Kuanzishwa kwa Jukwaa la Safari

Kuanzishwa kwa Jukwaa la Safari

Mla Bata

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2013
Posts
8,164
Reaction score
18,676
Wasalam,

Kumekuwa na wimbi kubwa la wadau hapa JF kutaka kujua taarifa mbalimbali za jinsi watakavyoweza kutoka nje ya mipaka ya nchi hii aidha afrika ama nje ya bara hili, Wapo wenye lengo la kutoka kimasomo, kutafuta kazi, kuzamia n.k.

Wadau mbalimbali wamekuwa wakija na nyuzi mbali mbali kwaajili ya kuuliza maswali ama taarifa juu ya fursa mbalimbali zinazopatikana nje ya mipaka hii, Shukrani kwa baadhi ya wadau wenye kujitoa kwa kushare taarifa mbalimbali za jinsi ya kutoka nje ya mipaka ya bongo , baadhi yao ni Jon Stephano lusungo Isanga family Kiranga The Icebreaker na wengineo.

Lengo la uzi huu ni kuwaomba wakuu Maxence Melo Moderator Farida
Kwa mamlaka mliyonayo muweze kutufungulia forum maalumu itakayohusu mambo na taarifa mbali mbali za safari aidha nje ama ndani ya bara hili, mnaweza mkaliita Safari forum, travel forum n.k

Kwa watumiaji wa forum maarufu ya nairaland mtakuwa mashahidi hawa jamaa wapo vizuri sana kwenye hili, wana forum yao ya travel ambayo wamekuwa wakipashana taarifa mbalimbali za huko duniani na jinsi gani ya kufika kwa namna tofauti tofauti, chungulia hapa Nairaland Travel - Nigeria - Nairaland jamaa hawapo nyuma wamekuwa wakichangamkia fursa kibao za kutoka.

Kuwepo kwa forum hiyo kutasaidia kurahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali za jinsi ya kutoka na kupashana habari za fursa huko nje.

Ni imani yangu ombi hili litafanyiwa kazi wakuu.
Natanguliza shukrani zangu.

Wasalam.
 
Jamaa wanafunguka sanaa huku.
20191108_155742.jpeg
Screenshot_20191108-155655.jpeg
 
Shukurani nyingi kwa wazo hili la kupanua wigo wa mawazo kuhusu safari.

Teknolojia hii ya mtandao tunayo, tuifanyie haki kwa kuitumia vizuri.
For sure mkuu, ifikie kipindi tuone watanzania wengi wanatapakaa nchi mbalimbali, wenzetu wanatuzidi sana katika hili.
 
For sure mkuu, ifikie kipindi tuone watanzania wengi wanatapakaa nchi mbalimbali, wenzetu wanatuzidi sana katika hili.
Mimi huku kila ninapoenda mara nyingi sana nikikutana na muafrika ni Mnigeria au Mghana.

Hata nikisema natoka Tanzania, wanauliza, is that near Nigeria?

Tukiwa wengi nje tunaweza kujiunga vizuri zaidi kufanya makubwa mengi.
 
Mimi huku kila ninapoenda mara nyingi sana nikikutana na muafrika ni Mnigeria au Mghana.

Hata nikisema natoka Tanzania, wanauliza, is that near Nigeria?

Tukiwa wengi nje tunaweza kujiunga vizuri zaidi kufanya makubwa mengi.
Aiseee kwamba ni nchi ngeni masikioni mwao???
 
Mimi huku kila ninapoenda mara nyingi sana nikikutana na muafrika ni Mnigeria au Mghana.

Hata nikisema natoka Tanzania, wanauliza, is that near Nigeria?

Tukiwa wengi nje tunaweza kujiunga vizuri zaidi kufanya makubwa mengi.
Remittance zitaongezeka watanzania wakiwa wengi nje ya nchi yao.

Ukiangalia nchi za Asia au Latin America, utaona jinsi kiwango cha fedha wanatuma kwenda kwao.
 
👏👏👏👏👏👏 wazo zuri, hii isiwe kwa safari za nje ya nchi tu, hata ndani ya nchi, kupeana experiences za maeneo mbalimbali katika safari, ratiba. Na maeneo ya hifadhi (guest house/lodge).

Nakumbuka last year nilikuwa naenda somewhere namanyere/kirando nilikuwa hata sijui kirando ndo wapi ila kwa msaada wa mwana JF nilifika fresh, na alinipa ratiba kamili ya magari kutoka sumbawanga hadi kirando na alinielekeza sehem nzuri na salama kwa kulala, kwahiyo nilifika kama mwenyeji sababu nilifika lodge najua hadi majina ya wahudumu
 
Back
Top Bottom