Kiukweli, Lowassa anaitesa CHADEMA

Kiukweli, Lowassa anaitesa CHADEMA

Ni shabiki wa kutupwa wa cdm na msimamo wangu uko wazi. Walichokifanya cdm ni kama kuwa vitani halafu unamchukua kamanda wa wapinzani wako na kumpa ujemadari kupambana na huko akikotoka. Kibaya zaidi huyo kamanda mamluki hana uwezo wa kujenga hoja zaidi ya siasa za chini ya meza. Hv viongozi wa cdm hamuoni haya malalamiko yetu kila siku kwamba hapo tumelamba galasa?
Tumelamba galasa kwelikweli...Mbowi kauza chama chetu kwa bei poa halafu kibaya zaidi amekula peke yake.
 
Petro Mselewa nlikua nakuonaga una akili ila kumbe na wewe sawa na Lizaboni tu na wachumia tumbo wengine.

Unaezaje kuja na hoja finyu kama hii? Ungetafuta namna nyingine ya uandishi ambayo ungeelezea mambo vzur lakini siyo kimbea mbea kama ulivyoleta hii.

Chadema wameshindwa nini?

Kwanini ninyi na mtukufu wenu mmeamua kuzuia mikutano ya hadhara ya kisiasa?

Huyo anaeibaka katiba ya nchi kwa kuwakamata wapinzani kila uchwapo humuoni na kumsema unaisema CDM.

Mimi sina chama ila unafiki ni kitu ovyo kabisa..

Leadership is a confidence and not the use of power!!!
 
Huu UMBEA, UNAFIKI na UCHONGANISHI sio wa kuwachonganisha wanaCHADEMA.

Labda wanalumumba.
 
Mimi binafsi naona kimebaki kuwa chama cha viongozi wanaojilia pesa zao, kwa raha zao bila kujali wananchi au wanachama wao.

Chadema mvuto hakuna kabisa, kama kabla ya uchaguzi.

Hata nani awe humo hasiwepo sasa hivi ni sawa tu, wafuasi wasubiri uongo mwingine washikilie bango wao wale.
Utawasikiaje CHADEMA wakati mikutano ya hadhara imepigwa marufuku?

Hata mikutano tu ya amani ya chama hairuhusiwi, mkikutana unashangaa polisi hawa hapa.

Ipingeni kwanza sera zinazozuia Demokrasia ya kweli kabla ya kuilaumu CHADEMA.
 
Mm binafsi naamini CDM wangepata wabunge zaidi na kura zaidi ya walizopata hata bila Lowassa, kiufupi Lowassa ndiye aliyefaidika zaidi na UKAWA kuliko UKAWA walivofaidika na Lowassa.
Huwa nikikaa na kuifikiria UKAWA ile kabla ya ujio wa Lowassa dhidi ya CCM vipande vipande, majibu yangu siku zote yanabaki CCM mshukuruni Lowassa na Mbowe!
Japo kwa upande mwingine huwa namuelewa Mbowe, nadhani alihofia Lowassa kwenda ACT kitu ambacho kingeharibu ushindani tuliouona!
Tatizo ni uhuru wa kufanya mikutano haipo tena

Demokrasia imeminywa na hakuna uhuru hata wa kufanya mikutano ya amani ya chama.
 
Hongera kwa kusema ukweli kijana wangu. Najua utatukanwa lakini,umeongea ukweli mtupu. Kwa sasa wamebaki na hoja moja tu...eti mtu akifa wanasema 'kafa sababu alimsema Lowassa'...ndio hivyo tena toka siasa za hoja hadi siasa za ramli. Kuelekea uchaguzi mkuu 2010 walitangazia umma kuwa chadema haitasimamisha Wagombea kumpinga Sitta,Mwakyembe,Olesendeka kwa jinsi walivyosimamia ufisadi serikalini lakini eti sasa wamekuwa maadui wao...wanasema eti ripoti ya Richmond ilikuwa ni uongo.
Kinachoiangamiza Chadema ni kuwa vigeugeu.
Hawaaminiki.
 
Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu. Humu humu JF nimewahi kuandika hivi: Sikubaliani na hoja ya Lowassa Kujiengua CCM na Kujiunga CHADEMA/UKAWA. Andiko langu hilo, nikiwa kama mtanzania nisiye na chama chochote cha siasa, lililenga kukosoa kujiunga kwa Lowassa huko CHADEMA.

Maneno hayo sasa yanakuwa ya uhalisia. Tangu Lowassa ajiunge CHADEMA, pamoja na kinachosemwa kuwa CHADEMA/UKAWA imeongeza idadi ya Wabunge na kuminywa kwa demokrasia, wanaCHADEMA kindakindaki wamekuwa kama 'wamejitenga' na chama chao. Wanakosa hoja za kukosoa masuala ya ufisadi kwakuwa waliyekuwa wakimsema sasa wanaye.

Tangu Lowassa kujiunga na CHADEMA, CCM imeibeba ajenda ya kupambana na ufisadi. Haikuwahi kutokea CCM kutamka hadharani kupambana na ufisadi kwenye kampeni zake au hata kwenye utawala wake kwa kujiamini kuliko kuanzia siku Lowassa alipojiunga na CHADEMA. Ufisadi, kama hoja ya kujidai kwa wananchi, umepokwa na CCM toka CHADEMA!

Kimsingi, hata kama ni kimya kimya, Lowassa anaitesa CHADEMA. Anawabana wasipate cha kusema kuhusu ufisadi. Imekuwa rahisi kwasasa kwa wanachama wa CCM kupindisha kila hoja ya ufisadi toka kwa CHADEMA kwa kusema kuwa hata Lowassa aliyesemwa miaka nenda miaka rudi naye yuko CHADEMA.
mi nadhani kwa uelewa wangu,hata kama asingekuwepo Lowassa,maadamu ccm wameibeba ajenda hiyo(ingawa sijakubaliana na namna inavyoshughulikia huo ufisadi,labda kama pia hakubaliana na ufisadi wote uliowahi kutajwa na chadema sasa wao wanatafuta ufisadi mpya) ni lazima kama chama cha siasa kiangalie jambo jipya. Fikiria chadema iseme ufisadi,ACT ufisadi,Cuf ufisadi,ccm ufisadi mambo mengine je?
Ajande ifanyiwe kazi,chadema wao waliimba,sasa leo sitarajii chama tawala kiimbe wimbo wa ufisadi badala ya kufanyia kazi ufisadi.

Awepo EL,asiwepo haiwezi kubaki chadema ya 2010.
Tuache kuvilisha maneno ya ajenda vyama vya siasa,Tuangalie uwajibikaji zaidi,maana hata chadema wakibaki na ajenda ya ufisadi midomoni haina maana. Rais afanyie kazi ubadhirifu wote uwe wa nyuma,sasa hata baadae ilimradi tunaokoa wachache kujilimbikizia mali na kulitia hasara taifa.
 
Mtoa mada umesema vyema. Tatizo moja lililopo kwa wanachama na hasa vyama vya upinzani hawachambui mambo kwa uhalisia wake bali wanafuata matakwa ya baadhi ya viongozi wao. Kwa mtindo kama huo wa kushindwa kuweka uhalisia wa mambo mbele basi tutegemee nchi kuwa na siasa chafu kwa muda mrefu. Hata chama tawala kina mapungufu kama hayo japo kwa namna flani sasaivi ni kama wanaanza kubadili mwelekeo.

Upinzani wa kweli ni ule unaolenga uhalisia na sio unafiki.
 
Chadema kwisha malegea. Ni mjinga pekee ndiye anaweza fikiria chadema bado ipo. Sina hamu nao hawa majamaa. Hawaeleweki mwanzo mwisho, hawa jamaa sasa ni wa hovyo kama walivyo ccm tuliyokuwa tunaisema kila siku.
 
Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu. Humu humu JF nimewahi kuandika hivi: Sikubaliani na hoja ya Lowassa Kujiengua CCM na Kujiunga CHADEMA/UKAWA. Andiko langu hilo, nikiwa kama mtanzania nisiye na chama chochote cha siasa, lililenga kukosoa kujiunga kwa Lowassa huko CHADEMA.

Maneno hayo sasa yanakuwa ya uhalisia. Tangu Lowassa ajiunge CHADEMA, pamoja na kinachosemwa kuwa CHADEMA/UKAWA imeongeza idadi ya Wabunge na kuminywa kwa demokrasia, wanaCHADEMA kindakindaki wamekuwa kama 'wamejitenga' na chama chao. Wanakosa hoja za kukosoa masuala ya ufisadi kwakuwa waliyekuwa wakimsema sasa wanaye.

Tangu Lowassa kujiunga na CHADEMA, CCM imeibeba ajenda ya kupambana na ufisadi. Haikuwahi kutokea CCM kutamka hadharani kupambana na ufisadi kwenye kampeni zake au hata kwenye utawala wake kwa kujiamini kuliko kuanzia siku Lowassa alipojiunga na CHADEMA. Ufisadi, kama hoja ya kujidai kwa wananchi, umepokwa na CCM toka CHADEMA!

Kimsingi, hata kama ni kimya kimya, Lowassa anaitesa CHADEMA. Anawabana wasipate cha kusema kuhusu ufisadi. Imekuwa rahisi kwasasa kwa wanachama wa CCM kupindisha kila hoja ya ufisadi toka kwa CHADEMA kwa kusema kuwa hata Lowassa aliyesemwa miaka nenda miaka rudi naye yuko CHADEMA.

Utakuwa na akili mbovu kupita maelezo kuamini kuwa ndani ya CCM ufisadi umeisha baada ya lowassa kuondoka.
Unataka kuniambia kuwa kashfa zote za kifisadi zilizotokea na zinazoendelea kutokea,lowassa anahusika?
Tangu Lowassa aondoke madarakani mwaka ule wa 2008,hakuna kashfa yoyote ya kifisadi ndani ya ccm?
Unataka chadema wamfanyaje lowassa wakati vyombo vinavyohusika na usimamizi wa mali za umma hazijamfikisha mahakamani?
Embu niambie tuhuma za miaka dahari ambazo hazijadhibitishwa mahali popote,kwa nini tuendelee kuziamini?
Kuna kashfa ngapi zimeibuliwa baada ya ishu ya richmond na kupelekwa mahakamani,kwa nini hili la ufisadi wa lowassa hawapeleki mahakamani mbivu na mbichi zijulikane kuliko kuendelea kuchafua taswira ya mtu?
Ninaamini hakuna mtu ndani ya cheadema anayeshindwa kuzungumzia ufisadi eti kwa sababu ya uwepo wa lowassa chadema kwani ishathibitika pasipo shaka kuwa zote zilizosemwa juu yake ilikuwa siasa chafu kwani kama sio siasa chafu wangeshampeleka mahakamani.
Tuhuma gani hii isiyopelekwa mahaamani?
 
Kuja hapa kusema CHADEMA inateswa na ufisadi haimsaidii mtu yeyote.. it is a good consolation for buffoons. Wote mnajua tatizo liko wapi. Chadema haina dhamana yoyote katika nchi hii. Hakuna mfumo ambao umejengwa na Chadema ambao sasa unaathiri maisha ya watanzania, haupo. Don't fool yourself, you know where the problem is...
 
Chadema wamekuwa na kila aina ya sifa mbaya. Ndumila kuwili, ukigeugeu, hakuna wanachosimamia sasa. kisingizio kimebaki eti kunyimwa mikutano, mbona tangiapo mikutano ilikuwa inazuiwa na mambo yalikuwa yanakwenda? Hadhi yao na kudharaulika na watawala ilitamalaki baada ya kupokea mtu aliyetupwa na ccm pamoja na umaarufu wake aliyokuwa nayo. Ndiyo maana Chadema wakisema lolote wanaonekana mbwa koko tu anayebweka bila kufanya lolote. Ukweli mchungu Chadema walisafiria nyota ya Dr. Slaa walivyokuwa wajinga eti wakaanza kumtukana na kumdhalilisha, malipo ni haahapa Duniani.Ukweli ni kwamba jamaa hakuwa maarufu bali pesa zake ndizo zilimfanya awe maarufu ndani ya ccm mtandao, hata kura alizopata na wabunge ni kutokana na umaarufu wa chadema iliyokuwa nao wala sio yeye. kwanini hakwenda NCCR au chausa?
 
Hata mwizi kufurahia sana moyoni anapoona hakuna uwezekano wa kukamatwa... Lakini hiyo haijawahi kuondoa ukweli kwamba yeye ni mwizi. Muda ni mwalimu mzuri sana. Mliuza sera hiyo uchaguzi uliopita na matokeo yake Chadema lipata 40% ya kura za Urais (Mbali na yale mambo yenu mnayofanyaga ya kuiba na kuvuruga). Hamkujifunza, na bado hamjajifunza. Mnafikiri wale wale mlioshindwa kuwadanganya wakati ule, sasa watakuwa wajinga zaidi.... wakati huo mkisema vile, mnaendelea kukumbatia na kutetea rushwa. Leo Chadema ikipeleka mswaada wa kuwachukulia hatua wale waliohusika na rushwa ya Lugumi au Escrow, ni wabunge wa chama chenu ndio watakaosimama kupinga hoja hiyo! kisha mkitoka huko, mnakimbilia hapa jf kuja kutwambia wala rushwa wako Chadema na hawako kwenye chama chenu! We know, and we are watching... you can't fool us.
 
Hata mwizi kufurahia sana moyoni anapoona hakuna uwezekano wa kukamatwa... Lakini hiyo haijawahi kuondoa ukweli kwamba yeye ni mwizi. Muda ni mwalimu mzuri sana. Mliuza sera hiyo uchaguzi uliopita na matokeo yake Chadema lipata 40% ya kura za Urais (Mbali na yale mambo yenu mnayofanyaga ya kuiba na kuvuruga). Hamkujifunza, na bado hamjajifunza. Mnafikiri wale wale mlioshindwa kuwadanganya wakati ule, sasa watakuwa wajinga zaidi.... wakati huo mkisema vile, mnaendelea kukumbatia na kutetea rushwa. Leo Chadema ikipeleka mswaada wa kuwachukulia hatua wale waliohusika na rushwa ya Lugumi au Escrow, ni wabunge wa chama chenu ndio watakaosimama kupinga hoja hiyo! kisha mkitoka huko, mnakimbilia hapa jf kuja kutwambia wala rushwa wako Chadema na hawako kwenye chama chenu! We know, and we are watching... you can't fool us.
 
Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu. Humu humu JF nimewahi kuandika hivi: Sikubaliani na hoja ya Lowassa Kujiengua CCM na Kujiunga CHADEMA/UKAWA. Andiko langu hilo, nikiwa kama mtanzania nisiye na chama chochote cha siasa, lililenga kukosoa kujiunga kwa Lowassa huko CHADEMA.

Maneno hayo sasa yanakuwa ya uhalisia. Tangu Lowassa ajiunge CHADEMA, pamoja na kinachosemwa kuwa CHADEMA/UKAWA imeongeza idadi ya Wabunge na kuminywa kwa demokrasia, wanaCHADEMA kindakindaki wamekuwa kama 'wamejitenga' na chama chao. Wanakosa hoja za kukosoa masuala ya ufisadi kwakuwa waliyekuwa wakimsema sasa wanaye.

Tangu Lowassa kujiunga na CHADEMA, CCM imeibeba ajenda ya kupambana na ufisadi. Haikuwahi kutokea CCM kutamka hadharani kupambana na ufisadi kwenye kampeni zake au hata kwenye utawala wake kwa kujiamini kuliko kuanzia siku Lowassa alipojiunga na CHADEMA. Ufisadi, kama hoja ya kujidai kwa wananchi, umepokwa na CCM toka CHADEMA!

Kimsingi, hata kama ni kimya kimya, Lowassa anaitesa CHADEMA. Anawabana wasipate cha kusema kuhusu ufisadi. Imekuwa rahisi kwasasa kwa wanachama wa CCM kupindisha kila hoja ya ufisadi toka kwa CHADEMA kwa kusema kuwa hata Lowassa aliyesemwa miaka nenda miaka rudi naye yuko CHADEMA.
sahihisha kauli sema kiukweli Lowassa anaitesa sana chama cha ma.jizi ccm
 
Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu. Humu humu JF nimewahi kuandika hivi: Sikubaliani na hoja ya Lowassa Kujiengua CCM na Kujiunga CHADEMA/UKAWA. Andiko langu hilo, nikiwa kama mtanzania nisiye na chama chochote cha siasa, lililenga kukosoa kujiunga kwa Lowassa huko CHADEMA.

Maneno hayo sasa yanakuwa ya uhalisia. Tangu Lowassa ajiunge CHADEMA, pamoja na kinachosemwa kuwa CHADEMA/UKAWA imeongeza idadi ya Wabunge na kuminywa kwa demokrasia, wanaCHADEMA kindakindaki wamekuwa kama 'wamejitenga' na chama chao. Wanakosa hoja za kukosoa masuala ya ufisadi kwakuwa waliyekuwa wakimsema sasa wanaye.

Tangu Lowassa kujiunga na CHADEMA, CCM imeibeba ajenda ya kupambana na ufisadi. Haikuwahi kutokea CCM kutamka hadharani kupambana na ufisadi kwenye kampeni zake au hata kwenye utawala wake kwa kujiamini kuliko kuanzia siku Lowassa alipojiunga na CHADEMA. Ufisadi, kama hoja ya kujidai kwa wananchi, umepokwa na CCM toka CHADEMA!

Kimsingi, hata kama ni kimya kimya, Lowassa anaitesa CHADEMA. Anawabana wasipate cha kusema kuhusu ufisadi. Imekuwa rahisi kwasasa kwa wanachama wa CCM kupindisha kila hoja ya ufisadi toka kwa CHADEMA kwa kusema kuwa hata Lowassa aliyesemwa miaka nenda miaka rudi naye yuko CHADEMA.
MBONA SIJWAHI KUWASIKIA CHADEMA WAKILALAMIKA KUWA WANATESWA NA LOWASSA AU NI ILE STYLE YA ANAKUNWA MWINGINE NA ANAYESIKIA RAHA NI MWINGINE TOFAUTI NA ANAYEKUNWA?????????????
PUNGUZA JOTO LA NDEGE NA MWENDO KASI
 
Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu. Humu humu JF nimewahi kuandika hivi: Sikubaliani na hoja ya Lowassa Kujiengua CCM na Kujiunga CHADEMA/UKAWA. Andiko langu hilo, nikiwa kama mtanzania nisiye na chama chochote cha siasa, lililenga kukosoa kujiunga kwa Lowassa huko CHADEMA.

Maneno hayo sasa yanakuwa ya uhalisia. Tangu Lowassa ajiunge CHADEMA, pamoja na kinachosemwa kuwa CHADEMA/UKAWA imeongeza idadi ya Wabunge na kuminywa kwa demokrasia, wanaCHADEMA kindakindaki wamekuwa kama 'wamejitenga' na chama chao. Wanakosa hoja za kukosoa masuala ya ufisadi kwakuwa waliyekuwa wakimsema sasa wanaye.

