The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 2,195
- 3,309
Kama serikali yetu ingekuwa na chembe ya uungwana ilitakiwa itoke na kuomba radhi kwa madhila yaliyotokea kwenye zilizoitwa chaguzi katika miaka tajwa hapo juu.
Na kwa ushahidi huo ilipaswa CCM Ione aibu ya kujisifia uongo kwamba wanashinda kwa kishindo badala yake walipaswa kufanya juu chini kufuta makovu waliyoyasababisha kwenye hizo chaguzi zilizopita.
Mkuu wa wilaya, Nape, Kamanda wa polis, Mchengerwa na hata Rais Magufuli alipata kusema haiwezekani akuteue yeye alafu wewe umtangaze mpinzani kuwa ameshinda.
Huu wote ni ushahidi kwamba serikali ilikusudia na kwa makusudi hujipanga kudhulumu uchaguzi.
Hivi unajivuniaje hii dhuluma!?
Na ninyi machawa humu ndani mnajivuniaje hii dhuluma!?
Nashauri serikali itoke iombe radhi kwa huu udhalimu uliolinajisi taifa letu.
Na kwa ushahidi huo ilipaswa CCM Ione aibu ya kujisifia uongo kwamba wanashinda kwa kishindo badala yake walipaswa kufanya juu chini kufuta makovu waliyoyasababisha kwenye hizo chaguzi zilizopita.
Mkuu wa wilaya, Nape, Kamanda wa polis, Mchengerwa na hata Rais Magufuli alipata kusema haiwezekani akuteue yeye alafu wewe umtangaze mpinzani kuwa ameshinda.
Huu wote ni ushahidi kwamba serikali ilikusudia na kwa makusudi hujipanga kudhulumu uchaguzi.
Hivi unajivuniaje hii dhuluma!?
Na ninyi machawa humu ndani mnajivuniaje hii dhuluma!?
Nashauri serikali itoke iombe radhi kwa huu udhalimu uliolinajisi taifa letu.