Kitambulisho cha taifa

Kitambulisho cha taifa

kadoda11

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2011
Posts
21,453
Reaction score
20,755
attachment.php



Kitambulisho cha Taifa(Citizen Identity Card).

Nina wiki kama mbili tangu nikabidhiwe.Ambapo sasa ID hiyo sambamba na zingine,natembea nayo 24/7 kwa majivuno na kwa kujiamini kwenye Wallet yangu.

Kuna bandiko hapa Jf mwana-Diaspora mmoja anadai Kitambulisho cha Taifa hakina umuhumu wowote,kwamba hati ya kusafiria(Passport) inatosha kutambulisha Utaifa wake.Je ni kweli Vitambulisho vya Taifa havina umuhimu wowote?,au ni maneno ya mkosaji aliyeukana utanzania na kuzamia huko ughaibuni. Wakuu tupeane uzoefu kuhusu hili.

lawmaina78 tunajua huko ''kwenu'' hii kitu ''muko nayo'' miaka ''mingi''.embu mutupee uzoefu ''yenu'' tafadhari,ukizingatia kwamba kwa hapo nairobi unapo kutana tu na Karao(Askari),iwe Mchana ama Usiku,kauli ya kwanza ni ''embu onyesha sisi ID yako".

sitashangaa karao wa TZ watakapo geuza kosa la kutotembea/kutokuwa na national ID,mradi wa kuwapatia pesa ya bia na nyama choma. Time will tell. LOL

Najua kwa East Africa na kwa Tanzania bara tumechelewa kupata national ID,ila si vibaya tukajadili.
CC Nyugunyugu wa mama Matola Hute Mtimti et al
Nawasilisha.

NB:Wakuu samahani kwa ubora duni wa picha,nimetumia simu ya kichina.
 

Attachments

  • vv.jpg
    vv.jpg
    216.6 KB · Views: 2,875
Nam support diaspora. Inabidi pass zetu ziboreshwe na apewe kila mwananchi. Ziwe na smart card
 
Ni kitambulisho cha Taifa(Citizen Identity Card).Nina wiki kama mbili tangu nikabidhiwe.Ambapo sasa ID hiyo sambamba na zingine,natembea nayo 24/7 kwa majivuno na kwa kujiamni kwenye Wallet yangu.
Kuna bandiko hapa Jf mwana-Diaspora mmoja anadai Kitambulisho cha Taifa hakina umihumu wowote,kwamba hati ya kusafiria(Passport) inatosha kutambulisha Utaifa wake.Je ni kweli Vitambulisho vya Taifa havina umuhimu wowote?,au ni maneno ya mkosaji aliyeukana utanzania na kuzamia huko ughaibuni.wakuu tupeane uzoefu kuhusu hili. lawmaina78 tunajua huko ''kwenyu'' hii kitu ''mukonayo'' miaka ''mingi''.embu mutupee uzoefu ''yenyu'' tafadhari,ukizingatia kwamba kwa hapo nairobi unapo kutana tu na Karao(Askari),iwe Mchana ama Usiku,kauli ya kwanza ni ''embu onyesha sisi ID yako".
sitashangaa karao wa tz watakapo geuza kosa la kutotembea/kutokuwa na national ID,mradi wa kuwapatia pesa ya bia na nyama choma.time will tell.LOL

Najua kwa East Africa na kwa Tanzania bara tumechelewa kupata national ID,ila si vibaya tukajidili.
CC Nyugunyugu wa mama Matola Hute Mtimti et al
Nawasilisha.

NB:wakuu samahani kwa ubora duni wa picha,nimetumia simu ya kichina.

Dah! hili halina mjadala, jameni kitambulisho cha taifa ni fahari ya kila mwananchi. Kinakupa mwamko mpya kujihusu na kuhusu nchi yako. Kinakufanya unahisi kuwa connected na raia wengine wote. Hii ndio mojawapo ya sababu Wakenya huwa tunajivunia Ukenya na uraia wetu.
Tatizo Bongo ni kuwa, mpo sana taratibu (slow) kwa kila kitu halafu hatimaye huwa mnajikuta kufanya kile mlichokataa.

Sisi tayari sasa tupo kwenye michakato ya ku-digitilize kitambulisho cha taifa, kiasi kwamba Mkenya hatakuwa na haja ya kuelezea majina yake upya kila akihitaji huduma iwe chuo, hospitali n.k. Yaani central database itakuwa na taarifa zetu sote.

