ShesRise_1
JF-Expert Member
- Aug 21, 2025
- 16,993
- 40,149
Kosa la Mwanamke Anapopenda Ni Nini?
Kuna mtoa mada juzi kasema kwamba dada yake alikuwa in love na mshikaji fulani na mwisho wa siku yule jamaa akamtapeli ikiwemo kadi yake ya bank, na kumuacha akiwa mjamzito
Nikaona baadhi ya comments wakisema kwamba wanawake huwa tunapenda sana bila kuchunguza au kutumia akili
Sasa najiuliza, kosa la huyo dada ni nini hasa?
Kumpenda huyo mwanaume na kumwamini hilo ndiyo kosa?
Kwa nini tusimlaumu kwanza mwanaume kwa kuwa msaliti na tapeli wa mapenzi?
In short ameaminiwa ila amefanya hiyana wakulaumiwa hapa ni huyu binadamu aliekosa utu na kuongozwa na tamaa
Ajabu ni kwamba mwanamke akipenda sana utasikia:
Utasikia 👇
Wanawake wakipenda wanapenda vibaya, hawatumii akili
ooh 👇
Mwanamke akitiwa vizuri hasikii wala haoni
Hapo mwanamke kaonekana amependa vibaya sio kupongezwa kwa kua na upendo usiopimika
Sasa ikitokea mwanamke kaamua kua bandidu
unasikia👇
Wanawake ni majambazi, tusiwaamini, ni watu wabaya, hawana mapenzi..🙄
Na bla bla kibao
Hata hapa jamvini tunaona hizi shutuma
Sasa mimi nashangazwa...
Mwanamke akipenda kwa moyo, akaamini na kujitoa kwa mtu, mwisho wa siku akapigwa matukio na kudhalilishwa, tunaishia kusema:
Alitumia hisia badala ya akili
Na kuacha kulaumu mharibifu
Akiamua kuwa bandidu, kujilinda na kutoweka moyo wake kirahisi, unaambiwa:👇
Huyu sio wife material
Sasa mwanamke afanye nini? 😅
Tukipenda sana, tunatumia akili vibaya
Tukijilinda, hatuna upendo
Tukiamini, tumejitoa bila kuchunguza
Tukikataa kuamini kirahisi, tunaambiwa tuna attitude
Basi kosa la mwanamke linakuwa nini hasa?
Nyinyi wanaume, nawaambieni kitu...
Mwanamke anapojitolea kukupenda kwa moyo bila kuwa na kasumba nyingi, wewe ambaye unapendwa appreciate hiyo nafasi
Usigeuze upendo wa mwenzako kuwa fimbo ya kumchapia
Usitumie udhaifu wa mtu anayekupenda kama silaha dhidi yake
Na kama unaona kwamba upendo unaopewa unakuzidi, au unaona huwezi kuurudisha kwa kiwango anachokupa, ni bora kuwa muwazi kwenye mapenzi kuliko kuendelea kumshikilia mtu huku ukijua humthamini na wala huna haja nae
Mwambie ukweli
Mwambie unachoweza na usichoweza kumpa ajue kabisa ananyoa au anasuka
Na hii hata kwa mwanamke pia ni vivyo hivyo ukiona hujamuelewa mshikaji be open mapema MUDA NI MALI!
Maana wakati mwingine kinachomuumiza mtu si kwamba hapendwi, bali ni kupewa matumaini na mtu ambaye tayari anajua hawezi kumpenda
Na mwisho wa siku, moyo wenye upendo si ule unaopenda tu
Moyo wenye upendo ni ule ambao haumuumizi mwingine kwa makusudi(labda bahati mbaya)
Swali la mjadala 👇
Kosa ni la anaependa sana na kujitolea?
Au kosa ni la anaeumiza mwingine
Kwa kumjeruhi kihisia au hata kiuchumi?
ShesRise_1 ✋️
Kuna mtoa mada juzi kasema kwamba dada yake alikuwa in love na mshikaji fulani na mwisho wa siku yule jamaa akamtapeli ikiwemo kadi yake ya bank, na kumuacha akiwa mjamzito
Nikaona baadhi ya comments wakisema kwamba wanawake huwa tunapenda sana bila kuchunguza au kutumia akili
Sasa najiuliza, kosa la huyo dada ni nini hasa?
Kumpenda huyo mwanaume na kumwamini hilo ndiyo kosa?
Kwa nini tusimlaumu kwanza mwanaume kwa kuwa msaliti na tapeli wa mapenzi?
In short ameaminiwa ila amefanya hiyana wakulaumiwa hapa ni huyu binadamu aliekosa utu na kuongozwa na tamaa
Ajabu ni kwamba mwanamke akipenda sana utasikia:
Utasikia 👇
Wanawake wakipenda wanapenda vibaya, hawatumii akili
ooh 👇
Mwanamke akitiwa vizuri hasikii wala haoni
Hapo mwanamke kaonekana amependa vibaya sio kupongezwa kwa kua na upendo usiopimika
Sasa ikitokea mwanamke kaamua kua bandidu
unasikia👇
Wanawake ni majambazi, tusiwaamini, ni watu wabaya, hawana mapenzi..🙄
Na bla bla kibao
Hata hapa jamvini tunaona hizi shutuma
Sasa mimi nashangazwa...
Mwanamke akipenda kwa moyo, akaamini na kujitoa kwa mtu, mwisho wa siku akapigwa matukio na kudhalilishwa, tunaishia kusema:
Alitumia hisia badala ya akili
Na kuacha kulaumu mharibifu
Akiamua kuwa bandidu, kujilinda na kutoweka moyo wake kirahisi, unaambiwa:👇
Huyu sio wife material
Sasa mwanamke afanye nini? 😅
Tukipenda sana, tunatumia akili vibaya
Tukijilinda, hatuna upendo
Tukiamini, tumejitoa bila kuchunguza
Tukikataa kuamini kirahisi, tunaambiwa tuna attitude
Basi kosa la mwanamke linakuwa nini hasa?
Nyinyi wanaume, nawaambieni kitu...
Mwanamke anapojitolea kukupenda kwa moyo bila kuwa na kasumba nyingi, wewe ambaye unapendwa appreciate hiyo nafasi
Usigeuze upendo wa mwenzako kuwa fimbo ya kumchapia
Usitumie udhaifu wa mtu anayekupenda kama silaha dhidi yake
Na kama unaona kwamba upendo unaopewa unakuzidi, au unaona huwezi kuurudisha kwa kiwango anachokupa, ni bora kuwa muwazi kwenye mapenzi kuliko kuendelea kumshikilia mtu huku ukijua humthamini na wala huna haja nae
Mwambie ukweli
Mwambie unachoweza na usichoweza kumpa ajue kabisa ananyoa au anasuka
Na hii hata kwa mwanamke pia ni vivyo hivyo ukiona hujamuelewa mshikaji be open mapema MUDA NI MALI!
Maana wakati mwingine kinachomuumiza mtu si kwamba hapendwi, bali ni kupewa matumaini na mtu ambaye tayari anajua hawezi kumpenda
Na mwisho wa siku, moyo wenye upendo si ule unaopenda tu
Moyo wenye upendo ni ule ambao haumuumizi mwingine kwa makusudi(labda bahati mbaya)
Swali la mjadala 👇
Kosa ni la anaependa sana na kujitolea?
Au kosa ni la anaeumiza mwingine
Kwa kumjeruhi kihisia au hata kiuchumi?
ShesRise_1 ✋️