Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 286
Kwa muda sasa nimekuwa nikifuatilia suala hili lakini kwa bahati mbaya nimekuwa nikisikia/kusoma habari zinazopingana . Je ni nani aliyefanikiwa kuwapatanisha Rais Mwai Kibaki na mpinzani wake Raila Odinga? Vyombo vingi vya habari vya Tanzania vimekuwa vikiandika/vikitangaza na kumsifu kwamba Rais Kikwete ndio aliyefanikiwa kuwapatanisha Rais Kibaki na Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga mpaka kupelekea kuundwa kwa serikali ya mseto na kumalizika kwa machafuko yaliyotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2008.
Wakati huo huo ukifuatilia vyombo vya habari vya nje/kimataifa kama CNN, BBC, Sky News n.k. vimekuwa vikitangaza kwenye habari zake kwamba mtu aliyewapatanisha Rais Kibaki na Raila Odinga ni Katibu Mkuu wa zamani wa UN Koffi Annan.
Nakumbuka Rais Kikwete ameshatunukiwa Shahada ya Juu ya Uzamivu (PhD) kwa kutambua juhudi zake katika kuwapatanisha viongozi hawa.
Je ukweli ukoje katika suala hili? Nani alifanikisha kuundwa kwa serikali ya mseto? Kama ni Koffi Annan, je degree aliyopewa Mh. Rais ilikuwa ni ya kutambua mchango wake katika jambo gani?
Mbona Rais mstaafu Benjamin Mkapa ambaye naye alishiriki bega kwa bega na Annan hajatunukiwa hiyo shahada?
Naomba mnijuze wanaJF!
Wakati huo huo ukifuatilia vyombo vya habari vya nje/kimataifa kama CNN, BBC, Sky News n.k. vimekuwa vikitangaza kwenye habari zake kwamba mtu aliyewapatanisha Rais Kibaki na Raila Odinga ni Katibu Mkuu wa zamani wa UN Koffi Annan.
Nakumbuka Rais Kikwete ameshatunukiwa Shahada ya Juu ya Uzamivu (PhD) kwa kutambua juhudi zake katika kuwapatanisha viongozi hawa.
Je ukweli ukoje katika suala hili? Nani alifanikisha kuundwa kwa serikali ya mseto? Kama ni Koffi Annan, je degree aliyopewa Mh. Rais ilikuwa ni ya kutambua mchango wake katika jambo gani?
Mbona Rais mstaafu Benjamin Mkapa ambaye naye alishiriki bega kwa bega na Annan hajatunukiwa hiyo shahada?
Naomba mnijuze wanaJF!