Afu, wafahamishe NIDA warekebishe hicho kitambulisho chako, neno gender kwa Kiswahili ni Jinsia sio Jinsi
 
Nina passport, birth certificate, I'd ya kupigia kura, ID ya kazi, Driving license, etc. hebu nidadavudie umuhimu wake zaidi ya hvyo nlivyovitaja!
 
Kina umuhimu sana, ukisikia mtu anasema hakina umuhimu mwekee walakini eitha ni operation kimbunga ama ni wale wanaojifanya kuishi huko nje kwa hiyo wanaona eti wanataka vitambulisho portable mara sijui viwe na smart phone ndani yake
 
Kina umuhimu sana, ukisikia mtu anasema hakina umuhimu mwekee walakini eitha ni operation kimbunga ama ni wale wanaojifanya kuishi huko nje kwa hiyo wanaona eti wanataka vitambulisho portable mara sijui viwe na smart phone ndani yake

hahaha itakuwa ni wale waliojilipua.
 
Nina passport, birth certificate, I'd ya kupigia kura, ID ya kazi, Driving license, etc. hebu nidadavudie umuhimu wake zaidi ya hvyo nlivyovitaja!

kila id ina umuhimu kutegemeana na nafasi yake.
 
lawmaina78
asante kwa post yako.
hakuna ubishi kwamba tumechelewa kupata national ID,inasemekana uchelewaji ulitokana na vita ya wakubwa kugombania tender .enzi za mkapa,watu walipiga siasa,zoezi likakwama.angalau ktk msimu wa JK,moja ya vitu tutakavyomkumbuka navyo ni kusimamia kwa dhati upatikanaji wa national ID.
kuhusu kuji-digitize hilo ondoa shaka.hata sisi tunafika huko soon.mchakato bado unaendelea.hapo kwenye "jinsi" sina hakika sana kama upo sahihi,ila nitacheki kwenye dictionary,nikiona walakini nitalifikisha NIDA.
 
Last edited by a moderator:
View attachment 178510


Kitambulisho cha Taifa(Citizen Identity Card).
Nina wiki kama mbili tangu nikabidhiwe.Ambapo sasa ID hiyo sambamba na zingine,natembea nayo 24/7 kwa majivuno na kwa kujiamini kwenye Wallet yangu.

Kuna bandiko hapa Jf mwana-Diaspora mmoja anadai Kitambulisho cha Taifa hakina umuhumu wowote,kwamba hati ya kusafiria(Passport) inatosha kutambulisha Utaifa wake.Je ni kweli Vitambulisho vya Taifa havina umuhimu wowote?,au ni maneno ya mkosaji aliyeukana utanzania na kuzamia huko ughaibuni. Wakuu tupeane uzoefu kuhusu hili.

lawmaina78 tunajua huko ''kwenu'' hii kitu ''muko nayo'' miaka ''mingi''.embu mutupee uzoefu ''yenu'' tafadhari,ukizingatia kwamba kwa hapo nairobi unapo kutana tu na Karao(Askari),iwe Mchana ama Usiku,kauli ya kwanza ni ''embu onyesha sisi ID yako".

sitashangaa karao wa TZ watakapo geuza kosa la kutotembea/kutokuwa na national ID,mradi wa kuwapatia pesa ya bia na nyama choma. Time will tell. LOL

Najua kwa East Africa na kwa Tanzania bara tumechelewa kupata national ID,ila si vibaya tukajadili.
CC Nyugunyugu wa mama Matola Hute Mtimti et al
Nawasilisha.

NB:Wakuu samahani kwa ubora duni wa picha,nimetumia simu ya kichina.

kadoda nimeona kidole chako na kiatu chako nimeshakujua, kumbe ni wewe..........
 
mbona haina mahali ya signature, na kuonesha mahali anapoishi mwenye id hiyo..na wapi kimetolewa.mimi naona kiko too local
 
mbona haina mahali ya signature, na kuonesha mahali anapoishi mwenye id hiyo..na wapi kimetolewa.mimi naona kiko too local

details za mahali ninapo ishi,signature,finger print etc wanazo wizara ya mambo ya ndani chini ya NIDA.kwa hivyo kilivyo mi naona ni poa tu.

NB :hapo juu kabisa nilipo ziba kwa alama nyeusi,pana special code #.incase hiyo code # ikachukuliwa na kwenda kuingizwa kwenye system ya NIDA,ita provide info zote za muhusika.
 
Dah! hili halina mjadala, jameni kitambulisho cha taifa ni fahari ya kila mwananchi. Kinakupa mwamko mpya kujihusu na kuhusu nchi yako. Kinakufanya unahisi kuwa connected na raia wengine wote. Hii ndio mojawapo ya sababu Wakenya huwa tunajivunia Ukenya na uraia wetu.
Tatizo Bongo ni kuwa, mpo sana taratibu (slow) kwa kila kitu halafu hatimaye huwa mnajikuta kufanya kile mlichokataa.

