KOROSHO NGOMA NZITO: Wakulima Watinga ofisini kwa Mkuu wa Wilaya kudai malipo yao

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
BAADHI ya wakulima wa korosho, makatibu na wenyeviti wa vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) wilayani Masasi mkoani Mtwara, jana walikusanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Selemani Mzee na kupiga kambi nje ya ofisi hiyo kwa zaidi ya saa saba wakishinikiza serikali kulipa fedha za korosho.

Walichukua hatua hiyo kutokana na serikali kutowalipa fedha za korosho, huku baadhi yao wakidai kuwa walipewa ahadi ya kufanyika ukaguzi wa mashamba yao baada ya kubainika korosho walizouza ni zaidi ya kilo 1,500.

Taratibu za malipo kwa walikuma wa zao hilo zinataka mkulima yeyote mwenye kilo zaidi ya 1,500 lazima akaguliwe shamba lake kabla ya malipo kufanyika.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Wilaya hiyo, (Mzee) aliamua kufanya kikao maalum cha dharura na wakulima hao akiwa na wajumbe wengine wa Kamati yake ya Ulinzi na Usalama na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Masasi, Eduward Mmavele, ili kwa pamoja kusikiliza malalamiko ya wakulima hao.

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya Mkuu wa Wilaya, mmoja wa wakulima hao ambaye ameuza korosho zake kwenye Chama cha Msingi Tuaminiane (AMCOS), Saidi Khatau, alisema ni miongoni mwa wakulima wanaotakiwa kufanyiwa ukaguzi wa mashamba yao. Alisema wanashangaa kuona ahadi ya serikali ya kukagua mashamba yao haitekelezwi licha ya kuuza korosho.

Alisema wakulima hawajui ni lini serikali itawalipa fedha zao na hawafahamu lini jopo linalofanya ukaguzi wa mashamba ya wakulima litafika shambani kwake, ili aingizwe kwenye orodha ya majina ya wakulima ambao watalipwa fedha zao.

“Ukaguzi wa mashamba ya wakulima tunashindwa kuuelewa kwanini umekuwa ukifanywa kwa kusuasua, tukiuliza tunajibiwa eti magari hayana mafuta, mimi niko tayari kutoa mafuta na gari langu litumike kufanya ukaguzi kwenye shamba langu na kwa sababu korosho kwangu ndiyo msingi wa kuendesha maisha na sasa sina hela, nategemea fedha hizi za korosho ili hata watoto wangu niwaandae kwenda shuleni," alisema Khatau.

Mkulima mwingine wa korosho, Jacob Hokororo, alidai kuuza kilo 1,563 za korosho kwa chama cha Tuaminiane, alidai kuna kundi kubwa la wakulima hajalipwa fedha za mauzo ya zao hilo.

Alisema haoni haja kwa sasa serikali kutumia muda mwingi kukagua mashamba ya korosho kwa kuwa zipo takwimu za miaka ya nyuma kuhusu ukaguzi wa mashamba hayo. Everina Kambulage, mkulima aliyeuza kilo 470 za korosho, alisema kiwango alichouza hakihitaji ukaguzi wa shamba lake, lakini hajalipwa hata senti moja.

Alisema anaiomba serikali kuharakisha mchakato wa wakulima, hasa wenye kiwango kidogo cha korosho, kulipwa fedha zao.

Alisema hali ya wakulima ambao hadi sasa hawajalipwa fedha zao ni mbaya, akidai wanashindwa kuendesha maisha yao kutokana na kukosa fedha.

Kiongozi wa Chama cha Msingi Lulindi AMCOS, Shiraji Athuman, alisema wamepata faraja kukutana na Mkuu wa Wilaya kwa kuwa chama chao ni miongoni mwa vyama ambavyo wakulima bado hawajalipwa fedha zao na hawajaelezwa sababu za kutofanyika kwa malipo hayo.

“Sisi viongozi wa AMCOS kwa sasa tunashindwa kuishi vizuri na familia zetu huko vijijini kwa sababu ya wakulima kutolipwa fedha zao, wanahitaji kufahamu kwanini serikali bado haijawalipa fedha zao hadi sasa na kila siku wanasikia serikali ikisema wakulima wamelipwa. Kwa kweli usalama wa maisha yetu ni mdogo, tunaomba kulipwa," alisema.

Akijibu maombi yao, Mkuu wa Wilaya ya Masasi (Mzee) alisema amesikiliza kwa umakini malalamiko ya wakulima na akasisitiza serikali bado inaendelea kuwalipa wakulima, hivyo kuwataka wawe wavumilivu.

“Nawaomba muwe wavumilivu kwa kuwa kila mkulima ambaye ni mkulima halali, lazima atalipwa fedha zake," alisema.

"Kuhusu suala la ukaguzi wa mashamba, hili nitakaa na wahusika kujua tatizo liko wapi, lakini ni lazima serikali inawalipa wakulima kupitia taratibu zake ambazo zinalenga kuhakikisha anayelipwa ni mkulima halali."

Watinga ofisini kwa DC kudai malipo ya korosho
 
tapatalk_jpeg_1542131910472.jpeg
 
Tulisema mwanzo kuwa serikali ilikurupuka kuvamia ununuzi wa zao la korosho lkn wakereketwa wa ccm wakatuona sisi ni wapinzani wa ccm sasa hivi ona sasa wamekwama
BAADHI ya wakulima wa korosho, makatibu na wenyeviti wa vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) wilayani Masasi mkoani Mtwara, jana walikusanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Selemani Mzee na kupiga kambi nje ya ofisi hiyo kwa zaidi ya saa saba wakishinikiza serikali kulipa fedha za korosho.

Walichukua hatua hiyo kutokana na serikali kutowalipa fedha za korosho, huku baadhi yao wakidai kuwa walipewa ahadi ya kufanyika ukaguzi wa mashamba yao baada ya kubainika korosho walizouza ni zaidi ya kilo 1,500.

Taratibu za malipo kwa walikuma wa zao hilo zinataka mkulima yeyote mwenye kilo zaidi ya 1,500 lazima akaguliwe shamba lake kabla ya malipo kufanyika.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Wilaya hiyo, (Mzee) aliamua kufanya kikao maalum cha dharura na wakulima hao akiwa na wajumbe wengine wa Kamati yake ya Ulinzi na Usalama na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Masasi, Eduward Mmavele, ili kwa pamoja kusikiliza malalamiko ya wakulima hao.

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya Mkuu wa Wilaya, mmoja wa wakulima hao ambaye ameuza korosho zake kwenye Chama cha Msingi Tuaminiane (AMCOS), Saidi Khatau, alisema ni miongoni mwa wakulima wanaotakiwa kufanyiwa ukaguzi wa mashamba yao. Alisema wanashangaa kuona ahadi ya serikali ya kukagua mashamba yao haitekelezwi licha ya kuuza korosho.

Alisema wakulima hawajui ni lini serikali itawalipa fedha zao na hawafahamu lini jopo linalofanya ukaguzi wa mashamba ya wakulima litafika shambani kwake, ili aingizwe kwenye orodha ya majina ya wakulima ambao watalipwa fedha zao.

“Ukaguzi wa mashamba ya wakulima tunashindwa kuuelewa kwanini umekuwa ukifanywa kwa kusuasua, tukiuliza tunajibiwa eti magari hayana mafuta, mimi niko tayari kutoa mafuta na gari langu litumike kufanya ukaguzi kwenye shamba langu na kwa sababu korosho kwangu ndiyo msingi wa kuendesha maisha na sasa sina hela, nategemea fedha hizi za korosho ili hata watoto wangu niwaandae kwenda shuleni," alisema Khatau.

