Kituko JNIA mgahawani: Immigration hii si sawa!

Kituko JNIA mgahawani: Immigration hii si sawa!

Nasafiri kwenda Mwanza flight FN 141 kuelekea Mwanza.
Kabla ya kupanda ndege naamua kupata kipasha moto, kahawa na keki, kwa kiswahili safi kabisa.

Namuuliza mhudumu kaunta aliyevaa shati bkuu, tai na kapendeza, muasia.

Cha kushangaza ananiuliza "what sir?"
Nashangaa, narudia tena kwa kiswahili.
Ajabu jamaa anasena"I dont understand sir"
Namuuliza "how did you get here, and where are you from"
Ananijibu "India sir"
Immigration, mtu asiyejua hata lugha ya kiswahili anafanya nini hapo?
Na ana kibali cha kazi au?

Sasa what is a big deal with this issue! I wish ungejua nchi za Europe zinazotumia lugha tofauti na kiingereza zimejaa watu wengi kutokea Afrika (watanzania wakiwepo)
wakifanya kazi za huduma na usafi lakini hawazungumzi kabisa lugha za nchi hizo.
 
Vipi unajisikia kufanya mdahalo na mimi,au unani quote kwa kujisikia tu .........???
Najua umenielewa,na hicho ndio kitu muhimu,hizi papara papara zingine za ushindani usio kua na maana hazitokufaa kitu.
 
Najua umenielewa,na hicho ndio kitu muhimu,hizi papara papara zingine za ushindani usio kua na maana hazitokufaa kitu.
Mimi huwa naongea vitu ninavyovijua sio ninajiropokea tu, kwa mfano hizo nchi ulizozitaja unajua sheria zao za kazi ............... Lakini kama hizo nchi sheria zao za kazi HAZIZUII KWA RAIA WA KIGENI KUFANYAKAZI NA HAJUI LUGHA YA WENYEJI,HILO SIO TATIZO NA MIMI SIONGELEI WA AINA HIYO. LAKINI KAMA SHERIA ZAO ZA KAZI ZINAMKATAZA MGENI HASIYEJUA LUGHA YA WENYEJI KUFANYAKAZI NCHINI KWAO,LAKINI WAPO BASI NA WAO WANA MATATIZO KAMA YETU.
 
Sasa what is a big deal with this issue! I wish ungejua nchi za Europe zinazotumia lugha tofauti na kiingereza zimejaa watu wengi kutokea Afrika (watanzania wakiwepo)
wakifanya kazi za huduma na usafi lakini hawazungumzi kabisa lugha za nchi hizo.
Tanzania ni chini ya 20% ndiyo wanajua English. sasa kama naenda Mwanza ntanunuaje keki na kahawa hapo mgahawani na Lugha sijui?
 
Hauna hoja ndugu yangu. Suala la mgahawa liko chini ya mamlaka ya uwanja wa ndege JNIA sasa uhamiaji wanahusika vp hapo. Ulishawahi kupewa chakula na uhamiaji?
Mkuu kama una uwezo mdogo wa kufikiri usijiumbue!
Nijibu swali moja tu ili ugutushe ubongo wako.
Mgeni anapoingia nchini kuanzia airport su bandarini, hujui kuwa afisa wa kwanza kabisa kumkagua ni wa Immigration?
Huyo afisa atamuuliza sababu za kuja nchini na muda atakaoishi, na mwenyeji wake.
Kama ni mtalii kuna vibali vyake, na kama ni kufanya kazi immigration watatoa vibali kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kwa hiyo hebu gutuka bure tu na ku imagine mtu asiyejua hata kusalimia kiswahili na anafanya kazi mgahawani, a public area.

Hii inaonyesha tu jinsi watu kama wewe mnavyoweza ku support uozo wowote unaoingia nchini, mradi business as usual.
 
Pamoja na kujifanya wewe ndio mjuaji zaidi na mwenye IQ ya juu lakini ndio wale wale tu,

Chukulia mfano wa Dubai international airport,kuna wahudumu/waiters kibao tu kwenye migahawa ya airport na hawajui kiarabu na wala sio waarabu! Qatar,Saudi arabia na hata Ujerumani ni hivyo hivyo pia,

Unaonekana hujawahi kutoka nje ya mipaka ya Tz,unaandika kwa hisia tu,mimi naandika/nacomment kwa experience.

Mleta mada bila shaka itakua hiyo ni mara yako ya kwanza kutumia Airport kwa ajili ya safari ndio maana umeshangaa kuona vitu ambavyo ni vya kawaida tu kwenye nchi nyingi tu.
Mkuu experience yako ni ya kitoto!
Na pengine kama ulisafiri unasahau kuwa airport zote duniani hutumia lugha mama kwanza na lugha kama kiingereza as a second option.

Usijifanye kuwa umesafiri sana wakati outstanding points huzioni.
 
Tanzania ni chini ya 20% ndiyo wanajua English. sasa kama naenda Mwanza ntanunuaje keki na kahawa hapo mgahawani na Lugha sijui?
Na hizo nchi nilizokuambia hali ni kama Tanzania. Na watu bado wanaweza kuwasiliana hata kwa kutumia broken english, au lugha nyingine. Ikibidi hata unaonyesha kwa mkono au unaomba mtu anakupa msaada. Tatizo letu watanzania huwa tunajiona kama kutojua kiingereza ni dhambi yenye kubeba aibu kubwa! Mimi sijaona tatizo lolote serious unless uwe hujasafiri nchi nyingine na kuona hali halisi.
 
Mkuu experience yako ni ya kitoto!
Na pengine kama ulisafiri unasahau kuwa airport zote duniani hutumia lugha mama kwanza na lugha kama kiingereza as a second option.

Usijifanye kuwa umesafiri sana wakati outstanding points huzioni.
Hali halisi: Ni watanzania wangapi huwa wanautumia huo mgahawa, na tena hawajui kiingereza? Hapo airport huwa napita sana na mara nyingi naona wateja wazungu kuliko waafrika. Na nadhani ndio maana mwenye mgahawa hakuona umuhimu wa kiswahili kwa huyo mfanyakazi. Katika vitabu vya sheria vya Tanzania hakuna sheria inayomlazimisha mfanyabiashara ya huduma kama hoteli kuajiri wafanyakazi wenye kujua kiswahili. Hii thread umeanzisha kwa kukurupuka.
 
Mkuu kuna wanyarwanda na wakenya wengi tu serikali imeshindwa kuwaondoa nchini kabisa, wanaajiriwa kwenye taasisi binafsi hasa makampuni na kisha kutoa rushwa wapewe vibali vya kazi au uraia.
 
Mkuu kama una uwezo mdogo wa kufikiri usijiumbue!
Nijibu swali moja tu ili ugutushe ubongo wako.
Mgeni anapoingia nchini kuanzia airport su bandarini, hujui kuwa afisa wa kwanza kabisa kumkagua ni wa Immigration?
Huyo afisa atamuuliza sababu za kuja nchini na muda atakaoishi, na mwenyeji wake.
Kama ni mtalii kuna vibali vyake, na kama ni kufanya kazi immigration watatoa vibali kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kwa hiyo hebu gutuka bure tu na ku imagine mtu asiyejua hata kusalimia kiswahili na anafanya kazi mgahawani, a public area.

Hii inaonyesha tu jinsi watu kama wewe mnavyoweza ku support uozo wowote unaoingia nchini, mradi business as usual.
You are wrong! HAKUNA sheria inayosema mtu anayekuja kufanya kazi Tanzania ni lazima ajue kiswahili!
 
Maajabu ya huu mgahawa wa JNIA..

Soda ya chupaaaaaa.... tshs 3,500...

Sodaaaa... tshs. 3,500... na serikali ipo inaangalia tu.. huu ni wizi na ujambazi wa wazi, na hasira sana na huyu mchina kafungua hii Cafeteria pale JNIA... na hasira sana
 
Tanzania ni chini ya 20% ndiyo wanajua English. sasa kama naenda Mwanza ntanunuaje keki na kahawa
Mkuu experience yako ni ya kitoto!
Na pengine kama ulisafiri unasahau kuwa airport zote duniani hutumia lugha mama kwanza na lugha kama kiingereza as a second option.