Sisi tayari sasa tupo kwenye michakato ya ku-digitilize kitambulisho cha taifa, kiasi kwamba Mkenya hatakuwa na haja ya kuelezea majina yake upya kila akihitaji huduma iwe chuo, hospitali n.k. Yaani central database itakuwa na taarifa zetu sote.

Afu, wafahamishe NIDA warekebishe hicho kitambulisho chako, neno gender kwa Kiswahili ni Jinsia sio Jinsi
Walichoandika ni sex in Swahili Ni jinsi... Gender Ni njisia wapo sahihi nida.. Big up nida maimu, makami,bathowond,R.Is,data entry mnafanya kazi nzur sana..I used to be there
 
Kina umuhimu sana, ukisikia mtu anasema hakina umuhimu mwekee walakini eitha ni operation kimbunga ama ni wale wanaojifanya kuishi huko nje kwa hiyo wanaona eti wanataka vitambulisho portable mara sijui viwe na smart phone ndani yake

Umuhimu wake nini tofauti na ID zingine?
 
Walichoandika ni sex in Swahili Ni jinsi... Gender Ni njisia wapo sahihi nida.. Big up nida maimu, makami,bathowond,R.Is,data entry mnafanya kazi nzur sana..I used to be there

asante sana mkuu kwa jibu lako kihusu jinsi na jinsia.sina shaka mtani lawmaina78 ameridhika na jibu.

sex =jinsi
gender =jinsia.

kiswahili ukikifahamu raha sana.
 
Last edited by a moderator:
Umuhimu wake nini tofauti na ID zingine?

1. Kitabulisho cha Taifa kitakumbulisha uraia
wako na shughuli zako za kila siku. Kitasaidia
mamlaka mbalimbali kujua uhalali wa
shughuli zako na mchango wako katika pato
la Taifa. Aidha hata ukiwa nje ya nchi
unaweza kukitumia kujitambulisha endapo
utapata matatizo yo yote ikiwa ni pamoja na
kupotelewa na passport yako. Kitambulisho
cha Taifa kitakuwezesha kushiriki katika
shughuli mbalimbali za kijamii na
kimaendeleo nchini bila kutiliwa shaka na
mtu ye yote. Kitambulisho cha Taifa ni cha
KUDUMU! Kitambulisho cha Taifa hakiwezi
kutumika kama hati ya kusafiria (PASSPORT)!

2. Hati ya kusafiria (Passport) itakuwezesha
wewe kusafiri mahala po pote duniani na pia
kukuwezesha wewe kuomba kutembelea,
kufanya kazi au kukaa katika nchi yo yote
duniani. Pamoja na kwamba passport
inaonyesha uraia wako lakini matumizi yake
ni ya MUDA MAALUM! Kwa maneno mengine
ina UKOMO WA MATUMIZI! Aidha PASSPORT
zinatolewa kulingana na hadhi ya msafiri au
madhumuni ya safari. Hivyo kuna hati za
kawaida ambazo hutolewa kwa kila mtu;
kuna hati za kibalozi ambazo ukisafiri
unaweza kuruka baadhi ya taratibu zikiwemo
za ukaguzi; kuna hati za watu mashuhuri
ambazo zitakuwezesha wewe kupata huduma
maalum kama vile ulinzi n.k.

www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/397659-kitambulisho-cha-taifa-passport-nini-cha-muhimu-zaidi.html
 
mbona haina mahali ya signature, na kuonesha mahali anapoishi mwenye id hiyo..na wapi kimetolewa.mimi naona kiko too local
Bank pia hawavipokei kwa vile havina sign,ni deal la wachache ila labda wenzetu wa mataifa mengine watufahamishe kama huwa havinaga sahihi,ila mbona walitusainisha?zimeenda wapi sahihi zetu?daaa ni ndio tz
 
Bank pia hawavipokei kwa vile havina sign,ni deal la wachache ila labda wenzetu wa mataifa mengine watufahamishe kama huwa havinaga sahihi,ila mbona walitusainisha?zimeenda wapi sahihi zetu?daaa ni ndio tz
vya nje vingi vina sign mkuuila mleta mada hii anasema kuna code sijui mpaka ingizwe kwa system ndiyo wataiona na details zaidi khsu mwenye kadi....lakini za wwnzetu sign ipo ..national id ya tz haina maelezo mengi
 
Back
Top Bottom