Marekani anaugomvi na Jordan? ana ugomvi na Oman? ana ugomvi na Iraq leo baada ya kuondoka Saddam? Ana ugomvi na Misri? au Yemeni amewahi kuwa na ugomvi nao? Saudi Arabia je? Au Kuwait
tusikuze mambo.
Hapo Uarabuni Marekani kwa sasa, narudia kwa sasa, ana ugomvi na Iran sababu viongozi wake wamekuwa vichwa ngumu, kabla ya mwaka 1989 Iran palikuwa kama sebureni kwa marekani, walikuwa na uswahiba mkubwa sababu walikuwa na rais hajielewielewi.
Haya mambo ya Nuclear ni uzushi tu, marekani ndio aliyewafundisha Iran mambo ya Nuclear mpaka alipoondoshwa shah, utasema marekani ana ugomvi na Taifa zima?
viongozi wa sasa wa Iran walikuwapo wakati wa utawala wa Obama, wakaingia makubaliano 2015 wingu la utulivu likashuka chini, kaja huyu kichaa you see what is happening, yaani hata kusema Taifa la Marekani linaugomvi na Taifa fulani ni uzushi pia.
Mkuu.
Ebu kamsome vema mmarekani nadhani humtambui vema.
Kabla ya hayo makubaliano 2015 je Obama alikua na uswahiba na Rouhani ?!!
Jibu laaah.
Obama mwaka 2011 alipeleka drone nne Iran kwa lengo lake baya lakini zikashushwa.
Akapeleka makomando wanamaji Iran wakakamatwa kabla hawajafanya uvamizi wa siri.
Je hivi ndivyo mataifa yanayokua na uswahiba yalivyo?!
Baada ya kuona ameshindwa kuiingia Iran huyo Obama wako akaona bora waingie mikataba ya amani sasa ya JCPOA.
Lakini kabla ya hapo walikua na uhasama vema tu.
US ana sera yake ya "no permanent friend no permanent enemy".
Yani hatokua rafiki wako wa kudumu na hatokua adui wako wa kudumu.
US ukifanya anavyotaka basi utakua na amani,yani atataka akuendeshe anyonye maliasili zako km wanavyofanyiwa hayo mataifa ulioyataja.
Lakini ukijielewa na kupingana nao umekwisha.
Nchi nyingi Afghanistan,Pakistan,Iraq kaziharibu yeye.
Hao Oman,Saudiarabia siku zao zinahesabika.
Halafu kama US ana ugomvi na kiongozi peke ake basi asingeiharibu Syria na Iraq kama vile.
Ukiwa na chuki kwa kiongozi wa taifa lenye kushikamana basi unalichukia ama una ugomvi na taifa zima.