dadam
Member
- Apr 20, 2011
- 56
- 9
wapendwa, nimekua nikisoma sana post na coments zenu za humu JF, lakini sijawahi waza kupost Topic au coment kwa sababu ninazozijua...ila leo imenibidi niwashirikishe hili...
Jamani nina furaha.......nilikua na tatizo na mume wangu kwa takribani miaka miwili sasa. kwa kweli ni tatizo ambalo hata kulisema hapa nilishindwa.. nilishaomba ushauri sana hadi kwa wachungaji na kuombewa ila ilishindikana..kiufupi, mume wangu alikua anapenda sana kujifunua na kuacha sehemu zake nyeti wazi kwa kumuonyesha mwanamke...mara nyingine alikua hadi anawachafua watu kwenye daladala na mbegu za kiume. amini usiamini hadi vitoto vidogo vilikua vinakuja kunilalamikia kua mume wangu anawaonyesha dudu lake. ...alishawahi kupigwa kwa kumchafua dada wa watu ktk daladala ila mimi nilikuja kujua baada ya muda mrefu sana.
mwanzoni nilikua nikimuuliza anakataa lakini ilifika siku nikamfumania ndipo alipokubali na kuniambia kua asipofanya hivyo hapati hamu ya kufanya mapenzi na mimi. leo kuna muujiza umetokea kwani sidhani kama ni kawaida
kuna rafiki yangu alinipa namba ya dada mmoja..yaani nikimkumbuka nafurahi hadi machozi yanatoka, huyo dada nahisi alisoma mambo ya saikolojia. tuliongea nae akasema kua angejaribu kuongea na mume wangu. tulifanikiwa kiujanja kumpa namba yake na kumwambia asimwambie kua ni mimi nimempa...
jamani, baada ya siku tano alinambia ameshakutana na mume wangu.
aliongea nae na alikua akinambia tusubiri na niwe namfuatilia kujua maendeleo yake. ninavyoandika sasa, nina miezi miwili sijasikia kesi ya namna ile... cha ajabu leo mume wangu kanitoa lunch..(haijawahi tokea kawa miaka miwili sasa) na kikubwa alitaka kunipongeza na kunishukuru kwa kua mvumilivu kwani sasa tatizo lake limeisha. sikuamini...niliruka hadi nikamwaga soda niliyo kua nakunywa..
leo nimempigia yule dada hapatikani....daaaa natamani nitoboe simu nimpate
natamani ni jue ni dawa gani alimpa ila alinambia hatonambia chochote isipokua kwa ridhaa ya mume wangu. mume wangu nae nahisi kanificha kwani anasema hajatumia dawa yoyote. eti mimi ndo nilikua dawa.
ila ndugu zangu wana Jf....naogopa kumwambia mume wangu kua mimi ndo niliemuunganisha kwa huyo dada kwani atahisi nilikua natangaza tatizo lake. natamani sana kujua ni tatizo gani hasa hili...Mungu ni mwema.....yaani nina raha sijui hata nisemeje,...namshukuru mungu kwa kweli...hakuna lisilowezekana kwa mungu chini ya jua kwani naamini sio akili ya yule dada bali ni mungu tuu looo...dada mwenyewe ni mtoto tuuuu alafu hata hafananii...usimjaji usiyemjua ...
usiku mwema.
Jamani nina furaha.......nilikua na tatizo na mume wangu kwa takribani miaka miwili sasa. kwa kweli ni tatizo ambalo hata kulisema hapa nilishindwa.. nilishaomba ushauri sana hadi kwa wachungaji na kuombewa ila ilishindikana..kiufupi, mume wangu alikua anapenda sana kujifunua na kuacha sehemu zake nyeti wazi kwa kumuonyesha mwanamke...mara nyingine alikua hadi anawachafua watu kwenye daladala na mbegu za kiume. amini usiamini hadi vitoto vidogo vilikua vinakuja kunilalamikia kua mume wangu anawaonyesha dudu lake. ...alishawahi kupigwa kwa kumchafua dada wa watu ktk daladala ila mimi nilikuja kujua baada ya muda mrefu sana.
mwanzoni nilikua nikimuuliza anakataa lakini ilifika siku nikamfumania ndipo alipokubali na kuniambia kua asipofanya hivyo hapati hamu ya kufanya mapenzi na mimi. leo kuna muujiza umetokea kwani sidhani kama ni kawaida
kuna rafiki yangu alinipa namba ya dada mmoja..yaani nikimkumbuka nafurahi hadi machozi yanatoka, huyo dada nahisi alisoma mambo ya saikolojia. tuliongea nae akasema kua angejaribu kuongea na mume wangu. tulifanikiwa kiujanja kumpa namba yake na kumwambia asimwambie kua ni mimi nimempa...
jamani, baada ya siku tano alinambia ameshakutana na mume wangu.
aliongea nae na alikua akinambia tusubiri na niwe namfuatilia kujua maendeleo yake. ninavyoandika sasa, nina miezi miwili sijasikia kesi ya namna ile... cha ajabu leo mume wangu kanitoa lunch..(haijawahi tokea kawa miaka miwili sasa) na kikubwa alitaka kunipongeza na kunishukuru kwa kua mvumilivu kwani sasa tatizo lake limeisha. sikuamini...niliruka hadi nikamwaga soda niliyo kua nakunywa..
leo nimempigia yule dada hapatikani....daaaa natamani nitoboe simu nimpate
natamani ni jue ni dawa gani alimpa ila alinambia hatonambia chochote isipokua kwa ridhaa ya mume wangu. mume wangu nae nahisi kanificha kwani anasema hajatumia dawa yoyote. eti mimi ndo nilikua dawa.
ila ndugu zangu wana Jf....naogopa kumwambia mume wangu kua mimi ndo niliemuunganisha kwa huyo dada kwani atahisi nilikua natangaza tatizo lake. natamani sana kujua ni tatizo gani hasa hili...Mungu ni mwema.....yaani nina raha sijui hata nisemeje,...namshukuru mungu kwa kweli...hakuna lisilowezekana kwa mungu chini ya jua kwani naamini sio akili ya yule dada bali ni mungu tuu looo...dada mwenyewe ni mtoto tuuuu alafu hata hafananii...usimjaji usiyemjua ...
usiku mwema.