kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 11,185
- 24,564
Korea Kaskazini yafanyia majaribio silaha mpya na ya kisasa chini ya usimamizi wa Kim Jong-un
Serikali ya Korea Kaskazini imefanyia majaribio kwa mafanikio, ya silaha ya 'kistratijia, mpya na ya kisasa' chini ya usimamizi wa kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong-un.
Shirika la Habari la Korea Kaskazini imetangaza kwamba, majaribio hayo yaliyofanyika asubuhi ya leo, yanaifanya silaha hiyo mpya iiongezee uwezo mkubwa wa kijeshi nchi hiyo. Hata hivyo taarifa hiyo hakusema muda wala aina ya silaha iliyofanyiwa majaribio hayo. Hii ni katika hali ambayo Shirika la Habari la Korea Kusini Yonhap limetangaza kwamba hadi sasa halijapata dondoo zozote kuhusiana na majaribio hayo. Majaribio hayo yamefanyika katika hali ambayo tarehe 12 Juni mwaka huu, rais wa Marekani, Donald Trump na Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini walikutana nchini Singapore na kutiliana saini makubaliano kadhaa ambapo kwa mujibu wake, Pyongyang ilikubali kuangamiza kikamilifu silaha zake za nyuklia.
Hata hivyo serikali ya Korea Kaskazini imekuwa ikiilalamikia Marekani kwa kukiuka makubaliano hayo, sambamba na Washington kuendelea kufanya maneva mbalimbali ya kijeshi katika eneo, suala ambalo limekuwa likipingwa vikali na Pyongyang. Kabla ya hapo vyombo vya habari nchini Marekani viliripoti kwamba sambamba na kufanyika mazungumzo kati ya viongozi wa Marekani na Korea Kaskazini katika miezi iliyopita, serikali ya Pyongyang imekuwa ikiendelea kuunda makombora ya mabara kwa kutumia fueli mpya ya majimaji katika viunga vya mji mkuu wa nchi hiyo.
Serikali ya Korea Kaskazini imefanyia majaribio kwa mafanikio, ya silaha ya 'kistratijia, mpya na ya kisasa' chini ya usimamizi wa kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong-un.
Shirika la Habari la Korea Kaskazini imetangaza kwamba, majaribio hayo yaliyofanyika asubuhi ya leo, yanaifanya silaha hiyo mpya iiongezee uwezo mkubwa wa kijeshi nchi hiyo. Hata hivyo taarifa hiyo hakusema muda wala aina ya silaha iliyofanyiwa majaribio hayo. Hii ni katika hali ambayo Shirika la Habari la Korea Kusini Yonhap limetangaza kwamba hadi sasa halijapata dondoo zozote kuhusiana na majaribio hayo. Majaribio hayo yamefanyika katika hali ambayo tarehe 12 Juni mwaka huu, rais wa Marekani, Donald Trump na Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini walikutana nchini Singapore na kutiliana saini makubaliano kadhaa ambapo kwa mujibu wake, Pyongyang ilikubali kuangamiza kikamilifu silaha zake za nyuklia.
Hata hivyo serikali ya Korea Kaskazini imekuwa ikiilalamikia Marekani kwa kukiuka makubaliano hayo, sambamba na Washington kuendelea kufanya maneva mbalimbali ya kijeshi katika eneo, suala ambalo limekuwa likipingwa vikali na Pyongyang. Kabla ya hapo vyombo vya habari nchini Marekani viliripoti kwamba sambamba na kufanyika mazungumzo kati ya viongozi wa Marekani na Korea Kaskazini katika miezi iliyopita, serikali ya Pyongyang imekuwa ikiendelea kuunda makombora ya mabara kwa kutumia fueli mpya ya majimaji katika viunga vya mji mkuu wa nchi hiyo.