Mkulima mwingine wa korosho, Jacob Hokororo, alidai kuuza kilo 1,563 za korosho kwa chama cha Tuaminiane, alidai kuna kundi kubwa la wakulima hajalipwa fedha za mauzo ya zao hilo.

Alisema haoni haja kwa sasa serikali kutumia muda mwingi kukagua mashamba ya korosho kwa kuwa zipo takwimu za miaka ya nyuma kuhusu ukaguzi wa mashamba hayo. Everina Kambulage, mkulima aliyeuza kilo 470 za korosho, alisema kiwango alichouza hakihitaji ukaguzi wa shamba lake, lakini hajalipwa hata senti moja.

Alisema anaiomba serikali kuharakisha mchakato wa wakulima, hasa wenye kiwango kidogo cha korosho, kulipwa fedha zao.

Alisema hali ya wakulima ambao hadi sasa hawajalipwa fedha zao ni mbaya, akidai wanashindwa kuendesha maisha yao kutokana na kukosa fedha.

Kiongozi wa Chama cha Msingi Lulindi AMCOS, Shiraji Athuman, alisema wamepata faraja kukutana na Mkuu wa Wilaya kwa kuwa chama chao ni miongoni mwa vyama ambavyo wakulima bado hawajalipwa fedha zao na hawajaelezwa sababu za kutofanyika kwa malipo hayo.

“Sisi viongozi wa AMCOS kwa sasa tunashindwa kuishi vizuri na familia zetu huko vijijini kwa sababu ya wakulima kutolipwa fedha zao, wanahitaji kufahamu kwanini serikali bado haijawalipa fedha zao hadi sasa na kila siku wanasikia serikali ikisema wakulima wamelipwa. Kwa kweli usalama wa maisha yetu ni mdogo, tunaomba kulipwa," alisema.

Akijibu maombi yao, Mkuu wa Wilaya ya Masasi (Mzee) alisema amesikiliza kwa umakini malalamiko ya wakulima na akasisitiza serikali bado inaendelea kuwalipa wakulima, hivyo kuwataka wawe wavumilivu.

“Nawaomba muwe wavumilivu kwa kuwa kila mkulima ambaye ni mkulima halali, lazima atalipwa fedha zake," alisema.

"Kuhusu suala la ukaguzi wa mashamba, hili nitakaa na wahusika kujua tatizo liko wapi, lakini ni lazima serikali inawalipa wakulima kupitia taratibu zake ambazo zinalenga kuhakikisha anayelipwa ni mkulima halali."

Watinga ofisini kwa DC kudai malipo ya korosho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama alivyojigamba kuhamia Dodoma ndani ya 2018 lakini kashindwa, ndivyo alivyojigamba kununua korosho zote na hatimaye anaelekea kashindwa. SGR na Stigler's Gorge HEP generation, bomba la mafuta kutoka Uganda ni miradi inayohitaji dua na maombi
 
BAADHI ya wakulima wa korosho, makatibu na wenyeviti wa vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) wilayani Masasi mkoani Mtwara, jana walikusanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Selemani Mzee na kupiga kambi nje ya ofisi hiyo kwa zaidi ya saa saba wakishinikiza serikali kulipa fedha za korosho.

Walichukua hatua hiyo kutokana na serikali kutowalipa fedha za korosho, huku baadhi yao wakidai kuwa walipewa ahadi ya kufanyika ukaguzi wa mashamba yao baada ya kubainika korosho walizouza ni zaidi ya kilo 1,500.

Taratibu za malipo kwa walikuma wa zao hilo zinataka mkulima yeyote mwenye kilo zaidi ya 1,500 lazima akaguliwe shamba lake kabla ya malipo kufanyika.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Wilaya hiyo, (Mzee) aliamua kufanya kikao maalum cha dharura na wakulima hao akiwa na wajumbe wengine wa Kamati yake ya Ulinzi na Usalama na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Masasi, Eduward Mmavele, ili kwa pamoja kusikiliza malalamiko ya wakulima hao.

