Tafakari mifano kadhaa ifuatayo na kisha tujadili nini chanzo cha kuporomoka kiwango cha uaminifu na uadilifu kwenye jamii yetu ya Kitanzania.
1) Umetuma fedha kwa njia ya simu kwa makosa, kwa watu watatu tofauti, halafu wapigie simu na uwajulishe kwamba umewatumia fedha kwenye simu zao kwa makosa, na unawaomba na kuwasihi wakurudishie fedha zako. Unadhani miongoni mwa watu hao watatu, wangapi watakurudishia fedha zako?
2) Kuna gari dogo limepata ajali, likiwa na abiria wanne ndani yake, ambao ni majeruhi wenye hali mbaya sana na hawajiwezi, ndani ya gari hilo kukiwa na mizigo yao, kama mabegi, laptops, simu zao za mkononi na fedha tasilimu. Unadhani wananchi watanzania wakifika eneo la ajali, watafanya nini kwanza? Watawaokoa na kuwawahisha majeruhi hospitali haraka? watawapa huduma ya kwanza? Je unafikiri ile mizigo ya abiria itakuwa salama? Ndiyo au hapana...Kwanini?
3) Mara ngapi, ndugu yako/rafiki yako amekuomba umsaidie kiasi cha fedha kama mkopo na kwamba atazirejesha baada 'wiki moja tu' au 'nikishalipwa tu nitakulipa' lakini wiki na miezi kadhaa itapita na kamwe hatarejesha fedha hizo, na huenda akaanza kukukwepa na hata kukusema vibaya kwa watu wengine, wakati wewe ndiye uliyemsaidia. Shida ni nini hapa?
4) Mara ngapi mtu ameibiwa au amefanyiwa uhalifu na watu wabaya, matapeli, vibaka nk, na akaenda kuripoti polisi kuomba msaada wahusika wachukuliwe hatua na haki yake irejeshwe, lakini badala yake, polisi watamwambia atoe chochote ili wapate 'hela ya mafuta' wawatafute wahalifu hao, na kwakweli hawatafanya lolote kuwatafuta wahalifu hao, akiendelea kufuatilia anaweza kujikuta amegeuziwa kibao yeye.
5) Mara ngapi, umesikia kwamba mtu fulani/ofisa fulani mwenye cheo fulani yenye kiwango fulani cha elimu, wakati si kweli, na hata cheti chake cha shule au chuo kikuu ameghushi. Yaani anafanya kazi kama mtaalamu wa fani fulani lakini kiukweli hana sifa za elimu anayodai anayo. Kwa lugha nyingine kuna Degrees, Masters na hata PHD feki.
6) Mara ngapi umemsikia kiongozi wa shirika/taasisi au Waziri fulani au Mkuu wa mkoa/wilaya fulani akitoa kauli ambao ni dhahiri kabisa inaonekana si ya ukweli? Kauli inayoonesha anawatetea wananchi lakini kiukweli ni uongo na anatetea maslahi yake binafsi au ya watu wake wachache.
7) Mara ngapi umepeleka mzigo wa bidhaa kwa wakala au msambazaji wako, kwamba auze mzigo na kisha achukue 'commission yake', lakini cha ajabu, anauza mzigo wote anakula hela zote, commission yake na hata zile zako zote!, ukimpigia simu hapokei na ujumbe hajibu, ukimfuata anakukimbia!!
Una mifano mingine kama hii? Unafikiri hii inasababishwa na nini hasa? Chanzo ni nini na tufanyeje ili tutoke kwenye hali hii?
Tiririka tafadhali.
1) Umetuma fedha kwa njia ya simu kwa makosa, kwa watu watatu tofauti, halafu wapigie simu na uwajulishe kwamba umewatumia fedha kwenye simu zao kwa makosa, na unawaomba na kuwasihi wakurudishie fedha zako. Unadhani miongoni mwa watu hao watatu, wangapi watakurudishia fedha zako?
2) Kuna gari dogo limepata ajali, likiwa na abiria wanne ndani yake, ambao ni majeruhi wenye hali mbaya sana na hawajiwezi, ndani ya gari hilo kukiwa na mizigo yao, kama mabegi, laptops, simu zao za mkononi na fedha tasilimu. Unadhani wananchi watanzania wakifika eneo la ajali, watafanya nini kwanza? Watawaokoa na kuwawahisha majeruhi hospitali haraka? watawapa huduma ya kwanza? Je unafikiri ile mizigo ya abiria itakuwa salama? Ndiyo au hapana...Kwanini?
3) Mara ngapi, ndugu yako/rafiki yako amekuomba umsaidie kiasi cha fedha kama mkopo na kwamba atazirejesha baada 'wiki moja tu' au 'nikishalipwa tu nitakulipa' lakini wiki na miezi kadhaa itapita na kamwe hatarejesha fedha hizo, na huenda akaanza kukukwepa na hata kukusema vibaya kwa watu wengine, wakati wewe ndiye uliyemsaidia. Shida ni nini hapa?
4) Mara ngapi mtu ameibiwa au amefanyiwa uhalifu na watu wabaya, matapeli, vibaka nk, na akaenda kuripoti polisi kuomba msaada wahusika wachukuliwe hatua na haki yake irejeshwe, lakini badala yake, polisi watamwambia atoe chochote ili wapate 'hela ya mafuta' wawatafute wahalifu hao, na kwakweli hawatafanya lolote kuwatafuta wahalifu hao, akiendelea kufuatilia anaweza kujikuta amegeuziwa kibao yeye.
5) Mara ngapi, umesikia kwamba mtu fulani/ofisa fulani mwenye cheo fulani yenye kiwango fulani cha elimu, wakati si kweli, na hata cheti chake cha shule au chuo kikuu ameghushi. Yaani anafanya kazi kama mtaalamu wa fani fulani lakini kiukweli hana sifa za elimu anayodai anayo. Kwa lugha nyingine kuna Degrees, Masters na hata PHD feki.
6) Mara ngapi umemsikia kiongozi wa shirika/taasisi au Waziri fulani au Mkuu wa mkoa/wilaya fulani akitoa kauli ambao ni dhahiri kabisa inaonekana si ya ukweli? Kauli inayoonesha anawatetea wananchi lakini kiukweli ni uongo na anatetea maslahi yake binafsi au ya watu wake wachache.
7) Mara ngapi umepeleka mzigo wa bidhaa kwa wakala au msambazaji wako, kwamba auze mzigo na kisha achukue 'commission yake', lakini cha ajabu, anauza mzigo wote anakula hela zote, commission yake na hata zile zako zote!, ukimpigia simu hapokei na ujumbe hajibu, ukimfuata anakukimbia!!
Una mifano mingine kama hii? Unafikiri hii inasababishwa na nini hasa? Chanzo ni nini na tufanyeje ili tutoke kwenye hali hii?
Tiririka tafadhali.