Kitu pekee ambacho Binadamu ameshindwa kukifanya

Kitu pekee ambacho Binadamu ameshindwa kukifanya

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,343
Reaction score
859,922
Bado binadamu si mkamilifu na mjuzi wa yote pamoja na ugunduzi na uvumbuzi kwenye nyanja za sayansi, teknolojia na ushirikina.

Kupitia nyanja hizi Dunia imekuwa kama Kijiji na magumu mengi yasiyowezekana yamewezekana
maendeleo ya kuweza kurusha chombo chenye uzito wa tani za kutosha na kikaruka mpaka anga tupu huko mbali kabisa na kuweza kuwasiliana nacho si jambo dogo hata kidogo.

Lakini vipi mwanga anaweza kuingia nyumbani mwako bila kuvunja hata kitasa na akafanya yake na kusepa bila wewe kujua?

Pamoja na yote hayo kuna hili dogo sana limeshindikana kabisa na siku hili likiwezekana. Dunia katika ulimwengu huu itakuwa kitu kingine kabisa, jambo hilo ni kurudisha wakati nyuma walau kwa Sekunde Moja Tu

Kwamba umeshafyatua risasi kwenye Bastola kisha ghafla ukaghairi! Uwezo wa kuirudisha nyuma risasi hatuna

Kwamba tumeshatamka neno lakini ghafla tukijua madhara yake tukataka kulirudisha mdomoni uwezo huo hatuna.

Mifano ni mingi ambayo matendo yake tungeweza kuyaghairi sekunde moja tu baada ya kutenda dunia hii tuliyonayo isingekuwa hivi ilivyo leo hii na saa hii

Just imagine ni kitendo cha sekunde moja tuu kizungu wanasema blink of an eye hubadilisha historia ya kila kitu sekunde ni kubwa sana. Ni kubwa kuliko saa moja yenye dakika 60.

Kwa uamuzi wowote unaotaka kuchukua katika zile sekunde za majeruhi. Tafakari tena na tena kabla hujaamua kutenda kwakuwa sekunde moja itakayofuata baada ya kitendo inatosha kubadili maisha yako milele

Kama uamuzi huo si wa kuumiza wala kuharibu basi una kheri milele lakini kama ni kinyume chake sekunde ile ya mwisho ndio imebeba furaha ama majuto yako mpaka kifo

Muda hauna kinyume hata kwa sekunde moja na muda huwa hausubiri mtu. Ukitenda tenda kwa tafakuri na ukiamua amua kwa hekima! Majuto yasijekuwa mjukuu

Vinyonga wote hawana Mama kwakuwa ili wazaliwe inabidi mama afe!
 
Eheee
Hembu turudi kwenye aya ya mwisho,
Hii mwanzo niliamini ni hivyo, baadae nikajua ni kamba, leo hii unataka unirudishe kaanani..

je kuna fact nyingne ya kushawishi zaidi ya ile Walikua wanasema eti akizaa(japo mi najua anataga) anapanda juu ya kilele anajiachia anapasuka...
 
Eheee
Hembu turudi kwenye aya ya mwisho,
Hii mwanzo niliamini ni hivyo, baadae nikajua ni kamba, leo hii unataka unirudishe kaanani..

je kuna fact nyingne ya kushawishi zaidi ya ile Walikua wanasema eti akizaa anapanda juu ya kilele anajiachia anapasuka...
Hilo ni fumbo.. Uhalisia huu hapa

 
Kuna kipindi nilikiona safari kama si itv wakimuelezea kinyonga, kua vinyonga wanataga na aina hyo pekee inapatikana tanzania ndio wanazaa. Pia wakasema kinyonga sio anakufa akizaa bali wakati mwingine ni kutokana na ukubwa wa kinyonga aliepo tumboni, hivyo angekua mwanadamu angefanyiwa operation , lakini kwa kua hakuna namna ya operation hvyo ndo anapasuka na huyo mtoto anatoka na yeye kufa
Pia wapo wanaozaa salama.
 
Bao unaweza ukalirudisha ukiona hela yako inaelekea kupotea mapemaaaa,

Hata kama halirudi huko linatokotoka, potelea mbali, ila sio kuuza mechi dk ya kwanza.
 
Kuna kipindi nilikiona safari kama si itv wakimuelezea kinyonga, kua vinyonga wanataga na aina hyo pekee inapatikana tanzania ndio wanazaa. Pia wakasema kinyonga sio anakufa akizaa bali wakati mwingine ni kutokana na ukubwa wa kinyonga aliepo tumboni, hivyo angekua mwanadamu angefanyiwa operation , lakini kwa kua hakuna namna ya operation hvyo ndo anapasuka na huyo mtoto anatoka na yeye kufa
Pia wapo wanaozaa salama.
Asante sana kwa ufafanuzi
 
Bao unaweza ukalirudisha ukiona hela yako inaelekea kupotea mapemaaaa,

Hata kama halirudi huko linatokotoka, potelea mbali, ila sio kuuza mechi dk ya kwanza.
Hahahaha unapeleka inje?
 
Vinyonga wote hawana Mama kwakuwa ili wazaliwe inabidi mama afe!
Pamoja na hiyo elimu uliyonayo bado unaamini huu upuuzi.? Bc huna tofauti na wale wanaosema zile ndege zinazotoa moshi mweupe ni roketi na viwanja vyao vipo Misri na SA
 

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vinyonga wote hawana Mama kwakuwa ili wazaliwe inabidi mama afe!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom