Kitanda chako na mke au mume Wako

Kitanda chako na mke au mume Wako

chopeko

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
1,527
Reaction score
1,113
Habari MMU!
Nina swali moja tu! Tuchukulie umeoa/kuolewa. Je, ni sahihi kutumia kitanda unachotumia na mke/mume wako pamoja na wageni endapo mwenza wako hayupo?
Kwa mfano tuseme wife/husband hayupo na umepata mgeni wa jinsia yako. Ni sahihi kulala naye kitanda kimoja unachotumia na mke/mume wako?


NB: Mgeni anaweza kuwa ndugu yako wa damu au swahiba wako wa karibu.
Tujadili!
 
Kama kweye chumba chenu vya kufichwa vinafichwa, thats just a bed.
Kama nyote watatu mko comfortable na mpango huo hakuna shida
Habari MMU!!
Nina swali moja tu! Tuchukulie umeoa/kuolewa. Je, ni sahihi kutumia kitanda unachotumia na mke/mume wako pamoja na wageni endapo mwenza wako hayupo???
Kwa mfano tuseme wife/husband hayupo na umepata mgeni wa jinsia yako. Ni sahihi kulala naye kitanda kimoja unachotumia na mke/mume wako?


NB: Mgeni anaweza kuwa ndugu yako wa damu au swahiba wako wa karibu.
Tujadili!!!!!!!!
 
Habari MMU!!
Nina swali moja tu! Tuchukulie umeoa/kuolewa. Je, ni sahihi kutumia kitanda unachotumia na mke/mume wako pamoja na wageni endapo mwenza wako hayupo???
Kwa mfano tuseme wife/husband hayupo na umepata mgeni wa jinsia yako. Ni sahihi kulala naye kitanda kimoja unachotumia na mke/mume wako?


NB: Mgeni anaweza kuwa ndugu yako wa damu au swahiba wako wa karibu.
Tujadili!!!!!!!!

Una chumba kimoja tu? Kama una chumba kimoja tu nadhani si tatizo sana but kama una vyumba zaidi ya kimoja, basi si vyema na haistahili kulala na mgeni kwani chumba chenu wewe na mkeo kina heshima yake ati!!
 
Ile ni altare jamaa yangu... siwezi.
ni kweli mkuu ila si mwenza hayupo? mchangiaji wa kwanza kasema it's just a bed!!!! Ila na mimi kwa upande wangu inaniwia vigumu kidogo!!
 
Una chumba kimoja tu? Kama una chumba kimoja tu nadhani si tatizo sana but kama una vyumba zaidi ya kimoja, basi si vyema na haistahili kulala na mgeni kwani chumba chenu wewe na mkeo kina heshima yake ati!!

waweza kuwa na vyumba zaidi ila kwa kumuonea aibu au kumpa kampani unamkaribisha kwa room yako na mwenza!!
 
Hata mim hili swal ni changamoto kwangu naendelea kupata mawazo hapa
 
Nasisitiza Siwezi,

Tofauti na hilo ,binafsi nilisha piga Marufuku kulala kitanda kimoja na Mwanaume mwenzangu.
 
si sahihi hata kidogo acheni kitanda cha ndoa kibaki na heshima zake. kimebeba kila aina na fujo za ndoa jamani.
 
Nooooooo!
Chumba kile ni lazima kipewe heshima yake, haifai hata kupiga stori na mgeni ikiwa kuna sebule or chumba kingine!
Haifai kumpa mtu asiehusika mipangilio na hali ya chumba cha wakubwa!
Ni lazima kuekwe mikakati ya kuenclose siri za chumba!
Kwa mawazo yangu: kuhadithia tu chumba kikoje na mpangilio wake haifai!
Kuna baadhi ya me hujiona wako sahihi pale wanapolalama wake zao ni wachafu na kuelezea hata hali ya chumba chao
...
Kwa kufungia: hata chumba kimeremete kuliko almasi haipaswi kumuingiza mgeni, isipokuwa, hakuna sehemu nyengine!
 
Kwa kweli sio vema kushare kitanda chako na mume/mke na rafiki yako, kwanza chumbani kwako ni sawa na theater (chumba cha upasuaji) huwa hakiingiliki hovyo hovyo na watu ambao sio wahusika, chumba chako ni siri yako na mume/mke wako tu, kinawahusu nyie wawili tu hata housegirl haruhusiwi kuingia wala kufanya usafi huko, ni marufuku jamani. Pale ni chumba special cha operation ya wawili wapendanao. Kwa mimi naheshimu sana chumba changu na mpenzi wangu, no entry kwa yeyote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom