia Kuna swala Zima la bahati linaweza likamfanikisha mtu.

Na ni kweli Kuna watu wanapambana sana kwenye utafutaji ila matokeo ni madogo sana halafu Kuna watu ni kama wakigusa button kidgo mambo yao yanatiki na huyu mwandishi anasema bahati humkuta Kila mtu,

Ikumbukwe huu mchezo ni bahati nasibu. Na kiukwel sio tu huu mchezo ndio bahati nasibu ila ukikaa na kufikir Kwa akili vizr utagundua Kila jambo linalofanyika duniani ni almost betting kwasababu hakuna unachoweza kufanya ukawa unauhakika wa 100% kwamba hiki lazma kitakuwa hvi

Kuna watu wamesoma coarse Fulani vyuoni wakiwa na matarajio makubwa lakini mwisho wake ni kinyume,

Kuna walioingia kwenye ndoa wakiwa na matarajio makubwa lakini mwisho wake pia ni kinyume

kuna wanaokwenda hospital na magonjwa ambayo wengine wamepona lakini wao hayohayo hawaponi na wanaweza wakafariki kabisa,

kwahyo unaweza ona mambo mengi sana hayo ni mfano tu ni kama kubet tu hayana uhakika sana na ndio maana yamkini hata Atheists wanaona kama kuwepo Kwa Mungu ni kubet pia Kwa upande wao kwasababu hawaamini kama yupo kweli au lah.

Sasa wewe unazungumziaje swala Zima la kubet especially sports betting maana ndio ambayo imekuwa habari ya mjini Leo hii ni Halali au si Halali Kwa misingi ya dini?

Unaruhusiwa pia kutoka nje box View attachment 2838822
Kubet ni kamari,kamari ni Haram, QUR'AN 5:90
 
Sasa wewe unazungumziaje swala Zima la kubet especially sports betting maana ndio ambayo imekuwa habari ya mjini Leo hii ni Halali au si Halali Kwa misingi ya dini?
Kamari ni dhambi, alafu Mungu hataki watu wanaomuabudu waishi maisha ya kubahatisha maana na yeye hafanyi mambo kwa kubahatisha.
 
Kuna afisa ubashiri aliwahi kuleta kifungu cha biblia kinasema tafuteni pesa hata kwa kubashiri.
Kifungu chenyewe nimesahau.
 
Yale yale ya Profit(faida) na Interest (riba). Watakuambia riba ni haramu lakini faida ni halali. Lakini ukifuatilia vizuri utagundua kuna tofauti ndogo sana kati ya riba na faida
Kuna kitu kinaitwa factors of production (Nyenzo za uzalishaji mali). Theory of distribution/Price Indices.

Kila nyezo ya uzalishaji mali ina ujira(reward)wake.

-Labour-(Salary/Wage)
-Land-(Rent)
-Capital-(Interest)
-Entrepreneur-(Profit/Loss)

Sasa kwa mtiririko huo tofauti ya riba na faida tutaibaini kwamba, huyo mjasiliamali(enterpreneur) sio mara zote anapata profit/faida, kuna muda ana incur loss/hasara, lakini kwa anaeweka Capital/mtaji ili apate interest (riba)yeye lazima apate faida yeye hanaga hasara, ila wa profit anaweza pata mara dufu ya kile alichoweka na wa interest yeye iko fixed kwa muda maalumu, kama ni 5000 kwa mwezi au kwa mwaka kiasi ni kilekile hakipungui wala kuzidi(fixed percentage over time).
 
Wanakuuliza juu ya ulevi na kamari. Sema:-

"Katika hivyo mna madhara makubwa na (baadhi ya) manufaakwa (baadhi ya) watu.Lakini madhara yake ni makubwa zaidi kuliko manufaa yake." (Al-Baqarah 2:219)

Hakika Sheitani anataka kukitilieni uadui na bughudha baina yenu kwa ajili ya ulevi na kamari.........."(Al-Maidah, 5:91)

Ni dhahiri kuwa mcheza kamari anayeshindwa na kupoteza fedha zake, huhamaki na kughadhabika kwa kumwona mwenzake akitumbukiza fedha hizo zote mfukoni mwake huku akicheka kwa furaha ya ushindi wake. Hivyo hasira na ghadhabu hizo huja wakati mmoja zikatokeza na kusababisha maafa makubwa.
 
Let
hata nikishusha aya za bibli zinazokataza kamari hutaelewa utabaki kupinga tu
Kama wewe, unavifungu viweke hapa sio lazima mimi ni elewe lakini sababu jamii forum ni platform ambayo ni accessible kwa wengi utafanya wengine waelewe Yale ambayo maandiko yanasema.
 
Kila kitu kwenye maisha ni kubeti,na kubeti sio dhambi.kubeti Ni Kama ofisi zingine unafanya Kazi na unapata mshahara wako,,
Naunga hoja mkuu,
Mkuu ONJO,
kitu chochote kile ambacho unafanya hujui ni kwa namna gani unapata pesa kina implication kubwa sana kwenye maisha yetu haswa sisi Vijana.

Betting ina negative implications kubwa sana, kwanza inaaminisha ubongo kuna njia rahisi ya kupata pesa pasipo kuelewa mchakato mzima wakupata pesa hiyo.

Huwezi fananisha betting na biashara ya kuuza mchele mfano, mfanyabiashara anaenda kujumua mzigo kiroba cha kg100 kwa kiasi fulani then anakuja kuuza kilo1 kwa kiasi fulani at the end unafahamu mchakato mzima wa kuingiza pesa.

Halafu huwezi kusema betting ni sawa na Mshahara, hilo haliwezekani! Una mkataba wa miaka5 kampuni X kila tarehe 23_29 mshahara wako kiasi cha shilingi Milioni1 kinaingia, unaweza kusema kila tarehe hizo nitabet nitaingiza kiasi cha shilingi kadhaa?

Sijaegemea angle ya dhambi, ila kuna vitu vinaharibu sana. Hasa hizi pesa tunazoaminishwa ni za kubahatisha.
 
Kwa kweli hii michezo ya kubeti ni ya kupigwa vita mpaka ipotee, ni uchezeaji wa hela na tamaa ya kupata hela kwa njia ya shot cut. Ni upotevu wa fedha, anayepata ni mwenye kampuni ya kubeti. Wizi mtupu wa kijanja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom