Kiwanda cha nyama ya Punda mjini Dodoma

Kiwanda cha nyama ya Punda mjini Dodoma

Wananchi wahamisishwe kufuga punda kwa sababu soko lipo.
 
janga hili bado zito angalia hii video kuhusu punda waliokamatwa Dodoma, ikisemaekana wameibwa Arusha!
 
Hali ya mnyapunda ambae ni maarufu kwa kumsaidia binadamu hasa wafugaji kufanya kazi hasa kubeba mizigo na kilimo iko hatarini kutoweka kutokana na wachina wanaosindika nyama ya punda Dodoma.

Wafugaji kwa sasa wanajikuta katika wakati mgumu kwani punda wao wamekua wakiibiwa kwa kasi kubwa kutokana na uhitaji mkubwa wa nyama hii kiwandani.Lakini pia kuna mashaka makubwa nyama hii tukawa tunauziwa humu nchini wakati sisi kula nyama ya punda sio utamaduni wetu.

Leo kupitia taarifa ya habari ITV limekamatwa Lorry limejaa punda huko Naberera simanjiro inasemekana wanapelekwa kiwandani Dodoma kusindikwa nyama.
Na mimi nilijiuliza hiki kiwanda cha kusindika punda kina ranch?
 
Sasa mnataka mipunda iwe mingi kiasi gani? Acha wachina wasindike. Kama wewe huli wengine wala na pesa inatengenezwa nje nje. Laleni tu
 
Sasa mnataka mipunda iwe mingi kiasi gani? Acha wachina wasindike. Kama wewe huli wengine wala na pesa inatengenezwa nje nje. Laleni tu
Tatizo lako wewe huoni umuhimu wa hawa punda na hata wakiisha wote kwako ni sawa tu.Mimi nimeishi mazingira yakifugaji,unachotakiwa kufahamu idadi ya punda sio kubwa sana.
Na mpaka sasa inaonekana uhitaji wa punda umekua mkubwa kuliko uwepo wake hivyo mpaka sasa punda wameshaanza kutoweka kwa wafugaji.
Lakini unapaswa kufaham punda ni mnyama muhimu sana huko maporini kwa ubebaji wa mizigo na kilimo hivyo kutoweka kwake kunaleta athari kubwa sana.
 
Naangalia Habari ITV naona Kiwanda cha Kuchinja punda Dodoma kilichokuwa kimefungwa sasa kimefunguliwa.

Kilichonishangaza ni malalamiko ya wafanyakazi wanalalamika kuwa idadi waliyoruhusiwa kuchinja kwa siku ni ndogo hivyo iongezwe hadi kufikia punda 60 kwa siku...Najiuliza hao punda wanaochinjwa nyama wanauzia wapi? Au ndo nyama choma tunayokula kwa Mfogo?

IMG_20180415_203701.jpg

 
Jamaa ataenda kufungua kiwanda hicho?, wanapeleka China mkuu.
 
Ni cha wachina, so wanasafirisha kupeleka kwao, Ila na kwa idadi ya maini na utumbo vilivyoko mtaani kuna ulaji mkubwa wa punda bila kujua
 
Ni kama samaki wa Mwanza
Minoko inasafirishwa na huko mtakula mabaki tu ya punda
Mshushie na bia kama wanavyosifia mdudu yule
 
Mkuu kwani mara ya mwisho Mishkaki umekula lini? Nadhani jibu umeshipata hapo
 
Hiyo misoseji mnayokula,Unaacha kula ugali wa dona kwa mkeo baba zima unakula tule tuvidole hapo mnalishwa punda,paka,nyani,chatu,Kobe konokono etc.
 
Back
Top Bottom