Siri za ndoa: Siri 5 ambazo mke hafai kumwambia mume wake licha ya utamu wa penzi lao

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,328
33,137
Siri 5 ambazo mke hafai kumwambia mume wake licha ya utamu wa penzi lao.jpg

Ndoa ni muhimu, na huwa muhimu kwasababu ni kitu kinachowaunganisha mume na mke na kuanzisha familia, na huleta baraka nyingi kama vile watoto na nyinginezo nyingi.

Hata hivyo siku hizi, ndoa nyingi huishia kuvunjika kutokana na sababu moja au nyingine, hususan kutokana na ugomvi ndani baina ya wanandoa.

Bila shaka haipaswi kuwa siri baina ya wanandoa, lakini kuna baadhi ya vitu ambavyo mwanamke hapaswi kumwambia mume wake, hata kama wanapendana kiasi gani.

Katika jamii nyingi za kiafrika kuna msemo usemao, masikio yasiposikia , moyo hauwezi kukasirika.

Na kama tunataka amani ndani ya familia lazima kutakuwa na matukio magumu , na mwanamke anapaswa kusaidia katika utatuzi wa mambo hayo.
Yafuatayo ni mambo 5 ambayo mwanamke hapaswi kumwambia mume wake:

1. Idadi ya wanaume uliojamiiana nao kabla ya kuoana na mume wako
Hupaswi kumfahamisha mpenzi wako wa kiume au mume wako ni wanaume wangapi ulikutana nao kimwili kabla ya kuishi naye.

Sababu ni kwamba unaweza kufikiri hautamkosea mume wako siku sijazo. Na kama idadi ya wanaume uliyomwambia ni wengi anaweza kufikiri wewe ni kahaba au mzinzi.

Kwahiyo, iwapo atakuuliza ni wanaume wangapi ulishawahi kukutana nao kimwili, unaweza kucheka tu na umwambie: ''Ebu acha, tuanachane na hayo, lakini suala la ni wangapi halihusiani na safari ya mapenzi. ".

2. Kusema siri za mpenzi wako wa kiume au mume wako wakati mmoja
Ukiulizwa maswali kumuhusu mwanaume, mjibu machache.

Usiseme mambo ambayo yanaweza kumfanya mume au mpenzi wako ahisi kwamba sio bora, au ajihisi kuwa mtu mbaya.

Usizungumzie kuhusu -ungependa kuwa na uhusiano na mwanaume tajiri kiasi fulani, mwenye uwezo wa kingono kiasi gani, na ni kwa vipi ungependa ampende mke wake..
3. Usimwambie mume wako kwamba unampenda sana rafiki yako au shemeji yako
Sote tunafahamu kuwa inawezekana kwa rafiki au shemeji kutaka kukuoa.

Lakini, ni hatari kumwambia mume wako kuhusu wazo hili .

Sababu ni kwamba mume wako anaweza kuanza kuwa na mashaka kuhusu tabia zake na vitendo vyako kumuhusu mwanaume huyo, jambo linaloweza kusambaratisha ndoa yako.
4. Usijaribu kumwambia kuwa unamchukia mama yake au familia yake
Hata mama mkwe awe ni mtu mbaya kiasi gani, usimwambie mume wako kuwa unamchukia.

Au unaichukia familia yake. Hata kama umekasirika kiasi gani, usijaribu kusema mambo mabaya kuwahusu, au kumuona mume wako sawa na familia yake.

Kama haupatani na yeyote katika familia ya mume wako, elezea kwa utulivu, ukiwa na matumaini kuwa ataelewa ni kwanini haupatani nao.

Mume wako pia ataweza kukusaidia kutatua tatizo, na pia itazuwia matatizo mengine ambayo yanaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi.

5. Usimtishe mume wako kuwa utakuja kuachana naye
Siku utakapomwambia mume wako kuwa utaachana naye wakati mnazozana, jua ndio mwanzo wa malumbano ndani ya ndoa.

Ndoa itaanza kukumbwa na misukosuko, wasi wasi na kutoaminiana.

Kutishia kutoa talaka katika ndoa inamaanisha kuwa hauna moyo wa imani katika ndoa, na hauoni umuhimu wake.

Isipokuwa kama katika ndoa kuna unyanyasaji au uhalifu mwingine mbaya, ni vyema kujaribu kushirikiana kutatua changamoto zozote mlizonazo. chanzo.. BBC
 
Kwanza Me unaanzaje kuuliza Ke katembea na wangapi kabla yako? It's obvious ni wengi, shukuru Mungu kama hawazidi watano, coz zaidi ya hapo utapata pressure tu.
 
Back
Top Bottom