Kitendawili

Kiby

JF-Expert Member
Nov 16, 2009
6,899
4,623
Nimeulizwa swali ambalo nimeshindwa kulitolea majibu. Hivyo nikaonelea nililete hapa JF, na kwa kua naamini hapa jamvini pana vichwa vilivyojaa hekima kwa kila nyanja jibu litapatikana. Swali lenyewe ni hili: inakuwa je watu wawili wenye status zinazo fanana kwa kila kitu ikiwa ni pamoja na uzito, urefu, group ya damu na hata jinsia, wanaugua malaria iliyofikia level moja mfano wa malaria tatu. Wanapewa dozi ya tiba ya uzito sawa, mmoja anapona na wa pili yake anafariki? Wataalamu wa jf tusaidiane kwa hili.
 
Mtu ni zaidi ya uzito, urefu, group ya damu, jinsia. He is a complex creature. Ndiyo maana kila mtu ni yeye tu (unique) hata kama atafanana kivipi na mwingine. Kuna vitu ambavyo ni vyake tu kati ya hivyo vinavyomuunda huyu mtu. Na kwa sababu ya upekee huo ambao haujirudii, ndiyo maana unakuta kwamba mwitikio wa huyu mtu kwa mazingira mbalimbali ikiwa ni pamoja na magonjwa unatofautiana kati yake na watu wengine. Vivyo hivyo katika kuitikia matibabu kutatofautiana kati ya mtu na mtu. Kwa hiyo sababu ni nyingi sana zikiwemo za kimwili, kimazingira, kisaikolojia, kiimani, nk. nk. nk.
 
Mtu ni zaidi ya uzito, urefu, group ya damu, jinsia. He is a complex creature. Ndiyo maana kila mtu ni yeye tu (unique) hata kama atafanana kivipi na mwingine. Kuna vitu ambavyo ni vyake tu kati ya hivyo vinavyomuunda huyu mtu. Na kwa sababu ya upekee huo ambao haujirudii, ndiyo maana unakuta kwamba mwitikio wa huyu mtu kwa mazingira mbalimbali ikiwa ni pamoja na magonjwa unatofautiana kati yake na watu wengine. Vivyo hivyo katika kuitikia matibabu kutatofautiana kati ya mtu na mtu. Kwa hiyo sababu ni nyingi sana zikiwemo za kimwili, kimazingira, kisaikolojia, kiimani, nk. nk. nk.

.
Ahsante mkuu. Sasa kama ni hivi kuna jitihada zozote kwa wataalamu wa tiba kutengeneza dozi ya kipekee kwa kila mtu maana kila mmoja hafanani na mwingine? Ukizingatia pia kuna ni ukweli usiopingika wa hizi tofauti. Hata dole gumba hakuna linalofanana na mwingine yeyote duniani.
 
Kama vipimo vya kitabibu vote vinafananana, inategemea na jinsi miili yao inavyoyeyusha dawa ile na kuiruhusu kuanza kufanya kazi, na uimara wa mifumo yao vingine vya mwilini kama nervous system, na circulation system. Ndiyo maana watu hao wanaweza kunywa pombe pamoja lakini mmoja wao akalewa mapema sana wakati yule mwingine bado anadai kabisa.
 
Kama vipimo vya kitabibu vote vinafananana, inategemea na jinsi miili yao inavyoyeyusha dawa ile na kuiruhusu kuanza kufanya kazi, na uimara wa mifumo yao vingine vya mwilini kama nervous system, na circulation system. Ndiyo maana watu hao wanaweza kunywa pombe pamoja lakini mmoja wao akalewa mapema sana wakati yule mwingine bado anadai kabisa.

.
Basi kumbe ni vema na sii kosa kwa ile tabia ya watu kutanguliza neno 'nikijaliwa na Mungu nitapona' bila kuwa na uhakika wa asilimia mia kwamba baada ya kumaliza dozi husika nimepona. Pili kumbe tiba ni probabilities. Na ndio maana hospitali zote zina mortuary ambazo hazipo tu kwa ajili ya wale waliocheleweshewa huduma ya tiba bali pia kwa wale dozi husuka imeshindwa kufanya kazi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom