Kiwanda cha nyama ya Punda mjini Dodoma

koryo

JF-Expert Member
Jun 21, 2010
639
278
Nimesoma kwenye magazeti na JamiiForums kuhusu kusimamishwa kazi kwa Maafisa wa NEMC kuwa walitumia madaraka yao vibaya kwa kukifungia kiwanda hicho kwa sababu walikuwa na vibali vyote vya kuendesha kiwanda hicho. Napenda kuelemiswa yafuatayo:-
  1. Hivi kweli Tanzania tumefikia hatua ya kufungua kiwanda cha nyama ya punda?
  2. Punda kama mnyama ni msaada mkubwa kwa jamii waishio vijijini, Je kuwa na kiwanda cha nyama ya punda haitapunguza idadi ya punda vijijini na kukinzana na dhana ya punda kuwa msaada mkubwa kule vijijini?.
Mimi binafsi siafiki Wachina kufungua kiwanda cha nyama ya punda nchini kwanza punda ni msaada mkubwa kwa maeneo vijijini na ninaomba sana kwa Serikali ya JPM kukifunga na kufuta kiwanda hicho kabisa..
 
wewe hujui punda nyama yake inaliwa? tena inaliwa ndanindani, watu wamekula mishikaki ya mbwa bila kujua, punda nae ana mishikaki!!
 
Hivi Watanzania tumefikia hatua ya kuwa na mawazo duni kama haya? Kama wewe huli punda shida yako nini? Mbona mabucha na vibanda vya nguruwe viingi wakati wengine hukwazika.
Nadhani ungehoji usalalama wa vyakula na mapodozi mnayoagiza Ulaya kuliko kanyama ketu katamu na ka asili.
 
wewe hujui punda nyama yake inaliwa? tena inaliwa ndanindani, watu wamekula mishikaki ya mbwa bila kujua, punda nae ana mishikaki!!
Mkuu,
Kuna thread zingine zinaletwa jamvini hapa kutafuta la kuzungumzia na kujua mawazo ya watu yako wapi na endapo hoja limetokea msimamo wako mini.
Naomba uniambie ukweli wa habari hizi za kiwanda cha nyama ya punda kilikuwa kimefunguliwa wapi na mmiliki nani Tafadhali.
Tunafahamu Kuwa punda analiwa singida Dodoma na Shinyanga kama sikosei lakini walaji ni wachache sana kufikia hatua ya kujenga kiwanda.
Umetaja wachina au wana mpango wa kusafirisha kwao?
 
Sizani kama kuwa na kiwanda cha kuchakata nyama ya punda ni tatizo kama walifuata taratibu za kufungua biashara hiyo kwani tukijiuliza kama biashara hiyo itafanya punda waishe, kwani hawazaliani?Mi nazani ndo itachochea wakazi wengi kuamasika kuwafuga hivyo kutengeneza ajira. Miaka fulani nilisafiri na gari moshi kufika singida nilikutana na nyama ambayo nazani ilikuwa ya punda lakini nilikula
 
Kama Punda ni mnyama kazi na kuzaliana ni nadra wanaweza kutoweka,basi kwanini tusiwashauri Wachina waanzishe cha nyumbu kwa maana wao Wachina wanakula kila kitu na kwa bahati Nyumbu wanazaliana kwa kasi ya Ajabu!
 
Nimesoma kwenye magazeti na JamiiForums kuhusu kusimamishwa kazi kwa Maafisa wa NEMC kuwa walitumia madaraka yao vibaya kwa kukifungia kiwanda hicho kwa sababu walikuwa na vibali vyote vya kuendesha kiwanda hicho. Napenda kuelemiswa yafuatayo:-
  1. Hivi kweli Tanzania tumefikia hatua ya kufungua kiwanda cha nyama ya punda?.
  2. Punda kama mnyama ni msaada mkubwa kwa jamii waishio vijijini, Je kuwa na kiwanda cha nyama ya punda haitapunguza idadi ya punda vijijini na kukinzana na dhana ya punda kuwa msaada mkubwa kule vijijini?.
Mimi binafsi siafiki Wachina kufungua kiwanda cha nyama ya punda nchini kwanza punda ni msaada mkubwa kwa maeneo vijijini na ninaomba sana kwa Serikali ya JPM kukifunga na kufuta kiwanda hicho kabisa.

taifa kusikiliza mawazo kama haya litapiga hatua kurudi nyuma.

taifa linahitaji watu wa kuwaza maendeleo ya watu na imani au hulka zao kuziweka pembeni.

kama wachina wanakula mbwa na wameona Tanzania wanaweza kupata mbwa kupeleka kwao na watanzania wakapata fedha za kigeni hao tuna wakaribisha bali.

kama wachina kwao punda ni chakula na wanaona hapa kwetu wapo tunawakaribisha watuletee fedha zao tuwape nyama hizo wanazozitaka.

msaada mmojawapo wa punda ni kumpatia fedha aliyemfuga na soko likipatikana basi biashara ya punda itashamiri na watazalishwa wengi kwa maana punda si madini kusema wakichukuliwa wanaisha bali wanaendelea kuzaliana kila siku.
 
