kookolikoo
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 2,800
- 694
Mafundi wezi sana wameiba sementi usimuamini fundi hata awe ndugu yako atakuibia tuuuyyy
fundi anataka usimamiaji wa karibu wa mhandisi. bila hilo kufanyika tegemea maafa kama tulivyoshuhudia.
Mafundi wezi sana wameiba sementi usimuamini fundi hata awe ndugu yako atakuibia tuuuyyy
Sasa wakuu ni cement ipi ambayo ni bora?
Tuache uongo, mbona slab kibao zinaonekana zipo zimeanguka nzima nzima na wala hazijapukutika?ni kifusi cha mchanga na nondo ndo vinavyoonekana!
Ubora wa Cement iliyptumika kujengea unatia wasi wasi kwa sababu jengo lile lilipukutika zikabakia nondo. Kuna fununu za kiwango hafifu cha ubora wa cement ya RHINO ambayo mwezi February kulitokea hasara kubwa kwa mawakala wa cement baada ya kununua cement isiyo na kiwango cha ubora na bidhaa hiyo haikurudi kiwandani kwa ajili ya marekebisho wala fidia kwa mawakala. Katika eneo la tukio kumekuwepo mifuko ya RHINO CEMENT kuashiria kwamba cement hiyo ilitumika kujengea jengo hilo kabla ya kuanguka kwake. Nadhani kuna haja uchunguzi uanze na ubora wa cement hususani cement ya RHINO CEMENT.
Tuache uongo, mbona slab kibao zinaonekana zipo zimeanguka nzima nzima na wala hazijapukutika?
![]()
Yote hii ni Ignorance ya watz na kushabikia uchakachuzi na nahau za tukale wapi ama kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake..tatizo limkute mwenzio bana..likikukuta wewe ndo utajua madhara ya unora hafifu katika viwango..iwe ni madawa,chakula,mafuta,bidhaa za ujenzi,vifaa vya umeme,elimu etcNakubariana na wewe,nimefanikiwa kukiona Kifusi cha hilo jengo ni as if ni mchanga tu na kokoto,Cement kiduchu! Here two things involved
1.Cement ni poor quality
2.Mafundi wamechakachua kiasi cha cement iliyokuwa inahitajika.Beam ya zege aiwezi kupukutika kama ukuta wa nyumba ya udongo
Ubora wa Cement iliyptumika kujengea unatia wasi wasi kwa sababu jengo lile lilipukutika zikabakia nondo. Kuna fununu za kiwango hafifu cha ubora wa cement ya RHINO ambayo mwezi February kulitokea hasara kubwa kwa mawakala wa cement baada ya kununua cement isiyo na kiwango cha ubora na bidhaa hiyo haikurudi kiwandani kwa ajili ya marekebisho wala fidia kwa mawakala. Katika eneo la tukio kumekuwepo mifuko ya RHINO CEMENT kuashiria kwamba cement hiyo ilitumika kujengea jengo hilo kabla ya kuanguka kwake. Nadhani kuna haja uchunguzi uanze na ubora wa cement hususani cement ya RHINO CEMENT.
Salaam!
Wakati mwingine kabla ya kuandika ni vyema kuuliza wataalamu wa sekta husika wakupe walau muhtasari wa hoja husika. Pamoja na kwamba unaona zege kuwa kama mchanga, bado huwezi kusema tatizo ni saruji iliyotumika. Mimi si mtengenezaji wa muuzaji wa saruji, lkn ni mtumiaji wa saruji. Napenda kukuhakikishia kwamba saruji ya RHINO ina ubora unaokubalika.
Kuanguka kwa jengo husika kunaweza kusababishwa na mambo mengi. Haya ni baadhi tu:
1. Poor design
2. Poor specification and selection of materials
3. Poor workmanship, including erratic curing of concrete
4. Poor quality control system
5. Failure by all parties to observe regulations
6. Overloading of the structure
7. Poor supervision of works
Ni vyema wahusika wote, Building team, yaani Client, Architect, Quantity Surveyos, Structural Engineer na Contractor wahojiwe kuhusu kuanguka kwa jengo hilo na kila mmoja aeleze alivyowajibika katika ujenzi wake. Waliotoa vibali pia wanapaswa kuhojiwa na watoe vielelezo vinavyoonesha jinsi walivyofikia uamuzi wa kutoa kibali.
Mwisho: napenda kuweka wazi kwamba, zege linaloonekana dhaifu linaweza kuwa ni kutokana na mshindo wa kuanguka kwa jengo lenyewe. Kama ulifuatilia WTC iliposhambuliwa, jengo lile lilisambaratika kama karatasi wakati lilikuwa jengo la chuma (Steel structure). Kwenye hili hakuna siasa, ni utaalamu unaopaswa kutupatia majibu sahihi. Wanaofanya siasa wakae kando hadi taarifa ya wataalamu itoke. Hakuna haja ya tume, ERB, CRB na AQRB wanao wataalam wa kutosha kufanya kazi hii bila gharama kubwa.