Inasikitisha sana kitengo hiki watu wanajifanya miungu watu na hawawezi kuguswa na mtu yeyeote, sasa Mheshimiwa Rais tunakuomba sana sie wakazi wa Dodoma jiji utusaidie sana maana watu wanaporwa ardhi na kuwapa madalali wauze na hivyo kuwafanya wananchi kujisikia kuwa serikali yao haiwajali.
Tunakuomba utume watu utashangaa misururu ya watu kwa ajili ya kuonana na Mkuu wa kitengo ili kutaka kuondoa kero zao lakini hakuna mafanikio yoyote yale wanayotatuliwa.
Tunakuomba Mheshimiwa mtetezi wa wanyonge ingilia kati wananchi wako tunateseka sana na hawa wanaojimilikisha ofisi za umma kwa ajili ya kupora na kujilimbikizia viwanja vya wananchi wako wanyonge.
Tuliambiwa kuwa hata vibali vya kujenga vitachukua siku saba lakini kuna watu hapa wametembea kuja jiji zaidi ya miezi mitatu na hakuna walilofanikiwa, tafadhali sana wamulikwe na kushughukikiwa haswa.
Tunakuomba utume watu utashangaa misururu ya watu kwa ajili ya kuonana na Mkuu wa kitengo ili kutaka kuondoa kero zao lakini hakuna mafanikio yoyote yale wanayotatuliwa.
Tunakuomba Mheshimiwa mtetezi wa wanyonge ingilia kati wananchi wako tunateseka sana na hawa wanaojimilikisha ofisi za umma kwa ajili ya kupora na kujilimbikizia viwanja vya wananchi wako wanyonge.
Tuliambiwa kuwa hata vibali vya kujenga vitachukua siku saba lakini kuna watu hapa wametembea kuja jiji zaidi ya miezi mitatu na hakuna walilofanikiwa, tafadhali sana wamulikwe na kushughukikiwa haswa.