Kongamano: Mwanza ya kijani

Kongamano: Mwanza ya kijani

Joined
Sep 14, 2011
Posts
8
Reaction score
45
Hakika Mkoa wa Mwanza umejihakikishia kushinda uchaguzi wa serikali za Mtaa pamoja na uchaguzi Mkuu 2020. Hii ni kutokana Na Hamasa iliyojengeka kwa vijana kwa kukubali Mambo mazuri yanayofanywa na Rais John Magufuli.

Hakika CCM Mwanza USHINDI NI SAA MBILI ASUBUHI.

HONGERA VIONGOZI WA UVCCM KITAIFA, KIMKOA NA VIONGOZI WENGINE WOTE.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
IMG-20190526-WA0001.jpeg
IMG-20190525-WA0086.jpeg
IMG-20190525-WA0078.jpeg
IMG-20190525-WA0077.jpeg
IMG-20190525-WA0079.jpeg
IMG_20190525_132810.jpeg
 
Fikra potofu zinakwamisha maendeleo ya vijana wengi sasa ccm ikishinda Sisi inatusaidia nini?

Au ulikuwa unanifunza kupost thread hapa jukwaani
Siyo lazima ikusaidie wewe Chadema inawasaidia CCM. Pita kimya kimya mkuu!!
 
Jinga sana! Kwahiyo vijana wa Mwanza ni wachache namna hiyo? Unafahamu nyomi la vijana lililopo kitaa? Kwa taarifa yako ccm haipendeki hadi chato vijijini, tena hadi kwa wazee kabisa! Fanya upelelezi utapata majibu
Wewe endelea kujipa moyo!
 
Siyo lazima ikusaidie wewe Chadema inawasaidia CCM. Pita kimya kimya mkuu!!

Mtizamo wa kila mtu hauhitaji kubezwa,ni mtizamo tu kuwa CCM Mwanza itashinda saa mbili asubuhi

Nisaidie ni kwa lipi litakalofanya ishinde asubuhi?

Tuko Mwanza mjini jimbo la Ilemela just few kms from lake victoria....Nyasaka tuna zaidi ya miezi sita hata tone la maji hatuna! Hayo ndo maendekeo unayoyaongea?

Jimbo la Nyamagana, Nyegezi majengo anakoishi mbunge mwenyewe maji ni shiiiidaaa kila leo mnakuja na song lilelile kuwa kuna mradi kabambe utamaliza tatizo la maji jiji la Mwanza...Are we crazy?

Kampeni unaruhusiwa endelea kufanya lakini mnafeli sana tu. Huwezi kutuambia maji yamekuwa kidogo sababu ya ongezeko la watu.....hivi serikali haina master plan?

Mkitaka kujipima kama mnakubalika unavyodai,wekeni tume huru na muachane na polisi halafu muone muziki ulivyo mnene!
 
Mtu anapost na picha yake kabisa eti sijui kijani!!

Kijani wakati vijana tunapauka mitaani!

Kilimo kinatufia mkononi na biashara zinakufa kila kukicha ajira nazo ndo usiseme!!
 
Kumbe ndio maana umeshauri Lissu asigombee,! Kumbe!!
 
Taja mambo matano yaliyofanywa na utawala huu yaliyomnufaisha mwananchi wa kawaia
Kwa kuwa wewe ni kipofu na kiziwi huwezi kuona wala kusikia .Hivyo hata ubiwe vp huwezi sikia wala kuona.

Maendeleo yapo mengi sana
 
Back
Top Bottom