Hapana sio ushamba ni mapendeleo yako tu.
Ni sawa na mtu mmoja anavuta sigara mwingine havuti, Kuna anayependa kula ugali na mlenda wakati mwingine hataki hata kuona.
Mara yangu ya kwanza kumuona pweza (samaki) pale ferry nilishangaa sana kuwa Kuna watu wanakula hilo lidude???????. Huwezi amini kaka yangu alinipeleka kwa mpemba mmoja maeneo ya mwenge pale akanunua pweza tukala.......lahaulaaaa! tangu hapo sikuwahi kuacha kula pweza.
Ndivyo maisha yalivyo. Kuna jambo unaweza kushangaa hivi inakuwaje kuwaje mtu anafanya hivo? Lakini ukweli unabaki kuwa ndio hivo anafanya, maisha yako na maajabu ( mbwembwe) mingi sana