Tunaojua Muziki Hasa Ya DRC Ukisema Koffi Olomide Hana Mpinzani TUTAKUCHEKA Na KUKUDHARAU Pia. Ili Ujue Tu Kuwa Huyo Koffi Wako Ni Cha Mtoto Kwa Vichwa Hivi Viwili Ambavyo Ndivyo Vinamsumbua Sasa Na Anaviogopa Pata Kwanza Tu Mchanganuo Huu Ufuatao:
1. Wenge Musica BCBG ( JB Mpiana ) 150 $ ( Ukumbi Ni Zenith )
Wenge Musica Maison Mere ( Werrason ) 100$
Quarter Latin ( Koffi Olomide ) 80$
2. Wenge Musica BCBG ( JB Mpiana ) 120$ ( Ukumbi Ni Bercy )
Wenge Musica Maison Mere ( Werrason ) 90$
Quarter Latin ( Koffi Olomide ) 60$
3. Wenge Musica BCBG ( JB Mpiana ) 130$ ( Ukumbi Ni Olympia )
Wenge Musica Maison Mere ( Werrason ) 110$
Quarter Latin ( Koffi Olomide ) 90$
Sijawaweka Akina Fally Ipupa Na Ferre Gola Kwakuwa Shows Zao Zote Ktk Hizo Kumbi Tajwa Hapo Juu Hazizidi 30$. Kama Wewe Umefanya Mambo Ya Marketing And Promotions Utagundua Kuwa Bei Husika Hupangwa Na UBORA Na UZURI Wa Bendi Na Kama Hiyo Haitoshi ILI Uwe Mwanamuziki Mkubwa DRC Ni Lazima Uthubutu Kupiga Katika Hizo Kumbi Kubwa Tatu Tajwa Hapo Juu. JB Mpiana Na Werrason Kila Wakipiga Shows Zao Hapo Lazima Kuwepo Na NYOMI Kama La Lowassa Ambapo Hupelekea Watu KUFA.
Na Kipi Kinamfanya Koffi Afunikwe Na Hao Ni Kwamba Koffi Ni Mzuri Ktk Utungaji Tu Na Miziki Ya KUREKODI Ila Hao WANAMUME Wawili Ndiyo MABINGWA WALIOTUKUKA Wa " Live Shows " Zote DRC Nzima. Fundi Anaonekana Ktk " Live " Na Siyo Ktk Nyimbo Zilizorekodiwa Na Kufanyiwa Editing Za Kutosha.
Kwa Sasa Naomba Nikuache Tu Na Haya Machache ILA Kama Utataka UFAFANUZI Zaidi Karibu.
Kwenye Muziki kitu kimoja wapo kinamfanya mwanamuziki kuwa bora ni consistence, Toka ameanza muziki sifa kubwa ya Koffi ni kumaintain muziki wake kwa kiwango kilekile kwa muda mrefu sana kuliko mwanamuziki yeyote wa Congo
Wenzake wengi sana hivi sasa wamebaki historia lakini Koffi ndio yuleyule
Pili kiingilio pekee sio kigezo cha ubora wa mwanamuziki inategemea kwa wakati huo umetoa wimbo gani na umekubalika vipi unaweza kuweka fees hata ya us 500 lakini consistence ikawa hakuna, yaani mwaka unaofuata unaanza kupiga baa bure
Kumbi nyingi ulizotaja ni za Paris ambapo kimsingi Koffi haendi kwa muda mrefu sasa kwasababu anamatatizo ya kisheria na Ufaransa na ndio maana unaona hao ulio wataja wanakwenda kama kwenda kariakoo
Swala la nani ni mkali wa jukwaani inategemeana na mtazamo na ladha yako mkuu, hao uliowataja ni wataalamu wa fujo ukumbini kwa maana ya kushambulia jukwaa balaa sababu ya aina yao ya muziki na utambulisho wao
Kiffi naye ana aina yake inayopendwa kwa ladha yake na sio lazima iwe kama akima Wenga
Chris brown kujua kucheza sana hakumfanyi kuwa bora sana kuliko wengine ambao si wachezaji sana
Its all about ladha
Indication nyingine kwamba Koffi yupo vizuri ni utajiri alionao, jaribu kugoogle mwanamuziki tajiri Africa mara nyingi sana koffi atakua juu ya wanamuziki wa Congo, ikimaanisha anavuta mkwanja wa kutosha na bado anamiliki band tofauti na akina Fally wanaounga unga wanamuziki
Naamini Koffi hana mpinzani kwa sababu hizo, jembe linajua kumaintain, hakuna mwanamuziki anafanya vema congo kwa muda mrefu kama koffi
Karibu unifafanulie zaidi