Kuanguka Jengo: Ubora wa Cement Uchunguzwe

Kuanguka Jengo: Ubora wa Cement Uchunguzwe

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2007
Posts
4,189
Reaction score
3,548
Ubora wa Cement iliyptumika kujengea unatia wasi wasi kwa sababu jengo lile lilipukutika zikabakia nondo. Kuna fununu za kiwango hafifu cha ubora wa cement ya RHINO ambayo mwezi February kulitokea hasara kubwa kwa mawakala wa cement baada ya kununua cement isiyo na kiwango cha ubora na bidhaa hiyo haikurudi kiwandani kwa ajili ya marekebisho wala fidia kwa mawakala. Katika eneo la tukio kumekuwepo mifuko ya RHINO CEMENT kuashiria kwamba cement hiyo ilitumika kujengea jengo hilo kabla ya kuanguka kwake. Nadhani kuna haja uchunguzi uanze na ubora wa cement hususani cement ya RHINO CEMENT.
 
Nakubariana na wewe,nimefanikiwa kukiona Kifusi cha hilo jengo ni as if ni mchanga tu na kokoto,Cement kiduchu! Here two things involved
1.Cement ni poor quality
2.Mafundi wamechakachua kiasi cha cement iliyokuwa inahitajika.Beam ya zege aiwezi kupukutika kama ukuta wa nyumba ya udongo
 
Nakubariana na wewe,nimefanikiwa kukiona Kifusi cha hilo jengo ni as if ni mchanga tu na kokoto,Cement kiduchu! Here two things involved
1.Cement ni poor quality
2.Mafundi wamechakachua kiasi cha cement iliyokuwa inahitajika.Beam ya zege aiwezi kupukutika kama ukuta wa nyumba ya udongo

Unajua mimi nliposikia kwamba huko Dar kuna ghorofa limeanguka nlidhani ntashuhudia beam zikiwa zimesimama ?
Lakini nlichoona ni KIFUSI tu !
Daaaaah....Jamaaa wamechakachua sanaa yaaani hata sijui ni ratio gani ya kuchanganya wametumia ?

Issue sio Rhino Cement bali ni Uchakachuaji wa Cement kwenye mchanga ndio issue sanaaa....
 
Mafundi wezi sana wameiba sementi usimuamini fundi hata awe ndugu yako atakuibia tuuuyyy
 
Ubora wa Cement iliyptumika kujengea unatia wasi wasi kwa sababu jengo lile lilipukutika zikabakia nondo. Kuna fununu za kiwango hafifu cha ubora wa cement ya RHINO ambayo mwezi February kulitokea hasara kubwa kwa mawakala wa cement baada ya kununua cement isiyo na kiwango cha ubora na bidhaa hiyo haikurudi kiwandani kwa ajili ya marekebisho wala fidia kwa mawakala. Katika eneo la tukio kumekuwepo mifuko ya RHINO CEMENT kuashiria kwamba cement hiyo ilitumika kujengea jengo hilo kabla ya kuanguka kwake. Nadhani kuna haja uchunguzi uanze na ubora wa cement hususani cement ya RHINO CEMENT.

Nalo ni wazo zuri mkuu, maana hata kama .............. ni kifusi cha mchanga na nondo ndo vinavyoonekana!
 
Ubora wa cement inaweza isiwe sababu ila kuto zingatia vipimo katika uchangaji na vifaa vyenye uwezo mdogo kama nondo inaweza kua sababu
 
Mkuu sidhani kama ubora wa cement ni issue hapa, especially unapotaja tatizo la February ambapo ni juzi tu kwani tumeambiwa na msemaji wa NHC kuwa hili jengo limekuwa likijengwa kwa muda sasa (zaidi ya miaka 5 kama nilimsikia vizuri).

Issue hapa inaweza kuwa ni uchakachuaji wa contractor au hata budget ya client ilikuwa ni ndogo kwa hiyo contractor na mshauri mradi wakaamua kufanya kazi inayoendana na bajeti ya mteja.

Kiukweli hata mimi nilishangaa sana kuona kuwa hakuna hata beam moja iliyosimama.
 
Hapo dawa ni wote wakamatwe, washitakiwe mahakamani, wakati huo pia timu ya wataalamu iundwe ili kujua ukweli wa mkasa mzima.
 
Nakubariana na wewe,nimefanikiwa kukiona Kifusi cha hilo jengo ni as if ni mchanga tu na kokoto,Cement kiduchu! Here two things involved
1.Cement ni poor quality
2.Mafundi wamechakachua kiasi cha cement iliyokuwa inahitajika.Beam ya zege aiwezi kupukutika kama ukuta wa nyumba ya udongo
Uadilifu ni mali adimu sana siku hizi. Uadilifu kwenye kila kitu imekua kazi sana kukutana nao. Nakubaliana na wewe kuna uchakachuaji wa cement na ubora wa cement pia uko chini sana. Kuna majengo nayaona kama yanabend hivi au hiyo nayo ni sawa tu.
 
