Kubadili majina baada ya kuolewa

Kubadili majina baada ya kuolewa

Ni vizuri lknini,doh hawa wanaume wa siku hizi vigeugeu sana. Yaan unaweza kukaa nae vizuri kwa miaka ya mwanzo ikafika mahali akaanza kukubadilikia mara wanawake mara kipondondo ilimradi amekunyanyasa tuu. Siwaamini sana hawa watu jamani.
 
Mkiachana unabadili na kurejea kwa la baba yako? ukipata bwana mwingine unahamia kwa jina lake??
 
acha wengine wakuite mama Lowasa ama mama Kikwete, ila wewe documents zako zibaki kama Regina xxxxx au Salima xxxxx.

Maana kubadiri jina baada kuolewa hakumanishi kwamba wewe kweli ni Regina Lowasa au Salma Kikwete, ila utabaki kuwa ni Regina xxxx ama Salma xxxx. Piga picha kesho mnaachana (siombei itokee hivyo) - je utapenda uendelee kuitwa nani?

ushauri wangu waache wao wakuite hivyo ila wewe utabaki kuwa Salma xxxx ama Regina xxxxx
 
Uamuzi wa hilo halianzii kichwani mwako wala si swala la mapenzi bali taratibu za tangu kuchmbia mpaka kuolewa.
Kabla hamjapinga au kuunga mkono jiulizeni jambo hiki; Je ni nini maana ya mahari? Athali zake ni zipi? Mkishapata majibu
 
Mwanaume mwenye status nani atakataa kuitwa jina lake? By z way mi sifagilii kuupa umaarufu ukoo wa mwenzio wakwenu udidimie. Unioe alafu uwe baba angu tena na wanetu baba yao atakuwa nanii???
 
I don't like it at all japo nilishafanya hivyo, sidhauri mtu abadili jina,
Kwanza inaleta contradiction kwenye Vyeti, vinasomeka jina jingine kama ni humu makazini unaendelea kuitwa jina jingine,
 
sikuhizi ni wachache sana na mimi natamani niwe miongoni mwa hao wachache

Zamani akina baba walikuwa wameenda shule wakati wakina mama walikua shule ndogo, ndio maana waliona fahari kuitwa mrs fulani, hata familia ya mwanamke walikuwa wanaona fahari mtoto wao kutumia jina mrs fulani tu kwasababu labda mwanaume ana pesa au cheo nk.

Tofauti na siku hzi, wanawake wanaenda shule sambamba na wanaume, kweli mwanaume kanikuta nipo kazini nianze kuangaika kubadili jina, khaa!!! Natafuta tuzo???

Mahaba sio kwenye jina hata.
 
Ni heshima tu lkn kwa kuweka kumbukumbu sawa sishauri kubadili jina unapolewa. Cha msingi hapa ni kuishi vizuri kwa upendo kama wanandoa na kuilea familia ipasavyo.
 
we badili tu haina madhara yoyote kwa maana we si wa wazazi tena bali ni wa mume wako
 
Ni utaratibu tu kama kutoa mahari na muwe kutunza Familia. Ila mwaweza kualikana kama utaona inafafaa wewe ukafanya ya mume na mume afanye yako.
 
Back
Top Bottom