ibramy
JF-Expert Member
- Jul 23, 2019
- 642
- 959
Rafiki wa kweli ni mama!! Mpaka mmefikia uko lazima na wewe una mapungufu!!! Ina maana kabla hujaoelwa hukuona hayo unayoadisia? Ni kama una karoho kabaya ivi....!!!!' kwaiyo mama kuja om napo ni shida? Kumpa pesa mama yake nayo ni shida? Wacha jamaa audumie mama yake bana mkuu.... Unataka hela zote uzuiie?Aisee aikwambie mtu kosea kuchagua nguo, utabadilisha, kosea rafiki utawapotezea lakini usikosee mume. Ukikosea mwanaume wa kuolewa nae tu, umekosea kila kitu.
Kikweli wanaume wa siku hizi, hawana uchungu hata kidogo na familia zao.
Utakuta mume ana mke na watoto lakini Bado anaongozwa na maeneno ya ndugu zake na mama yake. Sisemi kuwa Ni vibaya kuisikiliza wazazi wako na dada na Kaka zako la hasha. Unaweza kuwasikiliza lakini maneno ya kuambiwa changanya na ya kwako.
Wewe nii mume sasa na sio mtoto mdogo, unafamilia hao ndio kaka na dada zako wa kwanza, damu yako. Ndio watu wa kwanza unaotakiwa kuwasikiliza.
Unakuta mwanaume anapata mshahara wote anampelekea mama yake, mke akiitaji matumizi anaambiwa akayafutae kwa mama mkwe, hivi kweli jamani?
Wengine wanaleta wazazi, hasa mama zao waje wakae Hapo anapoishi na mke wake. Hivi unadhani Ni ustaarabu kwa mama kusikia mambo yote mnayoyafanya mkiwa chumbani.
Mnakosa hata muda wa faragha kati yenu mwishowe mnajikuta hamna mapenzi Tena kwenye ndoa kwasababu hamuhudumiani.
Na mwanamke hawezi kukuambia usimlete mama yako, kwasababu ataonekana ana roho mbaya. Ila ukweli ndio huo.
Wanaume wengine mkipata pesa kidogo tu mnataka ujionyeshe kwa watu kuwa wewe una mapesa, eti unaweka heshima baa. Embu acheni ujinga mkalee familia zenu. Kama hamuyataki majukumu kwanini mmeingia kwenye ndoa?
Wanaume mjirekebishe jamani, inasikitisha Sana.
Sent using Jamii Forums mobile app