Huyu naye anajipendekeza. Alipokuwa nje ya system alikuwa anapost post kwenye mitandao. Leo vipi tena?
Mkuu...wazungu wa wingereza wana methali yao, wakisema "the lips of righteous teaches many, but fools die for want of wisdom"..
Kina sie, wapenda kujifunza, halitushangazi hili la Kitila...wa, kinyume na kujifunza, watasumbuka na hili, na mengine mengi...
Rais wa awamu ya 3, wakati mmoja akihutubia bunge alitoa kisa cha mlevi, aliekosea,akaingia sehemu ya nyuma ya gari, na kwa vile nyuma hakuna usukano, wala vikanyagio vya kuongeza mwendo, na kusimamisha gari, nakulainisha kubadilisha gea, mlevi aliamini kaibiwa, na akapiga simu polisi akitaarifu juu ya wizi ktk gari lake, na akiomba msaada wa polisi....wakati polisi wakijiandaa kwenda eneo la tukio, wakapokea simu toka kwa mtu huyo huyo, akiwaomba msamaha kwa usumbufu, na kuwataarifu kuwa alipokuwa akipiga simu ya kwanza alikuwa nyuma, sasa kaingia mbele, ameona kila kitu kiko sawa na salama....
..kuishi kwingi(huku ukijifunza),ni kuona mengi na kujua mengi...
Na tumuombee Kitila ktk majukumu yake mapya, na kulijengà taifa