Tangu Lowassa kujiunga na CHADEMA, CCM imeibeba ajenda ya kupambana na ufisadi. Haikuwahi kutokea CCM kutamka hadharani kupambana na ufisadi kwenye kampeni zake au hata kwenye utawala wake kwa kujiamini kuliko kuanzia siku Lowassa alipojiunga na CHADEMA. Ufisadi, kama hoja ya kujidai kwa wananchi, umepokwa na CCM toka CHADEMA!

Kimsingi, hata kama ni kimya kimya, Lowassa anaitesa CHADEMA. Anawabana wasipate cha kusema kuhusu ufisadi. Imekuwa rahisi kwasasa kwa wanachama wa CCM kupindisha kila hoja ya ufisadi toka kwa CHADEMA kwa kusema kuwa hata Lowassa aliyesemwa miaka nenda miaka rudi naye yuko CHADEMA.
Unaweza kuwa sahihi katika mtazamo fulani,lakini hauko sahihi katika mtazamo wa jumla. Ni kweli Chadema walibeba ajenda ya ufisadi nchini, na ni kweli Chadema walitaja orodha ya mafisadi akiwemo Lowassa. Na ni vizuri kufahamu kwamba tuhuma za ufisadi wa Lowassa msingi wake ni suala la Richmond, ambalo baadaye tulikuja kusikia maelezo mengi tu. Kwa ufupi ukweli kuhusu Richmond uliishafunuliwa.

Chadema hawakumtaja Lowassa peke yake katika orodha ya mafisadi. Sasa kama tunakubaliana na orodha ya mafisadi waliotajwa na Chadema maana yake ni kwamba ndani ya CCM kuna mafisadi wengi tu na ambao wanaendelea kuheshimiwa na hata wewe mleta mada. Ni upuuzi kwa mtu kuamini kuwa CCM ndio waliobeba ajenda ya ufisadi ilhali tunaona kuna masuala ya Lugumi, milioni kumi kumi, escrow; na mengine mengi. Ni CCM ndio wanaohakikisha, kwa gharama kubwa, wanadhibiti uhuru wa maoni hii ni ili kuficha ufisadi ambao ndio sehemu ya maisha ya chama hicho. Ni ajabu leo hii kuwaamini CCM kama wabeba ajenda ya ufisadi ilhali wamekaa na Lowassa miaka yote hiyo wakimwambudu hadi alipoamua mwenyewe kuachana na chama hicho.

Ni jambo muhimu kufahamu. Kwamba Lowassa ni fisadi pale anapotaka kugombea urais,lakini ni mtu mwema na asiye na doa akiamua kukaa kimya na kufanya yake akawaachia wengine nafasi hiyo. Sasa kama Chadema hawana ajenda ya ufisadi kwa nini wamewazuia kufanya siasa? Kwamba CCM hawakuwahi kusema kuwa watapambana na ufisadi hadi Lowassa alipohama chama, ni kauli ya ajabu sana maana ilani zote za uchaguzi za CCM za miaka ya karibuni zimeweka mikakati ya kushughulika na ufisadi. Lakini itakuwa ni ajabu pia kama CCM walikuwa hawawezi kukemea ufisadi kwa kuwa kulikuwa na Lowassa fisadi ambaye hawawezi hata kumfikisha mahakamani.

Kugeuza Chadema kuwa ni mafisadi kwa kuwa tu wamempokea Lowasa waliyemtuhumu kuwa fisadi, ni hoja ya kijinga. Na kwa hili CCM wanataka kuendelea kutumia 'ujinga'wa wengi wa kutotaka kufikiri sawa sawa ili kujihalalisha.
 
Back
Top Bottom