Usijifanye kuwa umesafiri sana wakati outstanding points huzioni.
Wewe bora ungekua mkweli tu kua umeanzisha hii thread ili tujue tu kua na wewe umepanda domestic flight,unaongea pumba tu wala huna ujualo,tembea uione dunia kwanza acha kukurupuka na kuandika vitu vinavyozidi kukudharaulisha tu hapa.
 
Wewe bora ungekua mkweli tu kua umeanzisha hii thread ili tujue tu kua na wewe umepanda domestic flight,unaongea pumba tu wala huna ujualo,tembea uione dunia kwanza acha kukurupuka na kuandika vitu vinavyozidi kukudharaulisha tu hapa.
Ha ha ha!
Mkuu ukiperuzi passports zangu in the last 20 yrs uta bloo!
Tumechezea usafiri wa ATC toka enzi za Boeing,Twin Otter na Fokker Friendship F50,
All the same you are a spineless novice!
 
Kuna kitu kingine mkuu chakula pale wana tu uzia sawa Na wa zungu wakati kwengine raiya wa nyumbani wana punguzo kubwa mno , huwezi nunua chakula sawa Na mgeni hiyo ipo kwetu tu ! Tena kwa [emoji385] usd!!
Labda tatizo liwe kwa USD.. Maana hata kwenye Migahawa yao wanatumia Rupees/Dollar. Lakini kusema kuwe na flat price.. One size fits all.. Hilo halipo. Watanzania tuache kulalamikia tumbo. Hili ndilo hutuponza msimu wa uchaguzi! Airport zote Duniani zinazo run migahawa ndani gharama/bei huwa hazichagui. That's business...and business of the business is a business! Ukiona hilo linakupa tabu.. Basi fakamia makande yako au ugali dagaa wa kutosha na ukifika Airport kuwa busy na simu yao.

Kwa akili za haraka wewe mzawa una advantage kubwa sana ya kufika Airport ukiwa umeshiba. Hata kama upo on transit una access ya kuingia Mama ntilie ukashiba pia. Mgeni kama hajala hotelini atalazimika kununua. Tuache kupenda matumbo. Huwa yanaligharimu sana Taifa...watoto hawana mikopo huko... Safari njema mkuu. Kama ulifika salama basi salimia familia yako! [emoji23]
 
Na hizo nchi nilizokuambia hali ni kama Tanzania. Na watu bado wanaweza kuwasiliana hata kwa kutumia broken english, au lugha nyingine. Ikibidi hata unaonyesha kwa mkono au unaomba mtu anakupa msaada. Tatizo letu watanzania huwa tunajiona kama kutojua kiingereza ni dhambi yenye kubeba aibu kubwa! Mimi sijaona tatizo lolote serious unless uwe hujasafiri nchi nyingine na kuona hali halisi.
unaona ni sawa kuhangaika hivyo nchini kwako? kama nchi zingine hufanya haihalalishi kuwa sawa.tunatakiwa kurahisisha huduma kwa watu wetu. ingekuwaje wahudumu wa mahotel makubwa wangekuwa hawajui kiswahili?
 
unaona ni sawa kuhangaika hivyo nchini kwako? kama nchi zingine hufanya haihalalishi kuwa sawa.tunatakiwa kurahisisha huduma kwa watu wetu. ingekuwaje wahudumu wa mahotel makubwa wangekuwa hawajui kiswahili?
Unaenda hizo sehemu au unatoa tu mvuke kama gari lililochemsha? Eti wahudumu wa mahoteli makubwa! Tanzania kuna mswahili asiyejua kiingereza hata kidogo anayekwenda hotel kubwa? Watu wa sampuli yako si huwa manasema vyakula vya ''kizungu'' vinanyonya damu?
 
Unaenda hizo sehemu au unatoa tu mvuke kama gari lililochemsha? Eti wahudumu wa mahoteli makubwa! Tanzania kuna mswahili asiyejua kiingereza hata kidogo anayekwenda hotel kubwa? Watu wa sampuli yako si huwa manasema vyakula vya ''kizungu'' vinanyonya damu?
kujua lugha kidogo na kuweza kuitumia bila tabu kwenye kuwasiliana ni vitu tofauti.
 
Wakiweka wazawa ni rahisi kuzamia kwenda mamtoni, isitoshe na msosi u karibu hapo
 
Back
Top Bottom