Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,596
- 830,270
Kitengo hiki muhimu sana cha taifa kinaweza kuwa kashfa nyingine kubwa! Hatukuona makali yake hakikusikika popote mpaka waziri mkuu alipoamua kutembeza bakuli kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi lililotokea Bukoba na maeneo mengine ya Tanzania
Hiki kitengo kilipata umaarufu mkubwa enzi za Mzee Mkapa labda kutokana na majanga mengi ya wakati ule lakini pengine na mahitaji ya kisiasa
Kuna maswali mengi kukihusu hiki kitengo
Kiko chini ya wizara gani?
Wafanyakazi wake wanapatikanaje?
Mkurugenzi wake ni nani?
Ofisi zake ziko wapi?
Akaunti zake zikoje? Zinasimamiwa na nani?
Hili tukio la tetemeko linaweza kufumua makaburi yaliyokwisha sahauliwa lakini pia litukumbushe kuwa Tunahitaji kama taifa sasa kuwa na hiki kitengo kinachojitegemea bila mikono ya wanasiasa
Hiki kitengo kilipata umaarufu mkubwa enzi za Mzee Mkapa labda kutokana na majanga mengi ya wakati ule lakini pengine na mahitaji ya kisiasa
Kuna maswali mengi kukihusu hiki kitengo
Kiko chini ya wizara gani?
Wafanyakazi wake wanapatikanaje?
Mkurugenzi wake ni nani?
Ofisi zake ziko wapi?
Akaunti zake zikoje? Zinasimamiwa na nani?
Hili tukio la tetemeko linaweza kufumua makaburi yaliyokwisha sahauliwa lakini pia litukumbushe kuwa Tunahitaji kama taifa sasa kuwa na hiki kitengo kinachojitegemea bila mikono ya wanasiasa