TANZIA Kitundu wa tamthilia ya juakali afariki dunia

TANZIA Kitundu wa tamthilia ya juakali afariki dunia

jamaikatz

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2023
Posts
369
Reaction score
1,252
Aliyekuwa muigizaji wa Tamthilia ya JUAKALI maarufu kama Kitundu amefariki dunia jioni ya Leo, Juni 24. Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na @lamataleah ambaye ni muongozaji wa Tamthilia hiyo pendwa nchini.

Bado chanzo cha kifo cha muigizaji huyo hazijajulikana. Familia ya CROWN MEDIA inapenda kutoa pole kwa familia ya juakali tamthilia kwa pigo hilo kubwa.

Pumzika kwa Amani Kitundu.

snapins-ai_3662217088874064435.jpg
 
Mnyama kadondoka, asili imechukua mali yake, haya wengine tuendelee na maisha,

Mnyama kafa bila Jina, anatambulika kama Jamaa wa Jua Kali
Mnyama, ukiwa mtumwa, utakufa kama rafiki Yako mbwa,

Mnyama, angekuwepo angewaambia, kati yake na mtu ni nani alikuwa wa kwanza Kufa,
Ni mtu, na Kabla ya Kufa madaktari tayari walimkaribisha ndugu yake MTU anaitwa Sababu, Ili waweze kuondoka wote duniani

Nnaambiwa mtu anazima kama Mwanga wa tochi iliyoisha betri, na haendi mbinguni Wala peponi,

Kwaheri mnyama, kwaheri ya kutokuonana, Kwa maana Nami nitakuwa mfu mnyama, na sitokuona Tena,
 
Last time naangalia Tamthilia ya Jua Kali miaka ya hivi karibuni,nilimuona Kitundu kama amedhoofu sana kiafya.

Let us say " Upumzike kwa Amani kijana mdogo sana"
 
Apumzike kwa Amani, huyo dogo alikua na talent kubwa sana, alishaenda South africa na Kenya kupitia tamthilia ya jua kali kutokana na scene alizopangiwa
Apumzike kwa Amani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom