Kitilya wa TRA kupelekwa TANESCO ?

Kitilya wa TRA kupelekwa TANESCO ?

Mitambo ni real wakati hujui hata uchakavu wake ni wa kiasi gani? Kwa hiyo ukiwa na taratibu zako za manunuzi au za kuingia mikataba hata zikiukwa wewe huoni tatizo!!! Duh!

Sijachanga madawa popote pale niliyoyaandika yote ni facts ambazo zinaweza kuwa verified.


kuna vingi umeongea sio fact ni siasa tu za kina Rostam na Mwakyembe

huwezi kuiita kampuni ya kitapeli wakati mitambo yake unaitumia

tapeli maana yake 'hakuna kitu alichokupa' ni hewa tu

mitambo ilikuwepo na ipi mpaka leo

na Idrissa alikuwa right kutaka kununua na sio kuikodisha
 
Si bure, umetumwa! Kule nimekukuta na hoja hii hii. Mwisho utasema apewe Magogoni.

Kwanini usipewe wewe?, hujiamini?

Pitia posts vizuri usikurupuke, nimeshawaambia hilo. Wanipe waone kama ntakwenda kutafuta ruzuku ya Serikali.
 
Huyo Kitillya hata hapo TRA nadhani amesha overstay! Ndio wampe Tanesco?
 
Mwakyembe alitoa ripoti yake Bungeni kuhusu sakata la Richmond na kuweka bayana kwamba Wataalam wa Tanesco waliishauri Serikali isiingie mkataba na Richmond. Yeyote anayeifuatilia sakata la Richmond/Dowans anajua fika kwamba fisadi Rostam Azizi aliidanganya Serikali ili kupata mkataba ule. Kampuni yoyote ile inaposema uongo katika presentation yake basi ni kampuni ya kitapeli. Fisadi Rostam kuidangaya Serikali kwamba ana HQ ya kamouni yake Houston na pia ana uzoefu katika kazi ya kufua umeme ni utapeli ulioweza kumsaidia kupindisha taratibu na hatimate kupata mkataba kwa njia za udanganyifu, huo ni utapeli.

Serikali inapoweka taratibu zake za manunuzi au mikataba lazima zifuatwe kipengele kwa kipengele bila kupindisha hata kipengele kimoja. Wanapoanza kupindisha/kuzikwepa taratibu hizo ndio hapo nchi inaingia kwenye mikenge ya IPTL, uchimbaji wa dhahabu, Richmond, Rada n.k.

kuna vingi umeongea sio fact ni siasa tu za kina Rostam na Mwakyembe

huwezi kuiita kampuni ya kitapeli wakati mitambo yake unaitumia

tapeli maana yake 'hakuna kitu alichokupa' ni hewa tu

mitambo ilikuwepo na ipi mpaka leo

na Idrissa alikuwa right kutaka kununua na sio kuikodisha
 
Tanesco na makampuni mengi ya ummah yanahitaji wazungu tu kuiendesha....

nchi ya ajabu hiiii
tunaajiri wazungu kwa mpira
lakini hatutafuti wataalam wa kutoka nje kwa menejiment.....
hahahahaa, umenichekesha,,,,,tukodi ma-CEO sio
 
Kwanza ni mzee tayari anatakiwa apumzike maana umri wake hafai, pia ndiye huyu ambaye makampuni hayalipi kodi na anajua hafanyi lolote akazeeke mbali huko apishe vijana akacheze na wajukuu
 
Tanesco na makampuni mengi ya ummah yanahitaji wazungu tu kuiendesha....

nchi ya ajabu hiiii
tunaajiri wazungu kwa mpira
lakini hatutafuti wataalam wa kutoka nje kwa menejiment.....

Mkuu umesahau nani wale waliopewaga tanesco na mkapa! nusura waunguze mitambo ya mtera
 
Pitia posts vizuri usikurupuke, nimeshawaambia hilo. Wanipe waone kama ntakwenda kutafuta ruzuku ya Serikali.

Bila ruzuku utachemsha tu mkuu, billi tunazolipa hazitoshi hata kwa asilimia 75, ni ndogo sana kwa shirika kujiendesha bila govt subsidy hata kama mikataba yote ya kinyonyaji itafutwa. Tanesco inahitaji overhaul ya nguvu, si mchezo!
 
Bila ruzuku utachemsha tu mkuu, billi tunazolipa hazitoshi hata kwa asilimia 75, ni ndogo sana kwa shirika kujiendesha bila govt subsidy hata kama mikataba yote ya kinyonyaji itafutwa. Tanesco inahitaji overhaul ya nguvu, si mchezo!

Hakuna cha kuchemsha, mashirika yote ya umma yaliyoshindwa kuendeshwa kifaida na Serikali watu binafsi wameyachukuwa bila ruzuku ya Serikali na wanafanya vizuri tu. Mfano mzuri wa shirika kubwa ni NBC. Ilikuwa ni hasara tupu, sasa tunaona wanalipa kodi nyingi tu. TBL?
 
Wana Jf tuseme ukweli hakuna shirika linaloibiwa hujumiwa kama tanesco,govt hailipi,makampuni yanayoiuzia tanesco umeme na sisi wateja tunaiba sana umeme wa tanesco tunaita kupiga neutral.Na tanesco nao hawataki kusema kipato chao kwa siku mwezi
 
Usichanganye madawa...Waliokataa ni bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO, Nishati walikuwa wanamuunga mkono maana yule Ngeleja alijua kuna mgao wake toka kwa fisadi Rostam Aziz. Kumbuka pia hata kulipwa kwa $95 million kwa Dowans kuliridhiwa na Pinda, Ngeleja, Mwanasheria Mkuu, Na Serikali kwa ujumla tangu December 2010 lakini kutokana na kelele za Watanzania ndio hadi hii leo haijalipwa hata senti tano.

Na Mahakama ya Biashara mbona huitaji iliyotowa hiyo hukumu? na mahakama ya Uingereza ilipopelekwa pingamizi na TANESCO na kushindwa tena kisheria mbona huisemi? na Mahakama ya Tanzania kuamua walipwe mbona huisemi?

Sheria ni msumeno. Mitambo unayo halafu useme aliyeleta mwizi? kwanza mlipe halafu funguwa kesi yako kama kakuibia.

Leo mitambo hiyo hiyo ndio inasaidia mgao, ilikuwa inunuliwe yaishe, wenye mitambo badala ya kesi walishakubali kama mnaitaka nunuweni basi, Idrisa akashauri inunuliwe na Zitto Kabwe akashauri inunuliwe, mijinga fulani ikakataa, sasa gharama zote zinalipwa, kuinunuwa hamjainunuwa, bado mnaikodisha kwa kuwa tu inaonekana sasa ni ya Kimerekani.

Miafrika Ndivyo Ilivyo - Nyani Ngabu
 
Kwanini kodi iondolewe? Unadhani Tanesco ndio wanaolipa kodi au ni wananchi?

Serikali iwadhamini wakope walipe deni!, haya ni mawazo yako au ni mawazo ya bia!

Ili twende sawa lazima turudi nyuma tuulizane kwanza hela zote inazokopa na zile ambazo serikali imetoa kwa miaka mingi, zimepotelea wapi? Kumbuka kila senti inayokopwa wananchi tumeilipa kupitia bili za umeme

mkuu kama hujafanya research usiweke comments kuegemea upande mmoja

kwa kifupi financial difficulties za TANESCO zinachangiwa na
1) SIASA - hii ni pamoja na TANESCO kulazimishwa kuuza umeme kwa bei ndogo kuliko gharama halisi za uzalishaji mfano mzuri ni zanzibar kwa sababu za kimuungano tarriff yao ni gharama yake ni ndogo sana kuliko watumiaji wengine wote
2) UFISADI - hii ni pamoja mikataba mingi hasa ya umeme wa dharura iliyoingiwa na serikali kisha tanesco kulazimishwa kuitekeleza
 
Hakuna cha kuchemsha, mashirika yote ya umma yaliyoshindwa kuendeshwa kifaida na Serikali watu binafsi wameyachukuwa bila ruzuku ya Serikali na wanafanya vizuri tu. Mfano mzuri wa shirika kubwa ni NBC. Ilikuwa ni hasara tupu, sasa tunaona wanalipa kodi nyingi tu. TBL?

mheshimiwa usitetee ubinafsishaji tu ..... hata kama tanesco itabinafsishwa, national grid/ transmission inabidi ibaki serikalini .... hakuna nchi iliyobinafsisha mpaka transmission network na hiyo ni kwa usalama wa taifa .... wewe mwenyewe umeona sasa hivi tumewaachia hao wageni mambo ya gas ambavyo wanatingisha viberiti...gas imepungua, tunafanya ukarabati, etc kisa hawajakubaliana kitu na serikali
 
Na Mhakama ya Biashara mbona huitaji ilitowa hiyo hukumu? na mahakama ya Uingereza ilipopelekwa pingamizi na TNESCO kushindwa tena kisheria mbona huisemi? na Kahakama ya Tanzania kuamua walipwe mbona huisemi?

Sheria ni msumeno. Mitambo unayo halafu useme aliyeleta mwizi? kwanza mlipe halafu funguwa kesi yako kama kakuibia.

Leo mitambo hiyo hiyo ndio inasaidia mgao, ilikuwa inunuliwe yaishe, wenye mitabo badala ya kesi walishakubali kama mnaitaka nunuweni basi, Idrisa akashauri inunuliwe na Zitto Kabwe akashaufri inunuliwe, mijinga fulani ikakataa, sasa gharama zote zinalipwa, kuinunuwa hamjainunuwa, bado mnaikodisha kwa kuwa tu inaonekana sasa ni ya Kimerekani.

Miafrika Ndivyo Ilivyo - Nyani Ngabu

Mkataba wowote ule ulioingiwa kwa njia za udanganyifu na kisha wahusika kushindwa kutimiza masharti ya mkataba ule ya kufua umeme ni mkataba batili. Kama Serikali ingekuwa makini katika kuipanga kesi yake basi TANESCO ingeshinda katika kesi ile lakini wahusika wakuu toka Serikalini walikuwa wameshahesabu mgao wao toka kwa fisadi Rostam Azizi hivyo hawakuhakikisha umakini katika utetezi wa kesi yao dhidi Fisadi Rostam na mwenzie Al Alawi.

Kama Serikali iliweza kupinga hukumu ya kesi yake dhidi ya Valambhia na kukataa kulipa mabilini ya pesa kwa kampuni hiyo. Basi pia Serikali hii DHAIFU ikiwa makini inaweza kabisa kufanya hivyo. Kumbuka pesa hizo zilitakiwa kulipwa tangu December 2010 lakini kutokana na kupinga kwa Watanzania pamoja na hii Serikali DHAIFU kuridhia kulipa pesa hizo hazijalipwa na kama tukiweza kusimamia zislipwe hadi 2015 na CHADEMA kuchukua nchi basi Mafisadi ndani ya Serikali waliokuwa wanaumezea mate mgao wao haramu toka kwa mafisadi Rostam na Al Alawi hawataona hata senti tano toka hazina.

 
Rex Attorneys ni kashfa kubwa zaidi ya Dowans
Godfrey Dilunga

Toleo la 168
12 Jan 2011
RAIA MWEMA

Kuvunjwa mkataba wa Dowans
Msingi wa kuvunjwa mkataba kati ya TANESCO na Dowans ni ushauri wa wanasheria kutoka kampuni ya Rex-Attorneys. Ni Kampuni hii ya kisheria iliyonadiwa bungeni kuwa, imebobea katika masuala ya sheria za kimataifa.

Agosti 28, mwaka 2008, Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda (mwanasheria kitaaluma) aliimwangia sifa kampuni ya Rex-Attorneys bungeni.
Waziri Mkuu alisema; "Kutokana na utata uliojitokeza katika mchakato mzima kuhusu mkataba baina ya TANESCO na Richmond uliotiwa saini tarehe 23 Juni 2006..."
"...Serikali kupitia TANESCO iliamua kufanyike mapitio ya mkataba huo na kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wanasheria waliobobea katika masuala ya mikataba ya kimataifa wa Kampuni ya Rex Attorneys.

Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, uchunguzi wa Rex Attorneys ulibaini mambo matatu aliyoainisha kati ya mengi.
Mosi; manunuzi ya huduma ya umeme na kuingia mkataba na Richmond Development Company LLC ulikiuka Sheria ya Manunuzi wa Umma ya mwaka 2004.

Pili, kutokana na ukiukwaji huo, mkataba baina ya TANESCO na Richmond Development Company LLC, haukuwa halali na hauna nguvu kisheria.

Tatu, hata kama mkataba husika ungekuwa halali, uhamishaji (assignment) wa mkataba huo kutoka RDEVCO badala ya Richmond Development Company LLC kwenda Dowans Holdings S.A. na hatimaye Dowans Tanzania Limited, haukuwa halali.

Yatokanayo na kauli ya Waziri Mkuu
Maelezo hayo ya Waziri Mkuu yanaibua mengi. Kwanza, uamuzi wa kuvunja mkataba haukuwa wa kisiasa.
Si uamuzi uliotokana na shinikizo la kisiasa kama inavyopotoshwa bali ni uamuzi uliojengwa au kufikiwa kutokana na ushauri wa kisheria. Kwa mujibu wa Pinda, ni ushauri kutoka kwa wanasheria wabobeaji.

Pili, kwa kupambanisha hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Kibiashara ya Usuluhishi na maelezo ya Waziri Mkuu hasa katika kuipa sifa za ‘kutukuka' Rex-Attorneys, tunajikuta tukilazimika kuhoji suala moja kati ya mawili au yote mawili na kimsingi tukawa na haki ya kuanza kupuuza upande mmoja kama si pande zote.

Masuala hayo mawili ni pamoja na umakini wa serikali (Waziri Mkuu) hasa kutokana na kuinadi kampuni ya Rex-Attorneys au tuhoji uwezo wa Rex Attorneys.
Hapa izingatiwe ile kauli kuwa serikali "ina mkono mrefu" kama ingeweza kutafiti kwa umakini kama kweli hakuna maslahi binafsi yaliyopiganiwa ili kupiga kumbo maslahi ya nchi.

TANESCO imetakiwa sasa kuilipa Dowans mabilioni kwa kuvunja mkataba na kukataa kulipia huduma za kampuni hiyo kwa TANESCO katika kipindi cha mkataba.
Hukumu hii inatoka katika wakati ambao ushauri wa Rex-Attorneys (wazoefu wa mikataba ya kimataifa) ukiwa katika makabati ya TANESCO.
Fedha zimetumika kununua huduma ya ushauri wa kisheria kutoka Rex-Attorneys. Kampuni hiyo bila shaka, imelipwa mamilioni (kodi za wananchi). Bila shaka, katika kupima thamani ya matumizi ya fedha (value for money) malipo kwa Rex Attorneys ni kashfa.

Na kwa maana hiyo, hasara kwa taifa si tu malipo yatakayofanywa kwa Dowans bali hata kwa kampuni iliyotoa ushauri ‘tasa' wa kisheria.

Ushauri kwa mbunge yeyote makini
Kwa mbunge yeyote makini, ambaye anaweza kujitambua yupo kundi gani la watu kwa mujibu wa mtazamo wa Tully, anaweza kuhoji haya na mengine bungeni.
Ashinikize kuchunguzwa pia kwa Rex Attorneys ambayo ushauri wake umegeuka gharama kwa Taifa. Je, kampuni hii ilitoa ushauri usiongiliwa na maslahi ya pamoja kati ya wamiliki wa Dowans na kampuni husika?

Lakini pia ashinikize uchunguzi wa uhusiano kati ya kampuni hii na viongozi wa serikali, ikiwamo ofisi ya Waziri Mkuu iliyoipamba kampuni hiyo bungeni.
Ikumbukwe, kwa mara nyingine kampuni hii imefuatwa tena baada ya hukumu ya ICC ili kushauri kama Dowans ilipwe au la. Wameshauri ilipwe.
Ni kama vile kampuni hiyo mwanzo ilitoa ushauri wenye malengo ya kuandaa mazingira ya Dowans kushinda kesi na kulipwa.

Katika mazungumzo yake na waandishi wa habari wiki iliyopita, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alisema; "Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO ilishauriwa na kampuni ya Rex Attorneys Advocates kukubaliana na hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Usuluhishi bila kuipinga endapo itasajiliwa kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania."

Hapa, Rex Attorneys ndiyo iliyosifiwa na Waziri Mkuu bungeni, ikatoa ushauri wa kuvunja mkataba. Baada ya kuvunja mkataba, TANESCO ‘imehukumiwa' kulipa mabilioni.
Lakini baada ya hukumu kutoka, TANESCO imerudi kwa kampuni iliyotoa ushauri wa kuvunja mkataba, kampuni hiyo inashauri tena TANESCO ifanye malipo?!

Je, vigezo vya awali vya Rex Attorneys kushauri mkataba uvunjwe vimepotelea wapi hadi wakimbilie kushauri TANESCO ifanye malipo? Je, kuna uhusiano gani au kunaweza kuibuka uhusiano gani kati ya mabilioni itakayolipwa Dowans na kampuni hii ya kisheria? Je, kuna mgawo wa malipo hayo baadaye?

Kwa nini kampuni iliyoshauri kwa vigezo vya kisheria mkataba uvunjwe, baadaye igeuke ikipuuza vigezo hivyo na kutoa ushauri mpya wa kulipa mabilioni? Kwa mbunge makini bila shaka hapa kuna jambo la kuhoji.

Serikali kupitia TANESCO imevunja mkataba kwa ushauri wa kampuni hii, leo inakwenda kulipa faini kwa ushauri pia wa kampuni hii, je, kuna nini?
 
Na Mhakama ya Biashara mbona huitaji ilitowa hiyo hukumu? na mahakama ya Uingereza ilipopelekwa pingamizi na TNESCO kushindwa tena kisheria mbona huisemi? na Kahakama ya Tanzania kuamua walipwe mbona huisemi?

Sheria ni msumeno. Mitambo unayo halafu useme aliyeleta mwizi? kwanza mlipe halafu funguwa kesi yako kama kakuibia.

Leo mitambo hiyo hiyo ndio inasaidia mgao, ilikuwa inunuliwe yaishe, wenye mitabo badala ya kesi walishakubali kama mnaitaka nunuweni basi, Idrisa akashauri inunuliwe na Zitto Kabwe akashaufri inunuliwe, mijinga fulani ikakataa, sasa gharama zote zinalipwa, kuinunuwa hamjainunuwa, bado mnaikodisha kwa kuwa tu inaonekana sasa ni ya Kimerekani.

Miafrika Ndivyo Ilivyo - Nyani Ngabu

mkuu tunatofautiana mara kwa mara ila hapa lazima nikusifu umeongea points kubwa sana
 
Back
Top Bottom