lita 1 kwa km ngapi? yako ya mwaka gani
used bana.....
Habari wanajamii .....nnampango wa kuvuta forester naomba msaada nitumie kampuni gani kuagiza toka japan ambayo iko cheap na haina usumbufu au ujanjaujanja.Pia hizi gari hazna matatizo??? Nsaidien
Kama ndo gari yako ya kwanza nakushauri utafute aina nyingine sababu kubwa ni kwamba wataalam wake ni wachache sana (Dar es Salaam) Arusha wapo, then kuna baadhi nadhani zile za kuanzia 2003/2004 hvi zinazingua sana gia box.Kuna kijana mmoja ndo mtaalam kidogo wa hzo gari, garage yake ipo mwenge pale.
Kwa ushauri zaidi tuwasiliane
ndio mkoko wangu wa kwanza nimeona nichukue subaru than toyota
Unataka mpya au 2nd hand?
Yangu imekaa garage kwa mda haijatoka ikiwa na matatizo ya gia box,niliagiza vifaa adi nairobi lakini bdo hata juzi nimepita garage kwa huyo fundi nimeona ingine hata haijatembea mwenzi bongo lakin gia box ilishaanza kusumbua so kama unaitamani sana Forester basi chukua manual hzo ni bora kuliko Auto.
Unataka mpya au 2nd hand?
pole mkuuSubaru zimemaliza vijana wengi sana hapa Arusha. Hizi gari zinataka mtu aliyetuliza akili, lakini kama ndo gari ya kwanza kuimiliki ni hatari maana uta' tend kupenda kukimbia ili uonekane unaimudu, hapo ndo itakufinya.
Kuna jamaangu juzi alitoka kuinunua showroom Dar, alipofika Usa-River akatupigia washikaji zake kuwa atukute eneo fulani la matumizi, tukakusanyika tumsubiri, HAMAD akiwa kabakiza km 6 kuingia town alianza kuona watu wanaomjua, akaendelea kukanyagia, ghafla mzee ngoma ikamzidi ujanja, iliviringika mara 5 na kumvunjavunja mbavu zote mshikaji, tukapigiwa simu tukabebe mwili na vipande vipande vya mabati ya gari.
Ikawa ndo mwisho wa mshikaji na subaru yake mpya.
Tukakosa kupiga bata siku hiyo, bili ambayo ilikuwa a'settle yeye ikabidi tulipe chap' lakini mbaya zaidi tukamkosa best yetu.
Chezea kabisa Subaru.