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya Mkuu wa Wilaya, mmoja wa wakulima hao ambaye ameuza korosho zake kwenye Chama cha Msingi Tuaminiane (AMCOS), Saidi Khatau, alisema ni miongoni mwa wakulima wanaotakiwa kufanyiwa ukaguzi wa mashamba yao. Alisema wanashangaa kuona ahadi ya serikali ya kukagua mashamba yao haitekelezwi licha ya kuuza korosho.

Alisema wakulima hawajui ni lini serikali itawalipa fedha zao na hawafahamu lini jopo linalofanya ukaguzi wa mashamba ya wakulima litafika shambani kwake, ili aingizwe kwenye orodha ya majina ya wakulima ambao watalipwa fedha zao.

“Ukaguzi wa mashamba ya wakulima tunashindwa kuuelewa kwanini umekuwa ukifanywa kwa kusuasua, tukiuliza tunajibiwa eti magari hayana mafuta, mimi niko tayari kutoa mafuta na gari langu litumike kufanya ukaguzi kwenye shamba langu na kwa sababu korosho kwangu ndiyo msingi wa kuendesha maisha na sasa sina hela, nategemea fedha hizi za korosho ili hata watoto wangu niwaandae kwenda shuleni," alisema Khatau.

Mkulima mwingine wa korosho, Jacob Hokororo, alidai kuuza kilo 1,563 za korosho kwa chama cha Tuaminiane, alidai kuna kundi kubwa la wakulima hajalipwa fedha za mauzo ya zao hilo.

Alisema haoni haja kwa sasa serikali kutumia muda mwingi kukagua mashamba ya korosho kwa kuwa zipo takwimu za miaka ya nyuma kuhusu ukaguzi wa mashamba hayo. Everina Kambulage, mkulima aliyeuza kilo 470 za korosho, alisema kiwango alichouza hakihitaji ukaguzi wa shamba lake, lakini hajalipwa hata senti moja.

Alisema anaiomba serikali kuharakisha mchakato wa wakulima, hasa wenye kiwango kidogo cha korosho, kulipwa fedha zao.

Alisema hali ya wakulima ambao hadi sasa hawajalipwa fedha zao ni mbaya, akidai wanashindwa kuendesha maisha yao kutokana na kukosa fedha.

Kiongozi wa Chama cha Msingi Lulindi AMCOS, Shiraji Athuman, alisema wamepata faraja kukutana na Mkuu wa Wilaya kwa kuwa chama chao ni miongoni mwa vyama ambavyo wakulima bado hawajalipwa fedha zao na hawajaelezwa sababu za kutofanyika kwa malipo hayo.

“Sisi viongozi wa AMCOS kwa sasa tunashindwa kuishi vizuri na familia zetu huko vijijini kwa sababu ya wakulima kutolipwa fedha zao, wanahitaji kufahamu kwanini serikali bado haijawalipa fedha zao hadi sasa na kila siku wanasikia serikali ikisema wakulima wamelipwa. Kwa kweli usalama wa maisha yetu ni mdogo, tunaomba kulipwa," alisema.

Akijibu maombi yao, Mkuu wa Wilaya ya Masasi (Mzee) alisema amesikiliza kwa umakini malalamiko ya wakulima na akasisitiza serikali bado inaendelea kuwalipa wakulima, hivyo kuwataka wawe wavumilivu.

“Nawaomba muwe wavumilivu kwa kuwa kila mkulima ambaye ni mkulima halali, lazima atalipwa fedha zake," alisema.

"Kuhusu suala la ukaguzi wa mashamba, hili nitakaa na wahusika kujua tatizo liko wapi, lakini ni lazima serikali inawalipa wakulima kupitia taratibu zake ambazo zinalenga kuhakikisha anayelipwa ni mkulima halali."

Watinga ofisini kwa DC kudai malipo ya korosho
NI KIONGOZI WA PILI KWA UBORA AFRIKA!
 
Back
Top Bottom