Kosa lilikuwa la nani hapa?

Kosa lilikuwa la nani hapa?

kiss ov love

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2025
Posts
9,363
Reaction score
16,092
Siku moja baada ya kutoka kibaruani, kuna mtu aliniita Bar ya hapo jirani na ofisini kwetu nikaenda hapo tukawa tumekaa nikaagiza chakula nikawa nakula, kuna ndugu yangu akaniambia anakuja kwahiyo nikamwambia apitie hapo kama vipi tuondoke wote, sasa mimi nikawa napiga stori na huyo mbaba.

Nikamaliza kula akaniambia niagize kinywaji nikamwambia sijisikii kunywa pombe kwani huwa zinanisumbua naamka kichwa kizito akaniagizia sijui ni Whisky ile inaitwa Black and White sasa mambo hayo mimi sijazoea nilichanganya na soda nikashindwa kuinywa naiona kali ikabidi niagize tu juisi ya matunda.

Sasa yule ndugu yangu akaja ni wakike so tukawa tupo watatu hapo kwenye meza yetu mimi yule mbaba na huyo ndugu yangu, sasa kuna mbaba mwingine alikuwa yupo kwenye process za kunitongoza nilishamwambiaga huyu ndugu yangu alikuwa anamjua, sasa ndugu yangu alivyofika pale akawa ameniambia mbona fulani nimemuona hapo nyuma yetu na yupo na mdada eeeh! Nikashtuka ikabidi nigeuke kuangalia kweli.

Amekaa na msichana mrembo mweupe, nikatoka nikaenda chooni yule mbaba aliyekuwa amekaa na msichana hapo nyuma akanifata eti umekuja kufanyaje mbona hujaniambia kama unakuja na yule umekaa nae nani, heeeh yaani yeye kajisahau kama yupo na mwanamke mwingine pale, nikamwambia meseji zangu huwa hujibu ndiyo maana sijakwambia na yule ni rafiki yetu tunafahamiana naye. Nikamuuliza na yeye yule aliye naye pale ni nani akajifanya hamjui yupo mwenyewe ila wanaume 😁😁🙌

Mimi nikarudi zangu kukaa nilipokaa mwanzo, huyu mbaba akaja pale akajifanya anasalimia akawa kaingiwa na wasiwasi hadi unamuona kabisa akarudi kwenye meza yake akawa hamsogelei kabisa yule msichana sasa sijui alienda wapi huyo msichana akawa anaongea na wahudumu hadi wanacheka wanagonga na mikono mara akarudi akamuitia usafiri yule mdada akaondoka na yeye akaenda nje kuongea na simu, na mimi na ndugu yangu tukaondoka.

Nilichoshukuru Mungu ni kwamba nimemjua mapema kabla sijampa kwahiyo hakuambulia kitu kabisa.

Ikumbukwe yule mbaba ambaye nilikaa nae mwanzo hakuwa mtu wangu alikuwa ananiitaga tu akiwa anataka kampani na unaweza kukaa nae hata akitokea mtu akaja hapo hawezi kujua kama mpo pamoja nilipata taarifa zake baadae kuwa ni mtu wa mademu sana ndiyo maana anafanya hivyo.
 
Siku moja baada ya kutoka kibaruani, kuna mtu aliniita Bar ya hapo jirani na ofisini kwetu nikaenda hapo tukawa tumekaa nikaagiza chakula nikawa nakula, kuna ndugu yangu akaniambia anakuja kwahiyo nikamwambia apitie hapo kama vipi tuondoke wote, sasa mimi nikawa napiga stori na huyo mbaba.

Nikamaliza kula akaniambia niagize kinywaji nikamwambia sijisikii kunywa pombe kwani huwa zinanisumbua naamka kichwa kizito akaniagizia sijui ni Whisky ile inaitwa Black and White sasa mambo hayo mimi sijazoea nilichanganya na soda nikashindwa kuinywa naiona kali ikabidi niagize tu juisi ya matunda.

Sasa yule ndugu yangu akaja ni wakike so tukawa tupo watatu hapo kwenye meza yetu mimi yule mbaba na huyo ndugu yangu, sasa kuna mbaba mwingine alikuwa yupo kwenye process za kunitongoza nilishamwambiaga huyu ndugu yangu alikuwa anamjua, sasa ndugu yangu alivyofika pale akawa ameniambia mbona fulani nimemuona hapo nyuma yetu na yupo na mdada eeeh! Nikashtuka ikabidi nigeuke kuangalia kweli.

Amekaa na msichana mrembo mweupe, nikatoka nikaenda chooni yule mbaba aliyekuwa amekaa na msichana hapo nyuma akanifata eti umekuja kufanyaje mbona hujaniambia kama unakuja na yule umekaa nae nani, heeeh yaani yeye kajisahau kama yupo na mwanamke mwingine pale, nikamwambia meseji zangu huwa hujibu ndiyo maana sijakwambia na yule ni rafiki yetu tunafahamiana naye. Nikamuuliza na yeye yule aliye naye pale ni nani akajifanya hamjui yupo mwenyewe ila wanaume 😁😁🙌

Mimi nikarudi zangu kukaa nilipokaa mwanzo, huyu mbaba akaja pale akajifanya anasalimia akawa kaingiwa na wasiwasi hadi unamuona kabisa akarudi kwenye meza yake akawa hamsogelei kabisa yule msichana sasa sijui alienda wapi huyo msichana akawa anaongea na wahudumu hadi wanacheka wanagonga na mikono mara akarudi akamuitia usafiri yule mdada akaondoka na yeye akaenda nje kuongea na simu, na mimi na ndugu yangu tukaondoka.

Nilichoshukuru Mungu ni kwamba nimemjua mapema kabla sijampa kwahiyo hakuambulia kitu kabisa.

Ikumbukwe yule mbaba ambaye nilikaa nae mwanzo hakuwa mtu wangu alikuwa ananiitaga tu akiwa anataka kampani na unaweza kukaa nae hata akitokea mtu akaja hapo hawezi kujua kama mpo pamoja nilipata taarifa zake baadae kuwa ni mtu wa mademu sana ndiyo maana anafanya hivyo.
Kwahiyo ulimuonea wivu kabla hujamkubalia?
 
Back
Top Bottom