Kombe la Dunia na maigizo

vibertz

JF-Expert Member
Mar 15, 2022
1,373
2,513
Ni kama vile timu kubwa zinawekewa vipaumbele kwa kila namna zipate kufuzu hatua zinazofuata. Mechi ya Senegal dhidi ya Uingereza, kabla hata Uingereza kupata goli kulikuwa na tukio la wazi la mchezaji wa Senegal kuchezewa foul ndani ya 18 lakini mwamuzi na watu wa V.A.R wakamezea. Jana pia waamuzi wakaiharibu mechi ya Brazil dhidi ya Korea kusini kwa kutoa penati ya uonevu kabisa.

Korea wana roho ngumu sana ya kupambana, pamoja na kufungwa lile goli moja ni wazi kabisa lilionekana kuwa uwezo wa kuchomoa na kufanya comeback. Hivyo Brazil, wakabidi wabebwe ili kuidhoofisha kabisa Korea.

Ile haikuwa penati kabisa kwasababu mchezaji wa Korea ndiye aliyekuwa anaumiliki mpira kisha lengo lake ilikuwa kuubutua mpira lakini mchezaji wa Brazil kamtokea kwa nyuma. Jambo ambalo mchezaji wa Korea hakumuona.

Korea hao hao walichezewa faulo ndani ya 18 kwa kuzibiwa njia lakini hakuna cha V.A.R kucheck wala nini. Wanatuharibia radha ya mchezo japo wao lengo lao lipo kibiashara.
 
Nyie watu bana, katika mechi hakuna uamuzi ambao utaridhiaha kila mtu kwa 100%

Japan ilibebwa kwa kupewa goli lenye utata zaidi World Cup, na kama sio lile goli angetoa suluhu na Spain na Ujerumani ingesonga mbele
Ingekuwa timu ya Afrika ndio imefanyiwa hivyo sipati picha hayo makelele, ingekuwa FIFA inahujumu timu za Afrika

Ronaldo mwenyewe alifunga goli dhidi ya Ghana, goli likakataliwa kisa eti alisukuma, ingekuwa timu Afrika ndio imenyimwa goli kama lile ni mikelele kibao
 
Nyie watu bana, katika mechi hakuna uamuzi ambao utaridhiaha kila mtu kwa 100%

Japan ilibebwa kwa kupewa goli lenye utata zaidi World Cup, na kama sio lile goli angetoa suluhu na Spain na Ujerumani ingesonga mbele
Ingekuwa timu ya Afrika ndio imefanyiwa hivyo sipati picha hayo makelele, ingekuwa FIFA inahujumu timu za Afrika

Ronaldo mwenyewe alifunga goli dhidi ya Ghana, goli likakataliwa kisa eti alisukuma, ingekuwa timu Afrika ndio imenyimwa goli kama lile ni mikelele kibao
Tunazungumzia haki katika mpira na wala sio maamuzi ya kuridhisha kundi fulani. Ikiwa faulo iwe faulo ya kihalali. Jana ile penati ya Brazil hivi umeilewa kweli? Embu tuelezee ni vipi iwe penati

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
 
Baada ya ile penalti niliacha kuangalia hiyo gemu, nikaenda zangu kupiga konyagi
 
Ni kama vile timu kubwa zinawekewa vipaumbele kwa kila namna zipate kufuzu hatua zinazofuata. Mechi ya Senegal dhidi ya Uingereza, kabla hata Uingereza kupata goli kulikuwa na tukio la wazi la mchezaji wa Senegal kuchezewa foul ndani ya 18 lakini mwamuzi na watu wa V.A.R wakamezea. Jana pia waamuzi wakaiharibu mechi ya Brazil dhidi ya Korea kusini kwa kutoa penati ya uonevu kabisa.

Korea wana roho ngumu sana ya kupambana, pamoja na kufungwa lile goli moja ni wazi kabisa lilionekana kuwa uwezo wa kuchomoa na kufanya comeback. Hivyo Brazil, wakabidi wabebwe ili kuidhoofisha kabisa Korea.

Ile haikuwa penati kabisa kwasababu mchezaji wa Korea ndiye aliyekuwa anaumiliki mpira kisha lengo lake ilikuwa kuubutua mpira lakini mchezaji wa Brazil kamtokea kwa nyuma. Jambo ambalo mchezaji wa Korea hakumuona.

Korea hao hao walichezewa faulo ndani ya 18 kwa kuzibiwa njia lakini hakuna cha V.A.R kucheck wala nini. Wanatuharibia radha ya mchezo japo wao lengo lao lipo kibiashara.
Kombe la dunia si mechi za yanga utakuwa hufuatilii vizuri tu

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Penalty ya Jana ilikuwa ya mchongo ya Brazil ,lakin hayo madai yako et timu kubwa zinabebwa ni ya kipumbavu kabisa .....

Huyo Korea ni weak timu tu alizidiwa Sana
 
Back
Top Bottom