Hâta kama kwao ni chakula tatizo ni jinsi walivyokuwa wana waprocess hizi njia zikiachwa hivi zinaweza leta hâta mlipuko wa magonjwa ya kigeni
 
Hali ya mnyapunda ambae ni maarufu kwa kumsaidia binadamu hasa wafugaji kufanya kazi hasa kubeba mizigo na kilimo iko hatarini kutoweka kutokana na wachina wanaosindika nyama ya punda Dodoma.

Wafugaji kwa sasa wanajikuta katika wakati mgumu kwani punda wao wamekua wakiibiwa kwa kasi kubwa kutokana na uhitaji mkubwa wa nyama hii kiwandani.Lakini pia kuna mashaka makubwa nyama hii tukawa tunauziwa humu nchini wakati sisi kula nyama ya punda sio utamaduni wetu.

Leo kupitia taarifa ya habari ITV limekamatwa Lorry limejaa punda huko Naberera simanjiro inasemekana wanapelekwa kiwandani Dodoma kusindikwa nyama.
 
Hv hawa WACHINA si walikamatwa na NEMC tena ilitangazwa kabisa na kiwanda kufungwa cha punda..!! IWEJE HADI LEO BADO WANAENDELEA..? Hv hii nchi kuna nn..? Wachina hawa wataimaliza nchi hii.. Leo nimeona ITV news, PUNDA wengi ktk malori eti wanapelekwa DODOMA..!!

Hawa wachina kwnn serikali inawaacha wanafanya laana hii kubwa ktk nchi yetu..? Wachina ni watu wabaya sana... Wale tu wanaofanya kazi za ujenzi ndio waruhusiwe kuwa nchini... Mtaani na kwingineko hawatakiwi hawa...
 
Hv hawa WACHINA si walikamatwa na NEMC tena ilitangazwa kabisa na kiwanda kufungwa cha punda..!! IWEJE HADI LEO BADO WANAENDELEA..? Hv hii nchi kuna nn..? Wachina hawa wataimaliza nchi hii.. Leo nimeona ITV news, PUNDA wengi ktk malori eti wanapelekwa DODOMA..!!

Hawa wachina kwnn serikali inawaacha wanafanya laana hii kubwa ktk nchi yetu..? Wachina ni watu wabaya sana... Wale tu wanaofanya kazi za ujenzi ndio waruhusiwe kuwa nchini... Mtaani na kwingineko hawatakiwi hawa...
Kama kilifungwa na kama wamekifungua tena serikali ifuatilie nani amewarudishia kibali tena
 
Nasikia hawa hawa wachina kunakiwanda flani pale shinyanga napo wanachinja punda nakufungasha
 
Acheni kula nyama za supermarket aisee hii michina ni km wanyma pori tuu kwa jamii ya kistaarabu ni kz sana kuishi na wavimba macho ustaarabu kwao ni zero yaani tz tuna safr ndefu!!
 
Hawa jamii ya watu wa bara la asia hawa ni shida sana,
Ufilipino huenda ikawa inaongoza kwa kua na mbwa wengi mno wanaozagaa hovyo lakini kama ilivyo tz tunavyosumbuliwa na malaria wao gonjwa lao hatari ni kichaa cha mbwa.
Uwepo wa mbwa Ufilipino uligeuka fursa baada ya maelfu kwa maelfu ya mbwa kukamatwa na kwenda kuuzwa vietnam kwani huko nyama ya mbwa inaliwa kuliko nyama yoyote ile.
Hapa tz unaweza ona nyama ya punda inasindikwa na ukawa na imani kwamba wanasafirisha kwenda uchina lakini hawa jamaa hawashindwi kupandika nembo ya nyama ya ng'ombe wakatuuzia wabongo.
 
Hv hawa WACHINA si walikamatwa na NEMC tena ilitangazwa kabisa na kiwanda kufungwa cha punda..!! IWEJE HADI LEO BADO WANAENDELEA..? Hv hii nchi kuna nn..? Wachina hawa wataimaliza nchi hii.. Leo nimeona ITV news, PUNDA wengi ktk malori eti wanapelekwa DODOMA..!!

Hawa wachina kwnn serikali inawaacha wanafanya laana hii kubwa ktk nchi yetu..? Wachina ni watu wabaya sana... Wale tu wanaofanya kazi za ujenzi ndio waruhusiwe kuwa nchini... Mtaani na kwingineko hawatakiwi hawa...
Hili linamhusu January Makamba, naona yuko kimya anapotezea kazi yake kama hayupo.
 
Back
Top Bottom