Kiwanda cha vitenge kukidhi soko la SADC

Kiwanda cha vitenge kukidhi soko la SADC

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,349
Vitenge ni vazi la Afrika, kutoka Magharibi mpaka Mashariki, Kusini hadi Kaskazini. Ingawa Afrika Kaskazini wana utamaduni wa Asia sana lakini 1/3 ya Afrika tunatumia vitenge kama vazi la kila siku.

Ghana na Nigeria wana viwanda vya kuzalisha vitenge lakini hawajaweza kukidhi soko la Afrika Magharibi tu. Mahitaji makubwa ya vitenge Afrika yanategemea viwanda vya Holland. Mzungu anachuma faida katika bidhaa ambayo yeye wala haitumii.

Mpaka sasa nchi za SADC hazina uzalishaji mkubwa wa hii bidhaa muhimu. Kufaidika kuwa katika umoja huu tungekuwa na kuwanda ambacho kitazalisha vitenge vyenye ubora wa kimataifa kama vile vya Holland na kukata soko la Afrika ya Kusini

Pamba yetu itapata soko na pia ulimaji utaongezeka. Kiwanda kitazalisha ajira kwa vijana. Na warembo wetu wanaweza kuwa mabalozi wa kutangaza bidhaa hii.
 
Hivi kuna viwanda miaka ya nyuma nakumbuka MWATEX, walikuwa wanatengeneza vitenge, sijui vimefia wapi.
Urafiki nacho walikua wanatengeneza khanga nzuri nacho kimejifia.
 
Hivi kuna viwanda miaka ya nyuma nakumbuka MWATEX, walikuwa wanatengeneza vitenge, sijui vimefia wapi.
Urafiki nacho walikua wanatengeneza khanga nzuri nacho kimejifia.
Kulikuwa na vitenge vizuri mno kutoka Mutex, Musoma Textile
 
Kulikuwa na vitenge vizuri mno kutoka Mutex
Ni MUTEX kumbe hadi jina nimesahau, mzee wangu alikua na duka la vitenge na khanga nimeuza sana kipindi hicho khanga za urafiki tunauza rejareja 3500, vitenge vilikuwa 4000 kwa 5000.
 
Ni MUTEX kumbe hadi jina nimesahau, mzee wangu alikua na duka la vitenge na khanga nimeuza sana kipindi hicho khanga za urafiki tunauza rejareja 3500, vitenge vilikuwa 4000 kwa 5000.
Kulikuwa na Mwatex, Mutex, Urafiki na Sungura vyote hivi vilitumia pamba yetu.
 
Kulikuwa na Mwatex, Mutex, Urafiki na Sungura vyote hivi vilitumia pamba yetu.
Kuna pesa nyingi sana kwenye haya mavazi, uhitaji ni mkubwa. kwanza ni vazi rasmi kwa watu wazima wengi. kuna umri ukifika yale magauni mazuri mazuri na sketi havikai tena mwilini inabidi uhamie kwenye vazi la vitenge na khanga.
 
Kuna pesa nyingi sana kwenye haya mavazi, uhitaji ni mkubwa. kwanza ni vazi rasmi kwa watu wazima wengi. kuna umri ukifika yale magauni mazuri mazuri na sketi havikai tena mwilini inabidi uhamie kwenye vazi la vitenge na khanga.
West Africa hata vijana wanavaa vazi hili ni ubunifu tu. kwakweli hii biashara ina faida sana.

Miaka ya 1945 baada ya WWII Mfalme wa Holland alijenga kiwanda cha vitenge ili tu kuzalisha ajira kwa vijana. Soko kubwa likiwa Afrika.
 
West Africa hata vijana wanavaa bazillion hili ni ubunifu tu. kwakweli hii biashara ina faida sana.

Miaka ya 1945 baada ya WWII Mfalme wa Holland aligundua kiwanda cha vitenge ili tu kuzalisha ajira kwa vijana. Soko kubwa likiwa Afrika.
Serikali sikivu chini ya jemedari raisi John Joseph Pombe Magufuli mwana wa Africa chini ya sera yake ya Tanzania ya viwanda imeshasikia ushauri wako, hivyo usiwe na wasiwasi muda sio mrefu na sisi tutakua na kiwanda cha vitenge kitakachokidhi soko la ukanda mzima wa SADC.

Kua mzalendo
Ipende nchi yako
Usiwe kibaraka wa mabeberu
Maendeleo hayana chama

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
 
Back
Top Bottom