Nafikiri tukiongelea rhino twende kuweka ndan watu tbs wanaohusika na viwango na baada ya hapo kumbuken kama mmesiki ladha alipewa kibali kkujenga gorofa 10 kajenga 16 nani kampa kibali;kama ajapewa alipoongeza ya 12;13 watu wa manispaa wanapita kila baada uya wikimbili awakuiona so turudi manispaa fukuza wote waliohusika nenda NHC HIV WAHANDISI WA NHC WALIHUSIKA NA WALIKUWEPO KWENYE UJENZI ZILE NONDO AWAKUONA NA KAMA NDIO FLASH WOTE NHC WALIOHIUSIKA ;NENDA BODI YA WAHANDISI WANATEMBELEA KILA SIKU MAJENGO NA KUPEWA POSHO WANAKAA KIMYA AWAKUONA GOROFA ZINAONGEZEKA NAO FLASH
 
Nakubariana na wewe,nimefanikiwa kukiona Kifusi cha hilo jengo ni as if ni mchanga tu na kokoto,Cement kiduchu! Here two things involved
1.Cement ni poor quality
2.Mafundi wamechakachua kiasi cha cement iliyokuwa inahitajika.Beam ya zege aiwezi kupukutika kama ukuta wa nyumba ya udongo

Vyote vyawezekana na uchunguzi utatupa jibu.
1. Kwa mafundi kuiba cement sidhani saana sababu kwa majengo kama hayo wanakuwa makini kidogo si kama nyumba zetu za kawaida za kuishi au ujenzi wa barabara.
2. Ubora wa cement uchunguzwe
3. Mchanga uliotumika pia uchunguzwe
4. Wahandisi!
5. Wenye mamlaka, watoa vibali, wakaguzi!!
 
All in all kwa nchi kama yetu yenye utekelezaji wa sheria regerege mambo kama hayo ni kawaida kutokea.
 
Kwenye UJENZI, ni heri jengo liwe na Nondo(Reinforcement) Kidogo au hafifu ila kuliko zege (Concrete).

Kama umeshaangalia Crushing Test basi unajua ninaongelea nini na kama hujaona, basi angalia video chini.

Nondo zikizidiwa UZITO, basi huanza kuvutika hadi zipite ule uwezo wake wa kuvutika na kurudi kwenye umbo lake la mwanzo. Pia huendelea hadi zinaanza kuvutika kwa urefu wa milimita kadhaa kabla ya kuja kukatika (Young's Modulus of Elasticity - kwenye Hooke's Law).

Ila Zege, Elasticity yake (uwezo wa kuwa kama Spring) ni mdogo sana. Ndiyo maana huwa wanajenga na Nondo ili kuzipa uwezo wa mmoja anaweza kubeba uzito wa kukandamizwa (pressure on Concrete) na mwingine uwezo wa kuvutwa na kuvutika (Steel/Reinforcement tension).

Sasa basi, kama jengo likianza kuzidiwa uzito, ila Zege bado lipo imara, Nondo zitaanza kuvutika na kwenye jengo utaanza kuona MIANYA. Hapo ujuwe ni ONYO kuwa kimbia haraka sana ndani ya jengo hilo. Ila kama Nondo bado zipo IMARA ila Zege (Concrete) imeshaanza kuvutwa na ikazidiwa, uzito, basi linakuwa kama vile limegongwa na Kitu kizito kisicho na ncha kali. Linavunjika na kuanguka papo kwa papo (Crush).

Tafadhali muwe MAKINI sana na zege mnalotumia kwenye majengo yenu na si Nondo unazotumia. Hii pia ni kwa wale wanaosema hawakuona Nondo ila Kifusi. Kama Nondo zingeshindwa kazi, walau unapata taarifa mapema kama jengo lililoanza kupinda au unaona jengo linaanza kupata mipasuko, kimbia.

Kwa kuangalia kuwa jengo lilianguka GHAFLA, basi jibu siku zote ni kuwa CONCRETE (Zege) lilizidiwa uzito na kuvunjika ghafla. Angalia Video hii hapa chini:



Video ya Stress kwenye Steel. kwenye Video, unaona kabisa jinsi katikati panavyoanza kuvutika na mwisho chuma kinakatika. Huko kuvutika kwa chuma, kunaweza kukupa muda wa wewe kukimbia, kabla chuma hakijakatika.



Ila kwa jengo kama hilo, unaweza kukuta hata ndondo pia zilikuwa hazifai. Ila Zege ndiyo lilikuwa halifai zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tume ya uchunguzi wa village motel iliishiawapi
 
Back
Top Bottom