Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,504
- 911,249
1) Tangia abanduliwe ubavuni mwangu
Haachi usumbufu wake kwangu, arghh!
Kisa ni kiu yake apendayo niitulize vilivyo!
Lolote nilifanyalo haridhiki hadi hilo nimfanzie!
Kiu ya mwanamke waijua wewe?
2) Kunipenda yaani hana jinsi, yabidi tu!
Kama alinyofolewa ubavuni kwangu!
Watarajia nini kama siyo kuwa na upendo?
Aniumapo sikio nikunihakikishia mahaba tu!
Kiu ya mwanamke waijua wewe?
3) Ubavu wangu wa mashoto umejaa mahaba!
Asiponipenda hivi atapenda nini haswa walakini?
Alichonacho alipewa kwa matumizi yangu wajamani!
Asichonacho hata miye sikihitaji na hili halina usiri!
Kiu ya mwanamke waijua wewe?
4) La ajabu ni hii kiu yake ambaye inapingana nami!
Kumtulizia kiu yake lazima nijisalimishe kwake!
Aliumbwa anitumikie sasa ataka kunigeuzia kibao!
Kunitawala ndiyo hulka yake nami ananikwaza
Kiu ya mwanamke waijua wewe?
Haachi usumbufu wake kwangu, arghh!
Kisa ni kiu yake apendayo niitulize vilivyo!
Lolote nilifanyalo haridhiki hadi hilo nimfanzie!
Kiu ya mwanamke waijua wewe?
2) Kunipenda yaani hana jinsi, yabidi tu!
Kama alinyofolewa ubavuni kwangu!
Watarajia nini kama siyo kuwa na upendo?
Aniumapo sikio nikunihakikishia mahaba tu!
Kiu ya mwanamke waijua wewe?
3) Ubavu wangu wa mashoto umejaa mahaba!
Asiponipenda hivi atapenda nini haswa walakini?
Alichonacho alipewa kwa matumizi yangu wajamani!
Asichonacho hata miye sikihitaji na hili halina usiri!
Kiu ya mwanamke waijua wewe?
4) La ajabu ni hii kiu yake ambaye inapingana nami!
Kumtulizia kiu yake lazima nijisalimishe kwake!
Aliumbwa anitumikie sasa ataka kunigeuzia kibao!
Kunitawala ndiyo hulka yake nami ananikwaza
Kiu ya mwanamke waijua wewe?